< Mwanzo 2 >
1 Kisha mbingu na nchi zilimalizika, na viumbe hai vyote vilivyo jaza mbingu na nchi.
and to end: finish [the] heaven and [the] land: country/planet and all army their
2 Siku ya saba Mungu alifikia mwisho wa kazi yake ambayo aliifanya, na kwa hiyo alipumzika siku ya saba kutoka kwenye kazi yake yote.
and to end: finish God in/on/with day [the] seventh work his which to make: do and to cease in/on/with day [the] seventh from all work his which to make: do
3 Mungu akaibarikia siku ya saba na akaitakasa, kwa sababu katika siku hiyo alipumzika kutoka kwenye kazi yake yote ambayo aliifanya katika uumbaji.
and to bless God [obj] day [the] seventh and to consecrate: consecate [obj] him for in/on/with him to cease from all work his which to create God to/for to make: do
4 Haya yalikuwa ni matukio yahusuyo mbingu na nchi, wakati vilipoumbwa, katika siku ambayo Yahwe Mungu aliumba nchi na mbingu.
these generation [the] heaven and [the] land: country/planet in/on/with to create they in/on/with day to make LORD God land: country/planet and heaven
5 Hapakuwa na msitu wa shambani uliokuwa katika nchi, na hapakuwa na mmea wa shambani uliokuwa umechipuka, kwa kuwa Yahwe Mungu alikuwa hajasababisha mvua kunyesha juu ya nchi, na hapakuwa na mtu wa kulima ardhi.
and all bush [the] land: country before to be in/on/with land: country/planet and all vegetation [the] land: country before to spring for not to rain LORD God upon [the] land: country/planet and man nothing to/for to serve: labour [obj] [the] land: soil
6 Lakini ukungu uliinuka juu kutoka kwenye nchi na kuutia maji uso wote wa ardhi.
and mist to ascend: rise from [the] land: country/planet and to water: watering [obj] all face: surface [the] land: soil
7 Yahwe Mungu aliumba mtu kutoka mavumbi ya ardhi, na akampulizia puani pumzi ya uhai, na mtu akawa kiumbe hai.
and to form: formed LORD God [obj] [the] the man (Adam) dust from [the] land: soil and to breathe in/on/with face: nose his breath life and to be [the] the man (Adam) to/for soul: animal alive
8 Yahwe Mungu aliotesha bustani upande wa mashariki, katika Edeni, na pale akamuweka mtu ambaye alimuumba.
and to plant LORD God garden (in/on/with Eden *L(abh)*) from front: east and to set: put there [obj] [the] the man (Adam) which to form: formed
9 Kutoka ardhini Yahwe Mungu alifanya kila mti uote ambao unapendeza na ni mzuri kwa chakula. Hii ni pamoja na mti wa uzima ambao ulikuwa katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.
and to spring LORD God from [the] land: soil all tree to desire to/for appearance and pleasant to/for food and tree [the] life in/on/with midst [the] garden and tree [the] knowledge good and bad: evil
10 Mto ukatoka nje ya Edeni kuitia maji bustani. Na kutoka pale ukagawanyika na kuwa mito minne.
and river to come out: issue from Eden to/for to water: watering [obj] [the] garden and from there to separate and to be to/for four head: first
11 Jina la ule wa kwanza ni Pishoni. Huu ni ule ambao unatiririka kupitia nchi yote ya Havila, ambapo kuna dhahabu.
name [the] one Pishon he/she/it [the] to turn: turn [obj] all land: country/planet [the] Havilah which there [the] gold
12 Dhahabu ya inchi ile ni nzuri. pia kuna bedola na jiwe shohamu.
and gold [the] land: country/planet [the] he/she/it pleasant there [the] bdellium and stone [the] onyx
13 Jina la mto wa pili ni Gihoni. Huu unatiririka kupitia nchi yote ya kushi.
and name [the] river [the] second Gihon he/she/it [the] to turn: turn [obj] all land: country/planet Cush
14 Jina la mto wa tatu ni Hidekeli, ambao unatiririka mashariki mwa Ashuru. Mto wa nne ni Frati.
and name [the] river [the] third Tigris he/she/it [the] to go: walk east Assyria and [the] river [the] fourth he/she/it Euphrates
15 Yahwe Mungu alimtwaa mtu na kumweka ndani ya bustani ya Edeni kuilima na kuitunza.
and to take: take LORD God [obj] [the] the man (Adam) and to rest him in/on/with garden Eden to/for to serve: labour her and to/for to keep: guard her
16 Yahwe Mungu alimuagiza mtu akisema, “kutoka kwenye kila mti bustanini waweza kula kwa uhuru.
and to command LORD God upon [the] the man (Adam) to/for to say from all tree [the] garden to eat to eat
17 Lakini kutoka kwenye mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa kuwa siku utakayo kula kutoka katika mti huo, utakufa hakika.”
and from tree [the] knowledge good and bad: evil not to eat from him for in/on/with day to eat you from him to die to die
18 Kisha Yahwe Mungu akasema, “siyo jambo jema kwamba mtu huyu lazima awe pekeyake. Nitamfanyia msaidizi anaye mfaa.”
and to say LORD God not pleasant to be [the] the man (Adam) to/for alone him to make to/for him helper like/as before him
19 Kutoka ardhini Yahwe Mungu akafanya kila mnyama wa kondeni na kila ndege wa angani. Kisha akawaleta kwa mtu huyu aone angewapatia majina gani. Jina ambalo mtu huyu alimwita kila kiumbe hai, hili ndilo lilikuwa jina lake.
and to form: formed LORD God from [the] land: soil all living thing [the] land: country and [obj] all bird [the] heaven and to come (in): bring to(wards) [the] the man (Adam) to/for to see: see what? to call: call by to/for him and all which to call: call by to/for him [the] the man (Adam) soul: animal alive he/she/it name his
20 Mtu huyu akawapatia majina wanyama wote, ndege wote wa angani, na kila mnyama wa mwitu. Lakini kwa mtu mwenyewe hapakuwa na msaidizi wa kumfaa yeye.
and to call: call by [the] the man (Adam) name to/for all [the] animal and to/for bird [the] heaven and to/for all living thing [the] land: country and to/for Adam not to find helper like/as before him
21 Yahwe Mungu akaleta usingizi mzito kwa mtu huyu, kwa hiyo mtu huyu akalala. Yahwe Mungu akatwaa moja ya mbavu za mtu huyu na akapafunika pale alipo chukua ubavu.
and to fall: fall LORD God deep sleep upon [the] the man (Adam) and to sleep and to take: take one from side his and to shut flesh underneath: instead her
22 Kwa ubavu ambao Yahwe Mungu alichukua toka kwa mtu huyu, akafanya mwanamke na akamleta kwa mtu huyu.
and to build LORD God [obj] [the] side which to take: take from [the] the man (Adam) to/for woman and to come (in): bring her to(wards) [the] the man (Adam)
23 Mwanaume akasema, “kwa sasa, huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu. ataitwa 'mwanamke,' kwa sababu ametwaliwa katika mwanaume.
and to say [the] the man (Adam) this [the] beat bone from bone my and flesh from flesh my to/for this to call: call by woman for from man to take: take this
24 Kwa hiyo mwanaume atawaacha baba yake na mama yake, ataungamanika na mke wake, na watakuwa mwili mmoja.
upon so to leave: forsake man [obj] father his and [obj] mother his and to cleave in/on/with woman: wife his and to be to/for flesh one
25 Wote wawili walikuwa uchi, mwanaume na mke wake, lakini hawakuona aibu.
and to be two their naked [the] the man (Adam) and woman: wife his and not be ashamed