< Mwanzo 19 >

1 Malaika wawili wakaja Sodoma jioni, wakati ambao Lutu alikuwa amekaa langoni mwa Sodoma. Lutu akawaona, akainuka kuwalaki, na akainama uso wake chini ardhini.
Cependant les deux Anges vinrent à Sodome vers le soir, et Lot étant assis à la porte de la ville. Dès qu’il les eut vus, il se leva et alla au-devant d’eux, et se prosterna, incliné vers la terre.
2 Akasema, Tafadhari Bwana zangu, nawasihi mgeuke mwende kwenye nyumba ya mtumishi wenu, mlale pale usiku na muoshe miguu yenu. Kisha muamke asubuhi na mapema muondoke.” Nao wakasema, “Hapana, usiku tutalala mjini.”
Et il dit: Je vous conjure, seigneurs, venez dans la maison de votre serviteur, et demeurez-y; lavez vos pieds, et dès le matin vous continuerez votre route. Ils répondirent: Point du tout; mais c’est sur la place que nous demeurerons.
3 Lakini akawasihi sana, mwishowe wakaondoka pamoja nae, na wakaingia katika nyumba yake. Akaandaa chakula na kuoka mkate usiotiwa chachu, wakala.
Mais il les força par ses instances de venir chez lui; et lorsqu’ils furent entrés dans sa maison, il leur prépara un repas, et il fit cuire des azymes; et ils mangèrent.
4 Lakini kabla hawaja lala, wanaume wa mji, wa Sodoma, vijana kwa wazee wakaizunguka nyumba, wanaume wote kutoka kila kona ya mji.
Mais avant qu’ils allassent se coucher, les hommes de la ville environnèrent la maison, depuis l’enfant jusqu’au vieillard, tout le peuple ensemble.
5 Wakamwita Lutu, na kumwambia, “Wale wanaume walioingia kwako usiku wakowapi? watoe hapa nje waje kwetu, ili tuweze kulala nao.”
Et ils appelèrent Lot et lui dirent: Où sont les hommes qui sont entrés chez toi cette nuit? Amène-les ici, afin que nous les connaissions.
6 Lutu akatoka nje na akafunga mlango.
Lot étant sorti vers eux, et ayant fermé derrière lui la porte, dit:
7 Akasema, “Nawasihi, ndugu zangu, msitende uovu.
Ne faites pas, je vous prie, mes frères, ne faites pas ce mal.
8 Tazama, nina mabinti wawili ambao hawajawahi kulala na mwanaume yeyote. Nawaomba tafadhari niwalete kwenu, na muwafanyie lolote muonalo kuwa jema machoni penu. Msitende lolote kwa wanaume hawa, kwa kuwa wamekuja chini ya kivuli cha dari yangu.”
J’ai deux filles qui n’ont pas encore connu d’hommes: je vous les amènerai, et vous ferez d’elles ce qui vous plaira, pourvu qu’à ces hommes vous ne fassiez aucun mal; car ils sont venus à l’ombre de mon toit.
9 Wakasema, “Ondoka hapa!” Wakasema pia, huyu alikuja kukaa hapa kama mgeni, na sasa amekuwa mwamuzi! Sasa tutakushugulilia vibaya wewe kuliko wao.” Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, na wakakaribia kuvunja mlango.
Mais ils répondirent: Retire-toi d’ici. Et de nouveau: Tu es venu ici, dirent-ils, comme étranger; est-ce pour t’ériger en juge. C’est donc toi-même que nous maltraiterons plus qu’eux. Et ils faisaient à Lot la plus grande violence; et déjà ils étaient près d’enfoncer la porte.
10 Lakini wale wanaume wakamkamata Lutu na kumweka ndani na wakafunga mlango.
Mais voilà que les hommes avancèrent la main, firent rentrer Lot auprès d’eux et fermèrent la porte;
11 Kisha wale wageni wa Lutu wakawapiga kwa upofu wale wanaume waliokuwa nje ya nyumba, vijana na wazee kwa pamoja, kiasi kwamba wakachoka wakati wakiutafuta mlango.
Et ceux qui étaient dehors, ils les frappèrent d’aveuglement, depuis le plus petit Jusqu’au plus grand, en sorte qu’ils ne pouvaient retrouver la porte.
12 Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je una mtu mwingine yeyote hapa? wakwe zako, wanao na mabinti zako, na yeyote mwingine katika huu mji, ukawatoe hapa.
Alors ils dirent à Lot: As-tu ici quelqu’un des tiens, un gendre, ou des fils, ou des filles? tous ceux qui sont à toi, fais-les sortir de cette ville;
13 Kwa kuwa tunakaribia kuiangamiza sehemu hii, kwa sababu mashitaka dhidi yake mbele ya Yahwe yamezidi kiasi kwamba ametutuma kuuangamiza.”
Car nous détruirons ce lieu, parce que leur clameur s’est élevée de plus en plus devant le Seigneur qui nous a envoyés pour les perdre.
14 Lutu akatoka na akazungumza na wakwe zake, wanaume ambao walikuwa wamewaposa binti zake, akawambia, “Ondokeni upesi mahali hapa, kwa kuwa Yahwe anakaribia kuuangamiza mji.” Lakini kwa wakwe zake alionekana kuwa anawatania.
Lot étant donc sorti, parla à ses gendres, qui devaient épouser ses filles, et dit: Levez-vous, sortez de ce lieu; parce que le Seigneur détruira cette ville. Et il leur sembla parler comme en se jouant.
15 Alfajiri, malaika wakamsihi Lutu, wakisema, ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili ambao wako hapa, ili kwamba usipotelee katika adhabu ya mji huu.”
Mais lorsqu’il fut matin, les Anges le pressaient, disant: Lève-toi, prends ta femme, et les deux filles que tu as, afin que tu ne périsses pas, toi aussi, dans le châtiment de la ville.
16 Lakini akakawia-kawia. Kwa hiyo watu wale wakamshika mkono wake, na mkono wa mkewe, na mikono ya binti zake wawili, kwa sababu Yahwe alimhurumia. Wakawatoa nje, na kuwaweka nje ya mji.
Mais lui différant, ils prirent sa main et la main de sa femme et de ses deux filles, parce que le Seigneur lui faisait grâce.
17 Wakisha kuwatoa nje mmoja wa wale watu akasema, “jiponye nafsi yako! usitazame nyuma, au usikae mahali popote kwenye hili bonde. Toroka uende milimani ili kwamba usije ukatoweshwa mbali.”
Et ils l’emmenèrent, le mirent hors de la ville: et là, ils lui parlèrent, disant: Sauve ton âme; ne regarde point derrière toi, et ne t’arrête dans aucune contrée d’alentour; mais sauve-toi sur la montagne, de peur que tu ne périsses toi aussi avec les autres.
18 Lutu akawambia, “Hapana, tafadhali bwana zangu!
Et Lot leur répondit: Je vous prie, mon Seigneur,
19 Mtumishi wenu amepata kibali machoni pako, na umenionesha wema ulio mkuu kwa kuokoa maisha yangu, lakini sitaweza kutorokea milimani, kwa sababu mabaya yataniwahi na nitakufa.
Puisque votre serviteur a trouvé grâce devant vous et que vous avez signalé la miséricorde que vous m’avez faite, pour sauver mon âme, non, je ne puis être sauvé sur la montagne; il est à craindre que le mal ne m’atteigne, et que je ne meure.
20 Tazama, ule mji pale uko karibu nijisalimishe pale, na ni mdogo. Tafadhari niacheni nikimbilie pale ( Je Siyo mdogo ule?), na maisha yangu yataokolewa.”
Cette ville ici près, où je puis m’enfuir, est petite et j’y serai sauvé; n’est-elle pas de peu d’étendue? et mon âme n’y vivra-t-elle pas?
21 Akamwambia, “Sawa, nimekubali ombi hili pia, kwamba sitaangamiza mji ambaoumeutaja.
Et il lui répondit: Voici que même en cela, j’ai accueilli ta prière, de ne pas détruire la ville pour laquelle tu m’as parlé.
22 Harakisha! toroka uende pale, kwa kuwa sitafanya chochote mpaka ufike pale.” kwa hiyo mji ule ukaitwa Soari.
Hâte-toi, et tu y seras sauvé; car je ne pourrai rien faire jusqu’à ce que tu y sois entré. C’est pourquoi cette ville fut appelée du nom de Ségor.
23 Jua lilikuwa limekwisha chomoza juu ya nchi wakati Lutu alipofika Soari.
Le soleil se leva sur la terre, et Lot entra dans Ségor.
24 Kisha Yahwe akanyesha juu ya Sodoma na Gomora kiberiti na moto toka kwa Yahwe mbinguni.
Le Seigneur donc fit pleuvoir sur Sodome et Gomorrhe du soufre et du feu venus du ciel d’auprès du Seigneur;
25 Akaharibu miji ile, na bonde lote, na vyote vilivyomo katika miji, na mimea iliyo chipua juu ya ardhi.
Et il détruisit ces villes, et toute la contrée d’alentour, et tous les habitants des villes, et toutes les plantes de la terre.
26 Lakini mke wa Lutu aliye kuwa nyuma yake, akatazama nyuma, na akawa nguzo ya chumvi.
Et la femme de Lot, regardant derrière elle, fut changée en une statue de sel.
27 Abraham akaamuka asubuhi na mapema akaenda mahali alipokuwa amesimama mbele ya Yahwe.
Or Abraham se levant le matin, et venant où il avait été auparavant avec le Seigneur,
28 Akatazama chini kuelekea Sodoma na Gomora na kuelekea katika nchi yote bondeni. Akaona na tazama, moshi ulikuwauki ukienda juu kutoka chini kama moshi wa tanuru.
Regarda Sodome et Gomorrhe, et toute la terre de cette contrée, et il vit une fumée qui montait de la terre, comme la fumée d’une fournaise.
29 Wakati Mungu alipoharibu miji ya bondeni, Mungu akamkumbuka Abraham. Akamtoa Lutu kutoka katika maangamizi alipoangamiza miji ambayo katika hiyo Lutu aliishi.
Mais, lorsque le Seigneur détruisait les villes de cette contrée, s’étant souvenu d’Abraham, il sauva Lot de la ruine de ces villes dans lesquelles il avait habité.
30 Lakini Lutu akapanda juu kutoka Soari na kwenda kuishi katika milima akiwa pamoja na binti zake wawili, kwa sababu aliogopa kuishi Soari. Kwa hiyo akaishi pangoni, yeye na binti zake wawili.
Et Lot sortit de Ségor; il se retira sur la montagne, et ses deux filles avec lui (car il craignait de demeurer dans Ségor), et il demeura dans la caverne, lui et ses deux filles avec lui.
31 Yule wa kwanza akamwambia yule mdogo, “Baba yetu ni mzee, na hakuna mwanaume mahali popote wa kulala na sisi kulingana na desturi ya dunia yote.
Or l’aînée dit à la plus jeune: Notre père est vieux, et il n’est resté sur la terre aucun homme qui puisse nous épouser selon la coutume de toute la terre.
32 Njoo na tumnyweshe baba yetu mvinyo na tulale naye ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu.”
Viens, et enivrons-le de vin, et dormons avec lui, afin que nous puissions par notre père conserver une postérité.
33 Kwa hiyo wakamnywesha baba yako mvinyo usiku ule. Kisha yule wa kwanza akaingia na akalala na baba yake; Baba yake hakujua ni wakati gani alikuja kulala, wala wakati alipo amka.
Elles donnèrent donc à leur père du vin à boire cette nuit-là; et l’aînée vint et dormit avec son père; mais celui-ci ne s’aperçut, ni quand sa fille se coucha, ni quand elle se leva.
34 Siku iliyo fuata yule wa kwanza akamwambia mdogowake, “Sikiliza, usiku wa jana nililala na baba yangu. Na tumnyweshe mvinyo usiku wa leo pia, na uingie ukalale naye. Ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu.”
Et le lendemain, l’aînée dit à la plus jeune: Voilà que j’ai dormi hier avec mon père; donnons-lui à boire du vin encore cette nuit, et tu dormiras avec lui, afin que nous conservions une postérité de notre père.
35 Kwa hiyo wakamnywesha baba yao mvinyo usiku ule pia, na yule mdogo akaenda na akalala naye. Baba yake hakujua ni wakati gani alilala, wala wakati alipoamka.
Et elles donnèrent encore cette nuit-là à leur père du vin à boire; et la plus jeune fille dormit avec lui; et encore cette fois, il ne s’aperçut pas quand elle se coucha, ou quand elle se leva.
36 Basi hao binti wote wawili wa Lutu wakapata mimba kwa baba yao.
Ainsi les deux filles de Lot conçurent de leur père.
37 Wa kwanza akazaa mwana wa kiume, na akamwita jina lake Moabu. Akawa ndiye baba wa wamoabu hata leo.
L’aînée enfanta un fils, et l’appela du nom de Moab; c’est le père des Moabites, jusqu’au présent jour.
38 Nayule mdogo naye akazaa mwana wa kiume, na akamwita Benami. Huyu ndiye baba wa watu wa Waamoni hata leo.
La plus jeune aussi enfanta un fils, et l’appela du nom d’Ammon, c’est-à-dire le fils de mon peuple; c’est le père des Ammonites, jusqu’aujourd’hui.

< Mwanzo 19 >