< Mwanzo 18 >

1 Yahwe alimtokea Abraham katika Mialoni ya Mamre, alipokua ameketi mlangoni pa hema wakati wa jua.
Forsothe in the valei of Mambre the Lord apperide to Abraham, sittynge in the dore of his tabernacle, in thilke heete of the dai.
2 Akatazama juu na, tazama, akaona wanaume watatu wamesimama mbele yake. Alipo waona, alikimbia kupitia mlango wa hema kuwalaki na kuinama chini hadi ardhini.
And whanne he hadde reisid his iyen, thre men apperiden to hym, and stoden nyy hym. And whanne he hadde seyn hem, he ran fro the dore of his tabernacle in to the meting of hem, and he worschipide on erthe,
3 Akasema, “Bwana, kama nimepata upendelea machoni pako, nakuomba usinipite na kuniacha mtumishi wako.
and seide, Lord, if Y haue founde grace in thin iyen, passe thou not thi seruaunt,
4 Naomba maji kidogo yaletwe, mnawe miguu yenu, na mjipumzishe chini ya mti.
but I schal brynge a litil watir, and youre feet be waischid, and reste ye vndur the tre;
5 Nami acha nilete chakula kidogo, ili kwamba mjiburudishe wenyewe. Ndipo baadae mwaweza kwenda zenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.” Nao wakasema, “Fanya kama ulivyo sema.”
and Y schal sette a mussel of breed, and youre herte be coumfortid; aftirward ye schulen passe; for herfor ye bowiden to youre seruaunt. Whiche seiden, Do thou as thou hast spoke.
6 Kisha Abraham akaenda upesi hemani kwa Sara, na akasema, “Harakisha, chukua vipimo vitatu vya unga safi, uukande, na fanya mkate.”
Abraham hastide in to the tabernacle, to Sare, and seide to hir, Hast thou, meddle thou thre half buschelis of clene flour; and make thou looues bakun vndur aischis.
7 Kisha Abraham akakimbia kundini, akachukua ndama wa ng'ombe aliye laini na mzuri, na akampatia mtumishi na kwa haraka akamwandaa.
Forsothe he ran to the droue of beestis, and took therof a calf moost tendre and best, and yaf to a child, which hastide, and sethede the calfe;
8 Akatwaa siagi na maziwa na ndama aliye kwisha andaliwa, na akaweka chakula mbele yao, naye akasimama karibu nao chini ya mti wakati wanakula.
and he took botere, and mylk, and the calf which he hadde sode, and settide bifore hem; forsothe Abraham stood bisidis hem vndur the tre.
9 Wakamwambia, “Mke wako Sara yuko wapi?” akajibu. “pale hemani.”
And whanne thei hadden ete, thei seiden to hym, Where is Sare thi wijf? He answerde, Lo! sche is in the tabernacle.
10 akasema, “Hakika nitarejea kwako majira ya machipuko, na tazama Sara mkeo atakuwa na mtoto wa kiume.” Sara alikuwa akisikiliza mlangoni pa hema iliyokuwa nyuma yake.
To whom the Lord seide, Y schal turne ayen, and Y schal come to thee in this tyme, if Y lyue; and Sare, thi wijf, schal haue a sone. Whanne this was herd, Sare leiyede bihynde the dore of the tabernacle.
11 Abraham na Sara walikuwa wazee, umri wao ulikuwa umeendelea sana, na Sara alikuwa amepita umri ambao mwanamke anaweza kuzaa watoto.
Forsothe bothe weren olde, and of greet age, and wommans termes ceessiden to be maad to Sare.
12 Kwa hiyo Sara akajicheka mwenyewe, akijisemesha mwenyewe, “baada ya kuwa nimechakaa na bwana wangu ni mzee, je ni tapata furaha hii?”
And she leiyede, seiynge pryueli, after that Y wexede eld, and my lord is eld, schal Y yyue diligence to lust?
13 Yahwe akamwambia Abraham, “Kwa nini Sara amecheka na kusema, Je ni kweli nitazaa mtoto, nikiwa mzee'?
Forsothe the Lord seide to Abraham, Whi leiyeth Sare, thi wijf, seiynge, whether Y an eld womman schal bere child verili?
14 Je kuna jambo lolote gumu sana kwa Yahwe? Itakuwa katika wakati nilioweka mimi majira ya machipuko, nitarejea kwako. Majira haya mwakani Sara atakuwa na mtoto wa kiume.”
whether ony thing is hard to God? Bi the biheeste Y schal turne ayen to thee in this same tyme, if Y lyue; and Sara schal haue a sone.
15 Kisha Sara akakataa na kusema, “sikucheka,” kwa kuwa aliogopa. Yahwe akasema, “hapana ulicheka.”
Sare was aferd for drede, and denyede, seiynge, Y leiyede not. Forsothe the Lord seide, It is not so, but thou leiyedist.
16 Kisha wale wanaume walisimama kuondoka na wakatazama chini kuelekea Sodoma. Abraham akafuatana nao kuona njia yao.
Therfor whanne the men hadden risen fro thennus, thei dressiden the iyen ayens Sodom; and Abraham yede to gidre, ledynge hem forth.
17 Lakini Yahwe akasema, Je ni mfiche Abraham kile ninacho kusudia kufanya,
And the Lord seide, Wher Y mowe hele fro Abraham what thingis Y schal do,
18 Ikiwa kwa hakika Abraham atakuwa mkuu na taifa lenye nguvu, na katika yeye mataifa yote ya dunia watabarikiwa?
sithen he schal be in to a greet folk and moost strong, and alle naciouns of erthe schulen be blessid in hym?
19 Kwa kuwa nimemchagua ili awaelekeze wanawe na nyumba yake baada yake waishike njia ya Yahwe, watende utakatifu na haki, ili kwamba Yahwe ampatie Abraham yale aliyo yasema kwake.”
For Y woot that Abraham schal comaunde hise children, and his hows after hym, that thei kepe the weie of the Lord, and that thei do riytfulnesse and dom, that the Lord bringe for Abraham alle thingis whiche he spak to Abraham.
20 Kisha Yahwe akasema, “Kwa sababu kilio cha Sodoma na Gomora ni kikuu, na kwa kuwa dhambi yao ni kubwa,
And so the Lord seide, The cry of men of Sodom and of men of Gomorre is multiplied, and her synne is agreggid greetli; Y schal come doun,
21 sasa nitashuka pale na kuona kilio kilicho nifikia dhidi yake, ikiwa kweli wamefanya au hawakufanya, nitajua.”
and schal se whether thei han fillid in werk the cry that cam to me, that Y wite whether it is not so.
22 Kwa hiyo wale wanaume wakageuka toka pale, na kuelekea Sodoma, lakini Abraham akabaki amesimama mbele ya Yahwe.
And thei turneden han fro thennus, and yeden to Sodom. Abraham sotheli stood yit bifore the Lord,
23 Kisha Abraham alikaribia na kusema, “Je utawafutilia mbali watakatifu pamoja na waovu?
and neiyede, and seide, Whether thou schalt leese a iust man with the wickid man?
24 Huenda wakawepo wenye haki hamsini katika mji. Je utawakatilia mbali na usiuache mji kwa ajili ya hao watakatifu hamsini walioko hapo?
if fifti iust men ben in the citee, schulen thei perische togidere, and schalt thou not spare that place for fifti iust men, if thei ben ther ynne?
25 Hasha usifanye hivyo, kuwauwa watakatifu pamoja na waovu, ili kwamba watakatifu watendewe sawa na waovu. Hasha! Je muhukumu wa ulimwengu wote hatatenda haki?”
Fer be it fro thee that thou do this thing, and sle a iust man with a wickid man, and that a iust man be maad as a wickid man; this is not thin that demest al erthe; thou schalt not make this doom.
26 Yahwe akasema, “Katika Sodoma nikipata watakatifu hamsini kwenye mji, nita uacha mji wote kwa ajili ya hao.”
And the Lord seide to him, If Y schal fynde in Sodom fifti iust men in the myddis of the citee, Y schal foryyue to al the place for hem.
27 Abraham akajibu na kusema, “Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu, hata kama mimi ni mavumbi na majivu!
Abraham answerde and seide, For Y bigan onys, Y schal speke to my Lord, sithen Y am dust and aische;
28 Itakuwaje ikiwa kuna watano pungufu katika idadi ya hao watakatifu hamsini? Je utaangamiza mji wote kwa upungufu wa hao watano?” Akasema, “Sitaangamiza, ikiwa nitapata watu arobaini na watano pale.”
what if lesse than fifti iust men bi fyue ben, schalt thou do a wey al the cite for fyue and fourti? And the Lord seide, Y schal not do a wei, if I schal fynde fyue and fourti there.
29 Akaongea naye tena, na kusema, “Itakuwaje ikiwa arobaini watapatikana pale?” Akajibu, “Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini.”
And eft Abraham seide to hym, But if fourti ben there, what schalt thou do? The Lord seide, Y schal not smyte for fourti.
30 Akasema, Tafadhali usikasirike, Bwana, nikiongea. Pengine thelathini watapatikana pale.” Akajibu, 'Sitafanya, ikiwa nitapata thelathini pale.”
Abraham seide, Lord, Y biseche, take thou not to indignacioun, if Y speke; what if thretti be foundun there? The Lord answerde, Y schal not do, if Y schal fynde thretti there.
31 Akasema, Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu! Pengine ishirini watapatikana pale.” Akajibu, “Sitaharibu kwa ajili ya hao ishirini.”
Abraham seide, For Y bigan onys, Y schal speke to my Lord; what if twenti be foundun there? The Lord seide, Y schal not sle for twenti.
32 Akasema, “Tafadhali usikasirike, Bwana, na nitasema jambo hili kwa mara ya mwisho. Huenda kumi wakaonekana kule.” Na akasema, sitaangamiza kwa ajili ya hao kumi.”
Abraham seide, Lord, Y biseche, be thou not wrooth, if Y speke yit onys; what if ten be founden there? The Lord seide, Y schal not do a wey for ten.
33 Yahwe akaendelea na njia yake mara tu baada ya kumaliza kuongea na Abraham, na Abraham akarudi nyumbani.
The Lord yede forth, after that he ceesside to speke to Abraham, and Abraham turnede ayen in to his place.

< Mwanzo 18 >