< Mwanzo 22 >

1 Ikawa kwamba baada ya mambo hayo Mungu akampima Abraham. Akamwambia, “Abraham!” Abraham akasema, “Mimi hapa.”
And aftir that these thingis weren don, God assaiede Abraham, and seide to hym, Abraham! Abraham! He answerde, Y am present.
2 Kisha Mungu akasema, “Mchukue mwanao, mwanao wa pekee, umpendaye, Isaka, na uende katika nchi ya Moria. Mtoe kama sadaka ya kuteketezwa mahali pale juu ya moja ya milima hiyo, ambayo nitakwambia.”
God seide to him, Take thi `sone oon gendrid, whom thou louest, Ysaac; and go into the lond of visioun, and offre thou hym there in to brent sacrifice, on oon of the hillis whiche Y schal schewe to thee.
3 Kwa hiyo Abraham akaamka asubuhi na mapema, akatandika punda wake, akawachukuwa vijana wake wawili, pamoja na Isaka mwanawe. Akakata kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, kisha akapanga safari kwenda mahali ambapo Mungu alimwambia.
Therfor Abraham roos bi niyt, and sadlide his asse, and ledde with hym twey yonge men, and Ysaac his sone; and whanne he hadde hewe trees in to brent sacrifice, he yede to the place which God hadde comaundid to him.
4 Siku ya tatu Abraham akatazama juu na akaona mahali pakiwa mbali.
Forsothe in the thridde dai he reiside hise iyen, and seiy a place afer;
5 Abraham akawambia vijana wake, “kaeni hapa pamoja na punda, mimi pamoja na Isaka tutakwenda pale. Tutaabudu na kisha tutarudi hapa penu.”
and he seide to hise children, Abide ye here with the asse, Y and the child schulen go thidur; and aftir that we han worschipid, we schulen turne ayen to you.
6 Ndipo Abraham akachukua kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa akaziweka juu ya Isaka mwanawe. Mkononi mwake akachukua moto na kisu; na wote wawili wakaondoka pamoja.
And he took the trees of brent sacrifice, and puttide on Ysaac his sone; forsothe he bar fier, and a swerd in hise hondis. And whanne thei tweyne yeden togidere, Isaac seide to his fadir, My fadir!
7 Isaka akazungumza na Abraham baba yake akisema, “Baba yangu,” naye akasema, “Ndiyo mwanangu.” Akasema, “Tazama huu ni moto na kuni, lakini yuko wapi mwanakondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa?”
And he answerde, What wolt thou, sone? He seide, Lo! fier and trees, where is the beeste of brent sacrifice?
8 Abraham akasema, “Mungu mwenyewe atatupatia mwanakondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, mwanangu.” Kwa hiyo wakaendelea, wote wawili pamoja.
Abraham seide, My sone, God schal puruey to hym the beeste of brent sacrifice.
9 Walipofika mahali ambapo Mungu alikuwa amemwambia, Abraham akajenga madhabahu pale na akaweka kuni juu yake. Kisha akamfunga Isaka mwanawe, na akamlaza juu ya madhabahu, juu ya zile kuni.
Therfor thei yeden to gidere, and camen to the place whiche God hadde schewid to hym, in which place Abraham bildide an auter, and dresside trees a boue; and whanne he hadde bounde to gidere Ysaac, his sone, he puttide Ysaac in the auter, on the heep of trees.
10 Abraham akanyoosha mkono wake akachukua kisu ili kumuua mwanawe.
And he helde forth his hond, and took the swerd to sacrifice his sone.
11 Ndipo malaika wa Yahwe akamwita kutoka mbinguni na kusema, “Abraham, Abraham!” naye akasema, “Mimi hapa.”
And lo! an aungel of the Lord criede fro heuene, and seide, Abraham! Abraham!
12 Akasema, “usinyooshe mkono wako juu ya kijana, wala usifanye jambo lolote kumdhuru, kwa kuwa sasa najua unamcha Mungu, kwa kuona kuwa hukumzuilia mwanao, mwanao wa pekee, kwa ajili yangu.”
Which answerde, I am present. And the aungel seide to hym, Holde thou not forth thin honde on the child, nether do thou ony thing to him; now Y haue knowe that thou dredist God, and sparidist not thin oon gendrid sone for me.
13 Abraham akatazama juu na tazama, nyuma yake kulikuwa na kondoo mume amenaswa pembe zake kichakani. Abraham akaenda akamchukua kondoo na akamtoa kama sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
Abraham reiside hise iyen, and he seiy `bihynde his bak a ram cleuynge bi hornes among breris, which he took, and offride brent sacrifice for the sone.
14 Kwa hiyo Abraham akapaita mahali pale, Yahwe atatoa,” na panaitwa hivyo hata leo. “Juu ya mlima wa Yahwe itatolewa.”
And he clepide the name of that place, The Lord seeth; wherfore it is seyd, til to dai, The Lord schal see in the hil.
15 Malaika wa Yahwe akamwita Abraham kwa mara ya pili kutoka mbinguni
Forsothe the aungel of the Lord clepide Abraham the secounde tyme fro heuene,
16 na kusema - Hiki ni kiapo cha Yahwe, “Kwa ajili ya nafsi yangu nimeapa kwamba kwa kuwa umefanya jambo hili, na hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,
and seide, The Lord seith, Y haue swore bi my silf, for thou hast do this thing, and hast not sparid thin oon gendrid for me,
17 hakika nitakubariki na nitakuzidishia uzao wako kama nyota za angani, na kama mchanga ulioko kwenye ufukwe wa bahari; na uzao wakowatamiliki lango la adui zao.
Y schal blesse thee, and Y schal multiplie thi seed as the sterris of heuene, and as grauel which is in the brynk of the see; thi seed schal gete the yatis of hise enemyes;
18 Kupitia uzao wako mataifa yote ya dunia watabarikiwa, kwa sababu umetii sauti yangu.”
and alle the folkis of erthe schulen be blessid in thi seed, for thou obeiedist to my vois.
19 Kwa hiyo Abraham akarejea kwa vijana wake, na wakaondoka wakaenda pamoja Beerisheba, hivyo akakaa Beerisheba.
Abraham turnede ayen to hise children, and thei yeden to Bersabee to gidere, and he dwellide there.
20 Ikawa kwamba baada ya mambo haya ambayo Abraham aliambiwa, “Milka amemzalia pia watoto, ndugu yako Nahori.”
And so whanne these thingis weren don, it was teld to Abraham that also Melcha hadde bore sones to Nachor his brother;
21 Hawa walikuwa ni Usi mzaliwa wa kwanza, Busi ndugu yake, Kemueli aliye mzaa Aramu,
Hus the firste gendrid, and Buz his brothir, and Chamuhel the fadir of Sireis,
22 Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu, na Bethueli.
and Cased, and Asan, and Feldas,
23 Bethuel akamzaa Rebeka. Hawa walikuwa ni wale watoto wanane ambao Milka alizaa kwa Nahori, ndugu yake na Abraham.
and Jedlaf, and Batuhel, of whom Rebecca was borun; Melcha childide these eiyte to Nachor brother of Abraham.
24 Suria wake, ambaye aliitwa Reuma, pia akamzaa Teba, Gahamu, Tahashi, na Maaka.
Forsothe his concubyn, Roma bi name, childide Thabee, and Gaon, and Thaas, and Maacha.

< Mwanzo 22 >