< Mwanzo 19 >

1 Malaika wawili wakaja Sodoma jioni, wakati ambao Lutu alikuwa amekaa langoni mwa Sodoma. Lutu akawaona, akainuka kuwalaki, na akainama uso wake chini ardhini.
And the two Angels arrived at Sodom in the evening, and Lot was sitting at the gate of the city. And when he had seen them, he rose up and went to meet them. And he reverenced prone on the ground.
2 Akasema, Tafadhari Bwana zangu, nawasihi mgeuke mwende kwenye nyumba ya mtumishi wenu, mlale pale usiku na muoshe miguu yenu. Kisha muamke asubuhi na mapema muondoke.” Nao wakasema, “Hapana, usiku tutalala mjini.”
And he said: “I beg you, my lords, turn aside to the house of your servant, and lodge there. Wash your feet, and in the morning you will advance on your way.” And they said, “Not at all. But we will lodge in the street.”
3 Lakini akawasihi sana, mwishowe wakaondoka pamoja nae, na wakaingia katika nyumba yake. Akaandaa chakula na kuoka mkate usiotiwa chachu, wakala.
He pressed them very much to turn aside to him. And when they had entered his house, he made a feast for them, and he cooked unleavened bread, and they ate.
4 Lakini kabla hawaja lala, wanaume wa mji, wa Sodoma, vijana kwa wazee wakaizunguka nyumba, wanaume wote kutoka kila kona ya mji.
But before they went to bed, the men of the city surrounded the house, from boys to old men, all the people together.
5 Wakamwita Lutu, na kumwambia, “Wale wanaume walioingia kwako usiku wakowapi? watoe hapa nje waje kwetu, ili tuweze kulala nao.”
And they called out to Lot, and they said to him: “Where are the men who entered to you in the night? Bring them out here, so that we may know them.”
6 Lutu akatoka nje na akafunga mlango.
Lot went out to them, and blocking the door behind him, he said:
7 Akasema, “Nawasihi, ndugu zangu, msitende uovu.
“Do not, I ask you, my brothers, do not be willing to commit this evil.
8 Tazama, nina mabinti wawili ambao hawajawahi kulala na mwanaume yeyote. Nawaomba tafadhari niwalete kwenu, na muwafanyie lolote muonalo kuwa jema machoni penu. Msitende lolote kwa wanaume hawa, kwa kuwa wamekuja chini ya kivuli cha dari yangu.”
I have two daughters who as yet have not known man. I will bring them out to you; abuse them as it pleases you, provided that you do no evil to these men, because they have entered under the shadow of my roof.”
9 Wakasema, “Ondoka hapa!” Wakasema pia, huyu alikuja kukaa hapa kama mgeni, na sasa amekuwa mwamuzi! Sasa tutakushugulilia vibaya wewe kuliko wao.” Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, na wakakaribia kuvunja mlango.
But they said, “Move away from there.” And again: “You have entered,” they said, “as a stranger; should you then judge? Therefore, we will afflict you yourself more than them.” And they acted very violently against Lot. And they were now at the point of breaking open the doors.
10 Lakini wale wanaume wakamkamata Lutu na kumweka ndani na wakafunga mlango.
And behold, the men put out their hand, and they pulled Lot in to them, and they closed the door.
11 Kisha wale wageni wa Lutu wakawapiga kwa upofu wale wanaume waliokuwa nje ya nyumba, vijana na wazee kwa pamoja, kiasi kwamba wakachoka wakati wakiutafuta mlango.
And they struck those who were outside with blindness, from the least to the greatest, so that they were not able to find the door.
12 Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je una mtu mwingine yeyote hapa? wakwe zako, wanao na mabinti zako, na yeyote mwingine katika huu mji, ukawatoe hapa.
Then they said to Lot: “Do you have here anyone of yours? All who are yours, sons-in-law, or sons, or daughters, bring them out of this city.
13 Kwa kuwa tunakaribia kuiangamiza sehemu hii, kwa sababu mashitaka dhidi yake mbele ya Yahwe yamezidi kiasi kwamba ametutuma kuuangamiza.”
For we will eliminate this place, because the outcry among them has increased before the Lord, who sent us to destroy them.”
14 Lutu akatoka na akazungumza na wakwe zake, wanaume ambao walikuwa wamewaposa binti zake, akawambia, “Ondokeni upesi mahali hapa, kwa kuwa Yahwe anakaribia kuuangamiza mji.” Lakini kwa wakwe zake alionekana kuwa anawatania.
And so Lot, going out, spoke to his sons-in-law, who were going to receive his daughters, and he said: “Rise up. Depart from this place. For the Lord will destroy this city.” And it seemed to them that he was speaking playfully.
15 Alfajiri, malaika wakamsihi Lutu, wakisema, ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili ambao wako hapa, ili kwamba usipotelee katika adhabu ya mji huu.”
And when it was morning, the Angels compelled him, saying, “Arise, take your wife, and the two daughters that you have, lest you also should perish amid the wickedness of the city.”
16 Lakini akakawia-kawia. Kwa hiyo watu wale wakamshika mkono wake, na mkono wa mkewe, na mikono ya binti zake wawili, kwa sababu Yahwe alimhurumia. Wakawatoa nje, na kuwaweka nje ya mji.
And, since he ignored them, they took his hand, and the hand of his wife, as well as that of his two daughters, because the Lord was sparing him.
17 Wakisha kuwatoa nje mmoja wa wale watu akasema, “jiponye nafsi yako! usitazame nyuma, au usikae mahali popote kwenye hili bonde. Toroka uende milimani ili kwamba usije ukatoweshwa mbali.”
And they brought him out, and placed him beyond the city. And there they spoke to him, saying: “Save your life. Do not look back. Neither should you stay in the entire surrounding region. But save yourself in the mountain, lest you also should perish.”
18 Lutu akawambia, “Hapana, tafadhali bwana zangu!
And Lot said to them: “I beg you, my lord,
19 Mtumishi wenu amepata kibali machoni pako, na umenionesha wema ulio mkuu kwa kuokoa maisha yangu, lakini sitaweza kutorokea milimani, kwa sababu mabaya yataniwahi na nitakufa.
though your servant has found grace before you, and you have magnified your mercy, which you have shown to me in saving my life, I cannot be saved on the mountain, lest perhaps some misfortune take hold of me and I die.
20 Tazama, ule mji pale uko karibu nijisalimishe pale, na ni mdogo. Tafadhari niacheni nikimbilie pale ( Je Siyo mdogo ule?), na maisha yangu yataokolewa.”
There is a certain city nearby, to which I can flee; it is a little one, and I will be saved in it. Is it not a modest one, and will not my soul live?”
21 Akamwambia, “Sawa, nimekubali ombi hili pia, kwamba sitaangamiza mji ambaoumeutaja.
And he said to him: “Behold, even now, I have heard your petitions about this, not to overturn the city on behalf of which you have spoken.
22 Harakisha! toroka uende pale, kwa kuwa sitafanya chochote mpaka ufike pale.” kwa hiyo mji ule ukaitwa Soari.
Hurry and be saved there. For I cannot do anything until you enter there.” For this reason, the name of that city is called Zoar.
23 Jua lilikuwa limekwisha chomoza juu ya nchi wakati Lutu alipofika Soari.
The sun had risen over the land, and Lot had entered into Zoar.
24 Kisha Yahwe akanyesha juu ya Sodoma na Gomora kiberiti na moto toka kwa Yahwe mbinguni.
Therefore, the Lord rained upon Sodom and Gomorrah sulphur and fire, from the Lord, out of heaven.
25 Akaharibu miji ile, na bonde lote, na vyote vilivyomo katika miji, na mimea iliyo chipua juu ya ardhi.
And he overturned these cities, and all the surrounding region: all the inhabitants of the cities, and everything that springs from the land.
26 Lakini mke wa Lutu aliye kuwa nyuma yake, akatazama nyuma, na akawa nguzo ya chumvi.
And his wife, looking behind herself, was turned into a statue of salt.
27 Abraham akaamuka asubuhi na mapema akaenda mahali alipokuwa amesimama mbele ya Yahwe.
Then Abraham, rising up in the morning, in the place where he had stood before with the Lord,
28 Akatazama chini kuelekea Sodoma na Gomora na kuelekea katika nchi yote bondeni. Akaona na tazama, moshi ulikuwauki ukienda juu kutoka chini kama moshi wa tanuru.
looked out toward Sodom and Gomorrah, and the entire land of that region. And he saw embers rising up from the land like smoke from a furnace.
29 Wakati Mungu alipoharibu miji ya bondeni, Mungu akamkumbuka Abraham. Akamtoa Lutu kutoka katika maangamizi alipoangamiza miji ambayo katika hiyo Lutu aliishi.
For when God overthrew the cities of that region, remembering Abraham, he freed Lot from the overthrow of the cities, in which he had dwelt.
30 Lakini Lutu akapanda juu kutoka Soari na kwenda kuishi katika milima akiwa pamoja na binti zake wawili, kwa sababu aliogopa kuishi Soari. Kwa hiyo akaishi pangoni, yeye na binti zake wawili.
And Lot ascended from Zoar, and he stayed on the mountain, and likewise his two daughters with him, (for he was afraid to stay in Zoar) and he dwelt in a cave, he and his two daughters with him.
31 Yule wa kwanza akamwambia yule mdogo, “Baba yetu ni mzee, na hakuna mwanaume mahali popote wa kulala na sisi kulingana na desturi ya dunia yote.
And the elder said to the younger: “Our father is old, and no man remains in the land who can enter to us according to the custom of the whole world.
32 Njoo na tumnyweshe baba yetu mvinyo na tulale naye ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu.”
Come, let us inebriate him with wine, and let us sleep with him, so that we may be able to preserve offspring from our father.”
33 Kwa hiyo wakamnywesha baba yako mvinyo usiku ule. Kisha yule wa kwanza akaingia na akalala na baba yake; Baba yake hakujua ni wakati gani alikuja kulala, wala wakati alipo amka.
And so they gave their father wine to drink that night. And the elder went in, and she slept with her father. But he did not perceive it, neither when his daughter lay down, nor when she rose up.
34 Siku iliyo fuata yule wa kwanza akamwambia mdogowake, “Sikiliza, usiku wa jana nililala na baba yangu. Na tumnyweshe mvinyo usiku wa leo pia, na uingie ukalale naye. Ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu.”
Likewise, the next day, the elder said to the younger: “Behold, yesterday I slept with my father, let us give him wine to drink yet again this night, and you will sleep with him, so that we may save offspring from our father.”
35 Kwa hiyo wakamnywesha baba yao mvinyo usiku ule pia, na yule mdogo akaenda na akalala naye. Baba yake hakujua ni wakati gani alilala, wala wakati alipoamka.
And then they gave their father wine to drink that night also, and the younger daughter went in, and slept with him. And not even then did he perceive when she lay down, or when she rose up.
36 Basi hao binti wote wawili wa Lutu wakapata mimba kwa baba yao.
Therefore, the two daughters of Lot conceived by their father.
37 Wa kwanza akazaa mwana wa kiume, na akamwita jina lake Moabu. Akawa ndiye baba wa wamoabu hata leo.
And the elder gave birth to a son, and she called his name Moab. He is the father of the Moabites, even to the present day.
38 Nayule mdogo naye akazaa mwana wa kiume, na akamwita Benami. Huyu ndiye baba wa watu wa Waamoni hata leo.
Likewise, the younger gave birth to a son, and she called his name Ammon, that is, ‘the son of my people.’ He is the father of the Ammonites, even today.

< Mwanzo 19 >