< Mwanzo 18 >

1 Yahwe alimtokea Abraham katika Mialoni ya Mamre, alipokua ameketi mlangoni pa hema wakati wa jua.
And Jehovah appeareth unto him among the oaks of Mamre, and he is sitting at the opening of the tent, about the heat of the day;
2 Akatazama juu na, tazama, akaona wanaume watatu wamesimama mbele yake. Alipo waona, alikimbia kupitia mlango wa hema kuwalaki na kuinama chini hadi ardhini.
and he lifteth up his eyes and looketh, and lo, three men standing by him, and he seeth, and runneth to meet them from the opening of the tent, and boweth himself towards the earth,
3 Akasema, “Bwana, kama nimepata upendelea machoni pako, nakuomba usinipite na kuniacha mtumishi wako.
And he saith, 'My Lord, if, I pray thee, I have found grace in thine eyes, do not, I pray thee, pass on from thy servant;
4 Naomba maji kidogo yaletwe, mnawe miguu yenu, na mjipumzishe chini ya mti.
let, I pray thee, a little water be accepted, and wash your feet, and recline under the tree;
5 Nami acha nilete chakula kidogo, ili kwamba mjiburudishe wenyewe. Ndipo baadae mwaweza kwenda zenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.” Nao wakasema, “Fanya kama ulivyo sema.”
and I bring a piece of bread, and support ye your heart; afterwards pass on, for therefore have ye passed over unto your servant;' and they say, 'So mayest thou do as thou has spoken.'
6 Kisha Abraham akaenda upesi hemani kwa Sara, na akasema, “Harakisha, chukua vipimo vitatu vya unga safi, uukande, na fanya mkate.”
And Abraham hasteth towards the tent, unto Sarah, and saith, 'Hasten three measures of flour-meal, knead, and make cakes;'
7 Kisha Abraham akakimbia kundini, akachukua ndama wa ng'ombe aliye laini na mzuri, na akampatia mtumishi na kwa haraka akamwandaa.
and Abraham ran unto the herd, and taketh a son of the herd, tender and good, and giveth unto the young man, and he hasteth to prepare it;
8 Akatwaa siagi na maziwa na ndama aliye kwisha andaliwa, na akaweka chakula mbele yao, naye akasimama karibu nao chini ya mti wakati wanakula.
and he taketh butter and milk, and the son of the herd which he hath prepared, and setteth before them; and he is standing by them under the tree, and they do eat.
9 Wakamwambia, “Mke wako Sara yuko wapi?” akajibu. “pale hemani.”
And they say unto him, 'Where [is] Sarah thy wife?' and he saith, 'Lo — in the tent;'
10 akasema, “Hakika nitarejea kwako majira ya machipuko, na tazama Sara mkeo atakuwa na mtoto wa kiume.” Sara alikuwa akisikiliza mlangoni pa hema iliyokuwa nyuma yake.
and he saith, 'returning I return unto thee, about the time of life, and lo, to Sarah thy wife a son.'
11 Abraham na Sara walikuwa wazee, umri wao ulikuwa umeendelea sana, na Sara alikuwa amepita umri ambao mwanamke anaweza kuzaa watoto.
And Sarah is hearkening at the opening of the tent, which is behind him;
12 Kwa hiyo Sara akajicheka mwenyewe, akijisemesha mwenyewe, “baada ya kuwa nimechakaa na bwana wangu ni mzee, je ni tapata furaha hii?”
and Abraham and Sarah [are] aged, entering into days — the way of women hath ceased to be to Sarah;
13 Yahwe akamwambia Abraham, “Kwa nini Sara amecheka na kusema, Je ni kweli nitazaa mtoto, nikiwa mzee'?
and Sarah laugheth in her heart, saying, 'After I have waxed old I have had pleasure! — my lord also [is] old!'
14 Je kuna jambo lolote gumu sana kwa Yahwe? Itakuwa katika wakati nilioweka mimi majira ya machipuko, nitarejea kwako. Majira haya mwakani Sara atakuwa na mtoto wa kiume.”
And Jehovah saith unto Abraham, 'Why [is] this? Sarah hath laughed, saying, Is it true really — I bear — and I am aged? Is any thing too wonderful for Jehovah? at the appointed time I return unto thee, about the time of life, and Sarah hath a son.'
15 Kisha Sara akakataa na kusema, “sikucheka,” kwa kuwa aliogopa. Yahwe akasema, “hapana ulicheka.”
And Sarah denieth, saying, 'I did not laugh;' for she hath been afraid; and He saith, 'Nay, but thou didst laugh.'
16 Kisha wale wanaume walisimama kuondoka na wakatazama chini kuelekea Sodoma. Abraham akafuatana nao kuona njia yao.
And the men rise from thence, and look on the face of Sodom, and Abraham is going with them to send them away;
17 Lakini Yahwe akasema, Je ni mfiche Abraham kile ninacho kusudia kufanya,
and Jehovah said, 'Am I concealing from Abraham that which I am doing,
18 Ikiwa kwa hakika Abraham atakuwa mkuu na taifa lenye nguvu, na katika yeye mataifa yote ya dunia watabarikiwa?
and Abraham certainly becometh a nation great and mighty, and blessed in him have been all nations of the earth?
19 Kwa kuwa nimemchagua ili awaelekeze wanawe na nyumba yake baada yake waishike njia ya Yahwe, watende utakatifu na haki, ili kwamba Yahwe ampatie Abraham yale aliyo yasema kwake.”
for I have known him, that he commandeth his children, and his house after him (and they have kept the way of Jehovah), to do righteousness and judgment, that Jehovah may bring on Abraham that which He hath spoken concerning him.'
20 Kisha Yahwe akasema, “Kwa sababu kilio cha Sodoma na Gomora ni kikuu, na kwa kuwa dhambi yao ni kubwa,
And Jehovah saith, 'The cry of Sodom and Gomorrah — because great; and their sin — because exceeding grievous:
21 sasa nitashuka pale na kuona kilio kilicho nifikia dhidi yake, ikiwa kweli wamefanya au hawakufanya, nitajua.”
I go down now, and see whether according to its cry which is coming unto Me they have done completely — and if not — I know;'
22 Kwa hiyo wale wanaume wakageuka toka pale, na kuelekea Sodoma, lakini Abraham akabaki amesimama mbele ya Yahwe.
and the men turn from thence, and go towards Sodom; and Abraham is yet standing before Jehovah.
23 Kisha Abraham alikaribia na kusema, “Je utawafutilia mbali watakatifu pamoja na waovu?
And Abraham draweth nigh and saith, 'Dost Thou also consume righteous with wicked?
24 Huenda wakawepo wenye haki hamsini katika mji. Je utawakatilia mbali na usiuache mji kwa ajili ya hao watakatifu hamsini walioko hapo?
peradventure there are fifty righteous in the midst of the city; dost Thou also consume, and not bear with the place for the sake of the fifty — the righteous who [are] in its midst?
25 Hasha usifanye hivyo, kuwauwa watakatifu pamoja na waovu, ili kwamba watakatifu watendewe sawa na waovu. Hasha! Je muhukumu wa ulimwengu wote hatatenda haki?”
Far be it from Thee to do according to this thing, to put to death the righteous with the wicked; that it hath been — as the righteous so the wicked — far be it from Thee; doth the Judge of all the earth not do justice?'
26 Yahwe akasema, “Katika Sodoma nikipata watakatifu hamsini kwenye mji, nita uacha mji wote kwa ajili ya hao.”
And Jehovah saith, 'If I find in Sodom fifty righteous in the midst of the city, then have I borne with all the place for their sake.'
27 Abraham akajibu na kusema, “Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu, hata kama mimi ni mavumbi na majivu!
And Abraham answereth and saith, 'Lo, I pray thee, I have willed to speak unto the Lord, and I — dust and ashes;
28 Itakuwaje ikiwa kuna watano pungufu katika idadi ya hao watakatifu hamsini? Je utaangamiza mji wote kwa upungufu wa hao watano?” Akasema, “Sitaangamiza, ikiwa nitapata watu arobaini na watano pale.”
peradventure there are lacking five of the fifty righteous — dost Thou destroy for five the whole of the city?' and He saith, 'I destroy [it] not, if I find there forty and five.'
29 Akaongea naye tena, na kusema, “Itakuwaje ikiwa arobaini watapatikana pale?” Akajibu, “Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini.”
And he addeth again to speak unto Him and saith, 'Peradventure there are found there forty?' and He saith, 'I do [it] not, because of the forty.'
30 Akasema, Tafadhali usikasirike, Bwana, nikiongea. Pengine thelathini watapatikana pale.” Akajibu, 'Sitafanya, ikiwa nitapata thelathini pale.”
And he saith, 'Let it not be, I Pray thee, displeasing to the Lord, and I speak: peradventure there are found there thirty?' and He saith, 'I do [it] not, if I find there thirty.'
31 Akasema, Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu! Pengine ishirini watapatikana pale.” Akajibu, “Sitaharibu kwa ajili ya hao ishirini.”
And he saith, 'Lo, I pray thee, I have willed to speak unto the Lord: peradventure there are found there twenty?' and He saith, 'I do not destroy [it], because of the twenty.'
32 Akasema, “Tafadhali usikasirike, Bwana, na nitasema jambo hili kwa mara ya mwisho. Huenda kumi wakaonekana kule.” Na akasema, sitaangamiza kwa ajili ya hao kumi.”
And he saith, 'Let it not be, I pray Thee, displeasing to the Lord, and I speak only this time: peradventure there are found there ten?' and He saith, 'I do not destroy [it], because of the ten.'
33 Yahwe akaendelea na njia yake mara tu baada ya kumaliza kuongea na Abraham, na Abraham akarudi nyumbani.
And Jehovah goeth on, when He hath finished speaking unto Abraham, and Abraham hath turned back to his place.

< Mwanzo 18 >