< Mwanzo 2 >
1 Kisha mbingu na nchi zilimalizika, na viumbe hai vyote vilivyo jaza mbingu na nchi.
Les cieux, la terre et toute leur étendue furent achevés.
2 Siku ya saba Mungu alifikia mwisho wa kazi yake ambayo aliifanya, na kwa hiyo alipumzika siku ya saba kutoka kwenye kazi yake yote.
Le septième jour, Dieu acheva l'œuvre qu'il avait faite, et il se reposa au septième jour de toute son œuvre.
3 Mungu akaibarikia siku ya saba na akaitakasa, kwa sababu katika siku hiyo alipumzika kutoka kwenye kazi yake yote ambayo aliifanya katika uumbaji.
Dieu bénit le septième jour et le sanctifia, parce qu'il se reposa en ce jour de toute l'œuvre de la création qu'il avait faite.
4 Haya yalikuwa ni matukio yahusuyo mbingu na nchi, wakati vilipoumbwa, katika siku ambayo Yahwe Mungu aliumba nchi na mbingu.
Voici l'histoire des générations des cieux et de la terre, quand ils furent créés, au jour où Yahvé Dieu fit la terre et les cieux.
5 Hapakuwa na msitu wa shambani uliokuwa katika nchi, na hapakuwa na mmea wa shambani uliokuwa umechipuka, kwa kuwa Yahwe Mungu alikuwa hajasababisha mvua kunyesha juu ya nchi, na hapakuwa na mtu wa kulima ardhi.
Aucune plante des champs n'était encore sur la terre, et aucune herbe des champs n'avait encore poussé, car Yahvé Dieu n'avait pas fait pleuvoir sur la terre. Il n'y avait pas d'homme pour cultiver la terre,
6 Lakini ukungu uliinuka juu kutoka kwenye nchi na kuutia maji uso wote wa ardhi.
mais une brume montait de la terre et arrosait toute la surface du sol.
7 Yahwe Mungu aliumba mtu kutoka mavumbi ya ardhi, na akampulizia puani pumzi ya uhai, na mtu akawa kiumbe hai.
Yahvé Dieu forma l'homme de la poussière de la terre, il souffla dans ses narines une haleine de vie, et l'homme devint un être vivant.
8 Yahwe Mungu aliotesha bustani upande wa mashariki, katika Edeni, na pale akamuweka mtu ambaye alimuumba.
Yahvé Dieu planta un jardin à l'orient, en Éden, et il y mit l'homme qu'il avait formé.
9 Kutoka ardhini Yahwe Mungu alifanya kila mti uote ambao unapendeza na ni mzuri kwa chakula. Hii ni pamoja na mti wa uzima ambao ulikuwa katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.
Yahvé Dieu fit pousser du sol tous les arbres agréables à la vue et bons à manger, y compris l'arbre de vie au milieu du jardin et l'arbre de la connaissance du bien et du mal.
10 Mto ukatoka nje ya Edeni kuitia maji bustani. Na kutoka pale ukagawanyika na kuwa mito minne.
Un fleuve sortait d'Eden pour arroser le jardin; de là, il se divisait et devenait la source de quatre fleuves.
11 Jina la ule wa kwanza ni Pishoni. Huu ni ule ambao unatiririka kupitia nchi yote ya Havila, ambapo kuna dhahabu.
Le nom du premier est Pishon; il coule dans tout le pays de Havila, où il y a de l'or;
12 Dhahabu ya inchi ile ni nzuri. pia kuna bedola na jiwe shohamu.
et l'or de ce pays est bon. On y trouve aussi du bdellium et de la pierre d'onyx.
13 Jina la mto wa pili ni Gihoni. Huu unatiririka kupitia nchi yote ya kushi.
Le nom du second fleuve est Gihon. C'est le même fleuve qui coule dans tout le pays de Cusch.
14 Jina la mto wa tatu ni Hidekeli, ambao unatiririka mashariki mwa Ashuru. Mto wa nne ni Frati.
Le nom du troisième fleuve est Hiddékel. C'est celui qui coule devant l'Assyrie. Le quatrième fleuve est l'Euphrate.
15 Yahwe Mungu alimtwaa mtu na kumweka ndani ya bustani ya Edeni kuilima na kuitunza.
Yahvé Dieu prit l'homme et le plaça dans le jardin d'Eden pour le cultiver et le garder.
16 Yahwe Mungu alimuagiza mtu akisema, “kutoka kwenye kila mti bustanini waweza kula kwa uhuru.
Yahvé Dieu donna cet ordre à l'homme: « Tu peux manger librement de tous les arbres du jardin;
17 Lakini kutoka kwenye mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa kuwa siku utakayo kula kutoka katika mti huo, utakufa hakika.”
mais tu ne mangeras pas de l'arbre de la connaissance du bien et du mal, car le jour où tu en mangeras, tu mourras. »
18 Kisha Yahwe Mungu akasema, “siyo jambo jema kwamba mtu huyu lazima awe pekeyake. Nitamfanyia msaidizi anaye mfaa.”
Yahvé Dieu dit: « Il n'est pas bon que l'homme soit seul. Je vais lui faire une aide qui lui soit comparable. »
19 Kutoka ardhini Yahwe Mungu akafanya kila mnyama wa kondeni na kila ndege wa angani. Kisha akawaleta kwa mtu huyu aone angewapatia majina gani. Jina ambalo mtu huyu alimwita kila kiumbe hai, hili ndilo lilikuwa jina lake.
Yahvé Dieu forma de la terre tous les animaux des champs et tous les oiseaux du ciel, et il les amena à l'homme pour voir comment il les appellerait. Le nom que l'homme donna à chaque être vivant devint son nom.
20 Mtu huyu akawapatia majina wanyama wote, ndege wote wa angani, na kila mnyama wa mwitu. Lakini kwa mtu mwenyewe hapakuwa na msaidizi wa kumfaa yeye.
L'homme donna des noms à tout le bétail, aux oiseaux du ciel et à tous les animaux des champs; mais il ne fut pas trouvé pour l'homme un auxiliaire comparable à lui.
21 Yahwe Mungu akaleta usingizi mzito kwa mtu huyu, kwa hiyo mtu huyu akalala. Yahwe Mungu akatwaa moja ya mbavu za mtu huyu na akapafunika pale alipo chukua ubavu.
Yahvé Dieu fit tomber l'homme dans un profond sommeil. Comme l'homme dormait, il prit une de ses côtes et referma la chair à sa place.
22 Kwa ubavu ambao Yahwe Mungu alichukua toka kwa mtu huyu, akafanya mwanamke na akamleta kwa mtu huyu.
Yahvé Dieu fit une femme de la côte qu'il avait prise à l'homme, et il l'amena à l'homme.
23 Mwanaume akasema, “kwa sasa, huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu. ataitwa 'mwanamke,' kwa sababu ametwaliwa katika mwanaume.
L'homme dit: « Voici l'os de mes os et la chair de ma chair. On l'appellera femme, parce qu'elle est sortie de l'homme ».
24 Kwa hiyo mwanaume atawaacha baba yake na mama yake, ataungamanika na mke wake, na watakuwa mwili mmoja.
C'est pourquoi l'homme quittera son père et sa mère, et s'attachera à sa femme, et ils seront une seule chair.
25 Wote wawili walikuwa uchi, mwanaume na mke wake, lakini hawakuona aibu.
L'homme et sa femme étaient tous deux nus, et ils n'ont pas eu honte.