< Mwanzo 21 >
1 Yahwe akamsikiliza Sara kwa umakini kama alivyo kuwa amemwambia, Yahwe akamfanyia Sara kama alivyo kuwa amemwahidi.
And the Lord visited Sara, as he had promised: and fulfilled what he had spoken.
2 Sara akachukua mimba na akamzalia Abraham mtoto wa kiume katika uzee wake, katika muda ule ule ambao Mungu alikuwa amemwambia.
And she conceived and bore a son in her old age, at the time that God had foretold her.
3 Abraham akamwita jina mwanawe, ambaye alizaliwa kwake, na Sara, Isaka.
And Abraham called the name of his son, whom Sara bore him, Isaac.
4 Abraham akamtahiri mwanawe Isaka alipofikisha siku nane, kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza.
And he circumcised him the eighth day, as God had commanded him,
5 Abraham alikuwa na umri wa miaka mia moja wakati mwanawe Isaka anazaliwa kwake.
When he was a hundred years old: for at this age of his father was Isaac born.
6 Sara akasema, “Mungu amenifanya nicheke; kila mtu atakaye sikia atacheka pamoja na nami.”
And Sara said: God hath made a laughter for me: whosoever shall hear of it will laugh with me.
7 Pia akasema, “Nani angesema kwa Abraham kwamba Sara atalea mtoto, na sasa kweli nimemzalia mtoto wakiume katika uzee wake!”
And again she said: Who would believe that Abraham should hear that Sara gave suck to a son, whom she bore to him in his old age.
8 Mtoto akakua na akaachishwa kunyonya, na Abraham akafanya sherehe kubwa katika siku ambayo Isaka aliachishwa.
And the child grew and was weaned: and Abraham made a great feast on the day of his weaning.
9 Sara akamwona mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alikuwa amezaliwa kwa Abraham, akidhihaki.
And when Sara had seen the son of Agar the Egyptian playing with Isaac her son, she said to Abraham:
10 Kwa hiyo akamwambia Abraham, “Mfukuze huyu mwanamke huyu mtumwa pamoja na mtoto wake: kwa kuwa mtoto huyu wa mwanamke mtumwa hawezi kuwa mrithi pamoja na mwanangu Isaka.”
Cast out this bondwoman, and her son: for the son of the bondwoman shall not be heir with my son Isaac.
11 Jambo hili likamuhuzunisha sana Abraham kwa sababu ya mwanawe.
Abraham took this grievously for his son.
12 Lakini Mungu akamwambia Abraham, “Usihuzunike kwa sababu ya kijana huyu, na kwa sababu ya mwanamke huyu mtumwa wako. Sikiliza maneno asemayo Sara juu ya jambo hili, kwa sababu itakuwa kupitia Isaka kwamba uzao wako utaitwa.
And God said to him: Let it not seem grievous to thee for the boy, and for thy bondwoman: in all that Sara hath said to thee, hearken to her voice: for in Isaac shall thy seed be called.
13 Nitamfanya pia mtoto wa mjakazi kuwa taifa, kwa sababu ni uzao wako.”
But I will make the son also of the bondwoman a great nation, because he is thy seed.
14 Abraham akaamka asubuhi na mapema, akachukua mkate na kiriba cha maji, akampatia Hajiri, akiweka juu ya bega lake. Akamtoa kijana akampatia Hajiri na akawaondoa. Hajiri akaondoka akapotea katika jangwa la Beerisheba.
So Abraham rose up in the morning, and taking bread and a bottle of water, put it upon her shoulder, and delivered the boy, and sent her away. And she departed, and wandered in the wilderness of Bersabee.
15 Maji yalipokwisha kwenye kiriba akamtelekeza kijana katika moja ya vichaka.
And when the water in the bottle was spent, she cast the boy under one of the trees that were there.
16 Kisha akaondoka, na akakaa umbali kidogo na yule kijana, umbali kama wa kutupa mshale, kwa vile alisema, “Na nisitazame kifo cha mtoto.” Alipokuwa amekaa kumkabili, akapaza sauti yake akalia.
And she went her way, and sat over against him a great way off as far as a bow can carry, for she said: I will not see the boy die: and sitting over against, she lifted up her voice and wept.
17 Mungu akasikia kilio cha kijana, na malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, “Nini kinakusumbua? Usiogope, kwa kuwa Mungu amesikia kilio cha kijana mahali alipo.
And God heard the voice of the boy: and an angel of God called to Agar from heaven, saying: What art thou doing, Agar? fear not: for God hath heard the voice of the boy, from the place wherein he is.
18 Inuka msimamishe mtoto, na umtie moyo; kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa.”
Arise, take up the boy, and hold him by the hand: for I will make him a great nation.
19 Kisha Mungu akayafunua macho ya Hajiri, natazama akaona kisima cha maji. Akaenda akajaza kiriba maji, na akampatia kijana akanywa.
And God opened her eyes: and she saw a well of water, and went and filled the bottle, and gave the boy to drink.
20 Mungu akawa pamoja na kijana, na akakua. Akaishi jangwani akawa mwindaji.
And God was with him: and he grew, and dwelt in the wilderness, and became a young man, an archer.
21 Akaishi katka jangwa la Parani, na mama yake akampatia mke kutoka Misri.
And he dwelt in the wilderness of Pharan, and his mother took a wife for him out of the land of Egypt.
22 Ikawa kwamba katika wakati ule Abimeleki na Fikoli kamanda wa jeshi lake akamwambia Abraham, akisema, “Mungu yuko pamoja na wewe katika yote uyatendayo.
At the same time Abimelech, and Phicol the general of his army said to Abraham: God is with thee in all that thou dost.
23 Sasa niapie kwa Mungu kwamba hutanifanyia baya, wala mwanangu, wala uzao wangu. Onesha kwangu na kwa nchi ambayo umekuwa ukikaa agano lile lile la uaminifu ambalo nimekuonesha wewe.”
Swear therefore by God, that thou wilt not hurt me, nor my posterity, nor my stock: but according to the kindness that I have done to thee, thou shalt do to me, and to the land wherein thou hast lived a stranger.
24 Abraham akasema, “Nina apa.”
And Abraham said: I will swear.
25 Abraham pia akamlalamikia Abimeleki kuhusu kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki wamekinyang'anya.
And he reproved Abimelech for a well of water, which his servants had taken away by force.
26 Abimeleki akasema, “Sijui ni nani amefanya jambo hili. Hukuniambia mapema; na sijalisikia ila leo hii.”
And Abimelech answered: I knew not who did this thing: and thou didst not tell me, and I heard not of it till today.
27 Kwa hiyo Abraham akachukua kondoo na ng'ombe maksai akampatia Abimeleki, na wawili hawa wakafanya agano.
And Abraham took sheep and oxen and gave them to Abimelech: and both of them made a league.
28 Kisha Abraham akatenga wanakondoo wa kike saba pekeyao.
And Abraham set apart seven ewe lambs of the flock.
29 Abimeleki akamwambia Abraham, “Nini maana ya hawa wanakondoo wa kike saba ambao umewatenga pekeyao?”
And Abimelech said to him: What mean these seven ewe lambs which thou hast set apart?
30 Akajibu, “Hawa wanakondoo wa kike saba utawapokea kutoka mkonono mwangu, ili kwamba uwe ushahidi kwangu, kuwa nichimba kisima hiki.”
But he said: Thou shalt take seven ewe lambs at my hand: that they may be a testimony for me, that I dug this well.
31 Kwa hiyo akaita mahali pale Beerisheba, kwa sababu mahali pale wote wawili wali apa kiapo.
Therefore that place was called Bersabee: because there both of them did swear.
32 Walifanya agano hapo Bersheba, kisha Abimeleki na Fikoli, amiri wa jeshi, wakarudi katika nchi ya Wafilisti.
And they made a league for the well of oath.
33 Abraham akapanda mti wa mkwaju katika Beerisheba. Na pale akamwabudu Yahwe, Mungu wa milele.
And Abimelech, and Phicol the general of his army arose and returned to the land of the Palestines. But Abraham planted a grove in Bersabee, and there called upon the name of the Lord God eternal.
34 Abraham akasalia kuwa mgeni katika nchi ya Wafilisti kwa siku nyingi.
And he was a sojourner in the land of the Palestines many days.