< Mwanzo 17 >

1 Wakati Abram alipokuwa na umri wa miaka tisini na tisa, Yahwe alimtokea Abram na akamwambia, “Mimi ni Mungu wa uwezo. Uende mbele yangu, na uwe mkamilifu.
و چون ابرام نود و نه ساله بود، خداوندبر ابرام ظاهر شده، گفت: «من هستم خدای قادر مطلق، پیش روی من بخرام و کامل شو،۱
2 Kisha nitalithibitisha agano langu kati yangu mimi na wewe, na nitakuzidisha sana.
و عهد خویش را در میان خود و تو خواهم بست، و تو را بسیاربسیار کثیر خواهم گردانید.»۲
3 Abram akainama uso wake hadi chini ardhini na Mungu akazungumza naye, akisema,
آنگاه ابرام به روی در‌افتاد و خدا به وی خطاب کرده، گفت:۳
4 “Mimi, tazama, agano langu liko nawe. Utakuwa baba wa mataifa mengi.
«اما من اینک عهد من با توست و توپدر امت های بسیار خواهی بود.۴
5 Wala jina lako halitakuwa tena Abram, bali jina lako litakuwa Abraham - kwa kuwa ninakuchagua kuwa baba wa mataifa mengi.
و نام تو بعد ازاین ابرام خوانده نشود بلکه نام تو ابراهیم خواهدبود، زیرا که تو را پدر امت های بسیار گردانیدم.۵
6 Nitakufanya uwe na uzao mwingi zaidi, na nitakufanya mataifa, na wafalme watatoka kwako.
و تو را بسیار بارور نمایم و امت‌ها از تو پدیدآورم و پادشاهان از تو به وجود آیند.۶
7 Nitaimarisha agao langu kati yangu mimi na wewe na uzao wako baada yako, katika vizazi vyao vyote kwa agano la milele, nitakuwa Mungu kwako na kwa wazao wako baada yako.
و عهدخویش را در میان خود و تو، و ذریتت بعد از تو، استوار گردانم که نسلا بعد نسل عهد جاودانی باشد، تا تو را و بعد از تو ذریت تو را خدا باشم.۷
8 Nitakupa wewe, na wazao wako baada yako, nchi ambayo ulikuwa unaishi, nchi yote ya Kanaani, kuwa miliki ya milele, na nitakuwa Mungu wao.”
وزمین غربت تو، یعنی تمام زمین کنعان را، به تو و بعد از تو به ذریت تو به ملکیت ابدی دهم، وخدای ایشان خواهم بود.»۸
9 Kisha Mungu akamwambia Abraham, “nawe lazima ulishike agano langu, wewe pamoja na uzao wako baada yako kwa vizazi vyao.
پس خدا به ابراهیم گفت: «و اما تو عهد مرا نگاه دار، تو و بعد از توذریت تو در نسلهای ایشان.۹
10 Hili ndilo agano langu, ambalo utalishika, kati yangu na wewe na wazao wako baada yako: Kila mwanaume wa kwenu lazima atahiriwe.
این است عهد من که نگاه خواهید داشت، در میان من و شما و ذریت تو بعد از تو هر ذکوری از شما مختون شود،۱۰
11 Lazima mtatahiriwa katika nyama ya govi la ngozi ya mbele, na hii itakuwa ishara ya agano kati yangu mimi na ninyi.
وگوشت قلفه خود را مختون سازید، تا نشان آن عهدی باشد که در میان من و شماست.۱۱
12 Kila mwanaume wa kwenu aliye na umri wa siku nane lazima atahiriwe, katika vizazi ya watu wenu. Hii ni pamoja na yule azaliwaye katika nyumba yako na yeye ambaye amenunuliwa kwa fedha kutoka kwa mgeni yeyote ambaye si mmoja wa wazao wako.
هر پسرهشت روزه از شما مختون شود. هر ذکوری درنسلهای شما، خواه خانه زاد خواه زرخرید، ازاولاد هر اجنبی که از ذریت تو نباشد،۱۲
13 Mtu ambaye amezaliwa katika nyumba yako na yule aliye nunuliwa kwa fedha yako lazima atahiriwe. Hivyo agano langu litakuwa katika mwili wenu kuwa agano la milele.
هرخانه زاد تو و هر زر خرید تو البته مختون شود تاعهد من در گوشت شما عهد جاودانی باشد.۱۳
14 Mwanaume yeyote asiye tahiriwa katika mwili govi la ngozi yake ya mbele atatengwa na watu wake. Amevunja agano langu.”
واما هر ذکور نامختون که گوشت قلفه او ختنه نشود، آن کس از قوم خود منقطع شود، زیرا که عهد مرا شکسته است.»۱۴
15 Mungu akamwambia Abraham, “kwa habari ya Sarai mkeo, usimuite tena Sarai. Badala yake jina lake litakuwa Sara.
و خدا به ابراهیم گفت: «اما زوجه توسارای، نام او را سارای مخوان، بلکه نام او ساره باشد.۱۵
16 Nitambariki, na nitakupatia mtoto wa kiume kwake. Nitambariki, na atakuwa mama wa mataifa. Wafalme wa watu wa mataifa watapatikana kutokana na yeye.
و او را برکت خواهم داد و پسری نیز ازوی به تو خواهم بخشید. او را برکت خواهم داد وامتها از وی به وجود خواهند آمد، و ملوک امتهااز وی پدید خواهند شد.»۱۶
17 Kisha Abraham akainama uso wake hadi ardhini, na akacheka, akasema moyoni mwake, Je yawezekana mtoto azaliwe kwa mwanaume ambaye ana umri wa miaka miamoja? na Je Sara, ambaye ana umri wa miaka tisini anaweza kuzaa mwana?”
آنگاه ابراهیم به روی در‌افتاده، بخندید و در دل خود گفت: «آیابرای مرد صد ساله پسری متولد شود و ساره درنود سالگی بزاید؟»۱۷
18 Abraham akamwambia Mungu, “Lau Ishmaeli angeweza kuishi kabla yako!”
و ابراهیم به خدا گفت: «کاش که اسماعیل در حضور تو زیست کند.»۱۸
19 Mungu akasema, Hapana, Sarai mkeo atakuzalia mtoto wa kiume na utamwita jina lake Isaka. Nita imarisha agano langu na yeye kama agano la milele pamoja na uzao wake baada yake.
خدا گفت: «به تحقیق زوجه ات ساره برای توپسری خواهد زایید، و او را اسحاق نام بنه، و عهدخود را با وی استوار خواهم داشت، تا با ذریت اوبعد از او عهد ابدی باشد.۱۹
20 Na kwa habari ya Ishmaeli nimekusikia. Tazama, ninambariki, na nitamfanya kuwa na uzao na kumzidisha maradufu. Atakuwa baba wa viongozi kumi na mbili wa makabila, na nitamfanya kuwa taifa kuu.
و اما در خصوص اسماعیل، تو را اجابت فرمودم. اینک او را برکت داده، بارور گردانم، و او را بسیار کثیر گردانم. دوازده رئیس از وی پدید آیند، و امتی عظیم ازوی بوجود آورم.۲۰
21 Lakini agano langu nitalifanya imara na Isaka, ambaye Sarai atazaa kwako majira haya mwakani.”
لکن عهد خود را با اسحاق استوار خواهم ساخت، که ساره او را بدین وقت در سال آینده برای تو خواهد زایید.»۲۱
22 Alipo kuwa amemaliza kuzungumza naye, Mungu akaondoka kwa Abraham.
و چون خدا از سخن‌گفتن با وی فارغ شد، از نزد ابراهیم صعود فرمود.۲۲
23 Kisha Abraham akamtwaa Ishmaeli mwanawe, na wote ambao walizaliwa katika nyumba yake, na wote ambao walinunuliwa kwa fedha yake, kila mwanaume miongoni mwa watu wa nyumba ya Abraham, walitahiriwa mwili wa magovi ya ngozi ya mbele katika siku iyo hiyo, kama Mungu alivyo kuwa amesema.
و ابراهیم پسر خود، اسماعیل وهمه خانه زادان و زرخریدان خود را، یعنی هرذکوری که در خانه ابراهیم بود، گرفته، گوشت قلفه ایشان را در همان روز ختنه کرد، چنانکه خدا به وی امر فرموده بود.۲۳
24 Abraham alikuwa na umri wa miaka tisini na tisa alipotahiriwa katika mwili wa govi la ngozi yake ya mbele.
و ابراهیم نود و نه ساله بود، وقتی که گوشت قلفه‌اش مختون شد.۲۴
25 Na Ishmaeli mwanawe alikuwa na umri wa miaka kumi na tatu alipotahiriwa katika mwili wa govi la ngozi yake ya mbele.
و پسرش، اسماعیل سیزده ساله بود هنگامی که گوشت قلفه‌اش مختون شد.۲۵
26 Siku ile ile ambayo wote wawili Abraham na Ishmael mwanawe walipotahiriwa, ndipo
در همان روزابراهیم و پسرش، اسماعیل مختون گشتند.۲۶
27 wanaume wote wa nyumba yake walitahiriwa pia, hawa ni pamoja na wale waliozaliwa katika nyumba ile na wale walionunuliwa kwa fedha kutoka kwa mgeni.
وهمه مردان خانه‌اش، خواه خانه زاد، خواه زرخرید از اولاد اجنبی، با وی مختون شدند.۲۷

< Mwanzo 17 >