< Mwanzo 2 >
1 Kisha mbingu na nchi zilimalizika, na viumbe hai vyote vilivyo jaza mbingu na nchi.
And the heaven and the earth and all things in them were complete.
2 Siku ya saba Mungu alifikia mwisho wa kazi yake ambayo aliifanya, na kwa hiyo alipumzika siku ya saba kutoka kwenye kazi yake yote.
And on the seventh day God came to the end of all his work; and on the seventh day he took his rest from all the work which he had done.
3 Mungu akaibarikia siku ya saba na akaitakasa, kwa sababu katika siku hiyo alipumzika kutoka kwenye kazi yake yote ambayo aliifanya katika uumbaji.
And God gave his blessing to the seventh day and made it holy: because on that day he took his rest from all the work which he had made and done.
4 Haya yalikuwa ni matukio yahusuyo mbingu na nchi, wakati vilipoumbwa, katika siku ambayo Yahwe Mungu aliumba nchi na mbingu.
These are the generations of the heaven and the earth when they were made.
5 Hapakuwa na msitu wa shambani uliokuwa katika nchi, na hapakuwa na mmea wa shambani uliokuwa umechipuka, kwa kuwa Yahwe Mungu alikuwa hajasababisha mvua kunyesha juu ya nchi, na hapakuwa na mtu wa kulima ardhi.
In the day when the Lord God made earth and heaven there were no plants of the field on the earth, and no grass had come up: for the Lord God had not sent rain on the earth and there was no man to do work on the land.
6 Lakini ukungu uliinuka juu kutoka kwenye nchi na kuutia maji uso wote wa ardhi.
But a mist went up from the earth, watering all the face of the land.
7 Yahwe Mungu aliumba mtu kutoka mavumbi ya ardhi, na akampulizia puani pumzi ya uhai, na mtu akawa kiumbe hai.
And the Lord God made man from the dust of the earth, breathing into him the breath of life: and man became a living soul.
8 Yahwe Mungu aliotesha bustani upande wa mashariki, katika Edeni, na pale akamuweka mtu ambaye alimuumba.
And the Lord God made a garden in the east, in Eden; and there he put the man whom he had made.
9 Kutoka ardhini Yahwe Mungu alifanya kila mti uote ambao unapendeza na ni mzuri kwa chakula. Hii ni pamoja na mti wa uzima ambao ulikuwa katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.
And out of the earth the Lord made every tree to come, delighting the eye and good for food; and in the middle of the garden, the tree of life and the tree of the knowledge of good and evil.
10 Mto ukatoka nje ya Edeni kuitia maji bustani. Na kutoka pale ukagawanyika na kuwa mito minne.
And a river went out of Eden giving water to the garden; and from there it was parted and became four streams.
11 Jina la ule wa kwanza ni Pishoni. Huu ni ule ambao unatiririka kupitia nchi yote ya Havila, ambapo kuna dhahabu.
The name of the first is Pishon, which goes round about all the land of Havilah where there is gold.
12 Dhahabu ya inchi ile ni nzuri. pia kuna bedola na jiwe shohamu.
And the gold of that land is good: there is bdellium and the onyx stone.
13 Jina la mto wa pili ni Gihoni. Huu unatiririka kupitia nchi yote ya kushi.
And the name of the second river is Gihon: this river goes round all the land of Cush.
14 Jina la mto wa tatu ni Hidekeli, ambao unatiririka mashariki mwa Ashuru. Mto wa nne ni Frati.
And the name of the third river is Tigris, which goes to the east of Assyria. And the fourth river is Euphrates.
15 Yahwe Mungu alimtwaa mtu na kumweka ndani ya bustani ya Edeni kuilima na kuitunza.
And the Lord God took the man and put him in the garden of Eden to do work in it and take care of it.
16 Yahwe Mungu alimuagiza mtu akisema, “kutoka kwenye kila mti bustanini waweza kula kwa uhuru.
And the Lord God gave the man orders, saying, You may freely take of the fruit of every tree of the garden:
17 Lakini kutoka kwenye mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa kuwa siku utakayo kula kutoka katika mti huo, utakufa hakika.”
But of the fruit of the tree of the knowledge of good and evil you may not take; for on the day when you take of it, death will certainly come to you.
18 Kisha Yahwe Mungu akasema, “siyo jambo jema kwamba mtu huyu lazima awe pekeyake. Nitamfanyia msaidizi anaye mfaa.”
And the Lord God said, It is not good for the man to be by himself: I will make one like himself as a help to him
19 Kutoka ardhini Yahwe Mungu akafanya kila mnyama wa kondeni na kila ndege wa angani. Kisha akawaleta kwa mtu huyu aone angewapatia majina gani. Jina ambalo mtu huyu alimwita kila kiumbe hai, hili ndilo lilikuwa jina lake.
And from the earth the Lord God made every beast of the field and every bird of the air, and took them to the man to see what names he would give them: and whatever name he gave to any living thing, that was its name.
20 Mtu huyu akawapatia majina wanyama wote, ndege wote wa angani, na kila mnyama wa mwitu. Lakini kwa mtu mwenyewe hapakuwa na msaidizi wa kumfaa yeye.
And the man gave names to all cattle and to the birds of the air and to every beast of the field; but Adam had no one like himself as a help.
21 Yahwe Mungu akaleta usingizi mzito kwa mtu huyu, kwa hiyo mtu huyu akalala. Yahwe Mungu akatwaa moja ya mbavu za mtu huyu na akapafunika pale alipo chukua ubavu.
And the Lord God sent a deep sleep on the man, and took one of the bones from his side while he was sleeping, joining up the flesh again in its place:
22 Kwa ubavu ambao Yahwe Mungu alichukua toka kwa mtu huyu, akafanya mwanamke na akamleta kwa mtu huyu.
And the bone which the Lord God had taken from the man he made into a woman, and took her to the man.
23 Mwanaume akasema, “kwa sasa, huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu. ataitwa 'mwanamke,' kwa sababu ametwaliwa katika mwanaume.
And the man said, This is now bone of my bone and flesh of my flesh: let her name be Woman because she was taken out of Man.
24 Kwa hiyo mwanaume atawaacha baba yake na mama yake, ataungamanika na mke wake, na watakuwa mwili mmoja.
For this cause will a man go away from his father and his mother and be joined to his wife; and they will be one flesh.
25 Wote wawili walikuwa uchi, mwanaume na mke wake, lakini hawakuona aibu.
And the man and his wife were without clothing, and they had no sense of shame.