< Mwanzo 18 >
1 Yahwe alimtokea Abraham katika Mialoni ya Mamre, alipokua ameketi mlangoni pa hema wakati wa jua.
And the LORde apeared vnto him in the okegrove of Mamre as he sat in his tent doze in the heate of the daye.
2 Akatazama juu na, tazama, akaona wanaume watatu wamesimama mbele yake. Alipo waona, alikimbia kupitia mlango wa hema kuwalaki na kuinama chini hadi ardhini.
And he lyfte vp his eyes and looked: ad lo thre men stode not farr from hym. And whe he sawe them he ran agenst them from the tent dore and fell to the grounde
3 Akasema, “Bwana, kama nimepata upendelea machoni pako, nakuomba usinipite na kuniacha mtumishi wako.
and sayde: LORde yf I haue founde fauoure in thy syght goo not by thi seruaunte.
4 Naomba maji kidogo yaletwe, mnawe miguu yenu, na mjipumzishe chini ya mti.
Let a litle water be fett and wash youre fete and rest youre selves vnder the tree:
5 Nami acha nilete chakula kidogo, ili kwamba mjiburudishe wenyewe. Ndipo baadae mwaweza kwenda zenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.” Nao wakasema, “Fanya kama ulivyo sema.”
And I will fett a morsell of breed to comforte youre hartes wythall. And tha goo youre wayes for even therfore ar ye come to youre servaunte. And they answered: Do even so as thou hast sayde.
6 Kisha Abraham akaenda upesi hemani kwa Sara, na akasema, “Harakisha, chukua vipimo vitatu vya unga safi, uukande, na fanya mkate.”
And Abraha went a pace in to his tent vnto Sara ad sayde: make redy att once thre peckes of fyne meale kneade it and make cakes.
7 Kisha Abraham akakimbia kundini, akachukua ndama wa ng'ombe aliye laini na mzuri, na akampatia mtumishi na kwa haraka akamwandaa.
And Abraham ran vnto his beastes and fett a calfe that was tendre and good and gaue it vnto a yonge man which made it redy attonce.
8 Akatwaa siagi na maziwa na ndama aliye kwisha andaliwa, na akaweka chakula mbele yao, naye akasimama karibu nao chini ya mti wakati wanakula.
And he toke butter and mylcke and the calfe which he had prepared and sett it before them and stode hymselfe by them vnder the tree: and they ate.
9 Wakamwambia, “Mke wako Sara yuko wapi?” akajibu. “pale hemani.”
And they sayde vnto him: Where is Sara thy wife? And he sayde: in the tent.
10 akasema, “Hakika nitarejea kwako majira ya machipuko, na tazama Sara mkeo atakuwa na mtoto wa kiume.” Sara alikuwa akisikiliza mlangoni pa hema iliyokuwa nyuma yake.
And he sayde: I will come agayne vnto the as soone as the frute can lyue. And loo: Sara thy wife shall haue a sonne. That herde Sara out of the tent doore which was behind his backe.
11 Abraham na Sara walikuwa wazee, umri wao ulikuwa umeendelea sana, na Sara alikuwa amepita umri ambao mwanamke anaweza kuzaa watoto.
Abraham and Sara were both olde and well stryken in age and it ceased to be with Sara after the maner as it is wyth wyves.
12 Kwa hiyo Sara akajicheka mwenyewe, akijisemesha mwenyewe, “baada ya kuwa nimechakaa na bwana wangu ni mzee, je ni tapata furaha hii?”
And Sara laughed in hir selfe saynge: Now I am waxed olde shall I geue my selfe to lust and my lorde olde also?
13 Yahwe akamwambia Abraham, “Kwa nini Sara amecheka na kusema, Je ni kweli nitazaa mtoto, nikiwa mzee'?
Than sayd the LORde vnto Abraha: wherfore doth Sara laughe saynge: shal I of a suertie bere a childe now when I am olde?
14 Je kuna jambo lolote gumu sana kwa Yahwe? Itakuwa katika wakati nilioweka mimi majira ya machipuko, nitarejea kwako. Majira haya mwakani Sara atakuwa na mtoto wa kiume.”
is the thinge to harde for the LORde to do? In the tyme appoynted will I returne vnto the as soone as the frute can haue lyfe And Sara shall haue a sonne.
15 Kisha Sara akakataa na kusema, “sikucheka,” kwa kuwa aliogopa. Yahwe akasema, “hapana ulicheka.”
Than Sara denyed it saynge: I laughed not for she was afrayde. But he sayde: yes thou laughtest.
16 Kisha wale wanaume walisimama kuondoka na wakatazama chini kuelekea Sodoma. Abraham akafuatana nao kuona njia yao.
Than the men stode vp from thence ad loked towarde Sodome. And Abraham went with them to brynge them on the waye.
17 Lakini Yahwe akasema, Je ni mfiche Abraham kile ninacho kusudia kufanya,
And the LORde sayde: Can I hyde from Abraham that thinge which I am aboute to do
18 Ikiwa kwa hakika Abraham atakuwa mkuu na taifa lenye nguvu, na katika yeye mataifa yote ya dunia watabarikiwa?
seynge that Abraham shall be a great ad a myghtie people and all the nations of the erth shalbe blessed in him?
19 Kwa kuwa nimemchagua ili awaelekeze wanawe na nyumba yake baada yake waishike njia ya Yahwe, watende utakatifu na haki, ili kwamba Yahwe ampatie Abraham yale aliyo yasema kwake.”
For I knowe him that he will commaunde his childern and his housholde after him yt they kepe the waye of the LORde to do after righte and conscyence that the LORde may brynge vppon Abraham that he hath promysed him.
20 Kisha Yahwe akasema, “Kwa sababu kilio cha Sodoma na Gomora ni kikuu, na kwa kuwa dhambi yao ni kubwa,
And the LORde sayde? The crie of Sodome and Gomorra is great and there synne is excedynge grevous.
21 sasa nitashuka pale na kuona kilio kilicho nifikia dhidi yake, ikiwa kweli wamefanya au hawakufanya, nitajua.”
I will go downe and see whether they haue done all to gedder acordynge to that crye which is come vnto me or not that I may knowe.
22 Kwa hiyo wale wanaume wakageuka toka pale, na kuelekea Sodoma, lakini Abraham akabaki amesimama mbele ya Yahwe.
And the me departed thece and went to Sodomeward. But Abraham stode yet before ye LORde
23 Kisha Abraham alikaribia na kusema, “Je utawafutilia mbali watakatifu pamoja na waovu?
and drewe nere and saydeWylt thou destroy the rightwes with the wyked?
24 Huenda wakawepo wenye haki hamsini katika mji. Je utawakatilia mbali na usiuache mji kwa ajili ya hao watakatifu hamsini walioko hapo?
Yf there be. l. rightwes within the cyte wilt thou destroy it and not spare the place for the sake of. l. rightwes that are therin?
25 Hasha usifanye hivyo, kuwauwa watakatifu pamoja na waovu, ili kwamba watakatifu watendewe sawa na waovu. Hasha! Je muhukumu wa ulimwengu wote hatatenda haki?”
That be farre from the that thou shuldest do after thys maner to sley the rightwes with the weked ad that the rightwes shulde be as the weked: that befarre from the. Shulde not the iudge of all ye worlde do acordynge to righte?
26 Yahwe akasema, “Katika Sodoma nikipata watakatifu hamsini kwenye mji, nita uacha mji wote kwa ajili ya hao.”
And the LORde sayde: Yf I fynde in Sodome. l. rightwes within the cyte I will spare all the place for their sakes.
27 Abraham akajibu na kusema, “Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu, hata kama mimi ni mavumbi na majivu!
And Abraham answered and sayde: beholde I haue taken vppon me to speake vnto ye LORde ad yet am but dust ad asshes.
28 Itakuwaje ikiwa kuna watano pungufu katika idadi ya hao watakatifu hamsini? Je utaangamiza mji wote kwa upungufu wa hao watano?” Akasema, “Sitaangamiza, ikiwa nitapata watu arobaini na watano pale.”
What though there lacke. v. of. l. rightwes wylt thou destroy all the cyte for lacke of. v? And he sayde: Yf I fynde there. xl. and. v. I will not destroy them.
29 Akaongea naye tena, na kusema, “Itakuwaje ikiwa arobaini watapatikana pale?” Akajibu, “Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini.”
And he spake vnto him yet agayne and sayde: what yf there be. xl. foude there: And he sayde: I wyll not do it for forties sake.
30 Akasema, Tafadhali usikasirike, Bwana, nikiongea. Pengine thelathini watapatikana pale.” Akajibu, 'Sitafanya, ikiwa nitapata thelathini pale.”
And he sayde: O let not my LORde be angrye that I speake. What yf there be foude. xxx. there? And he sayde: I will not do it yf I finde. xxx. there.
31 Akasema, Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu! Pengine ishirini watapatikana pale.” Akajibu, “Sitaharibu kwa ajili ya hao ishirini.”
And be sayde: Oh se I haue begonne to speake vnto my LORde what yf there be. xx. founde there? And he sayde: I will not distroy the for tweties sake.
32 Akasema, “Tafadhali usikasirike, Bwana, na nitasema jambo hili kwa mara ya mwisho. Huenda kumi wakaonekana kule.” Na akasema, sitaangamiza kwa ajili ya hao kumi.”
And he sayde: O let not my LORde be angrye that I speake yet but eue once more only. What yf ten be founde there? And he sayde: I will not destroy the for. x. sake.
33 Yahwe akaendelea na njia yake mara tu baada ya kumaliza kuongea na Abraham, na Abraham akarudi nyumbani.
And the LORde wet his waye as soone as he had lefte comenynge with Abraha. And Abraham returned vnto his place