< Mwanzo 17 >
1 Wakati Abram alipokuwa na umri wa miaka tisini na tisa, Yahwe alimtokea Abram na akamwambia, “Mimi ni Mungu wa uwezo. Uende mbele yangu, na uwe mkamilifu.
Alors qu'Abram était âgé de quatre-vingt-dix-neuf ans, Yahvé apparut à Abram et lui dit: « Je suis le Dieu tout-puissant. Marche devant moi et sois irréprochable.
2 Kisha nitalithibitisha agano langu kati yangu mimi na wewe, na nitakuzidisha sana.
Je conclurai mon alliance entre moi et toi, et je te multiplierai à l'infini. »
3 Abram akainama uso wake hadi chini ardhini na Mungu akazungumza naye, akisema,
Abram tomba sur sa face. Dieu lui parla, en disant:
4 “Mimi, tazama, agano langu liko nawe. Utakuwa baba wa mataifa mengi.
« Quant à moi, voici que mon alliance est avec toi. Tu seras le père d'une multitude de nations.
5 Wala jina lako halitakuwa tena Abram, bali jina lako litakuwa Abraham - kwa kuwa ninakuchagua kuwa baba wa mataifa mengi.
Ton nom ne sera plus Abram, mais ton nom sera Abraham, car je t'ai établi père d'une multitude de nations.
6 Nitakufanya uwe na uzao mwingi zaidi, na nitakufanya mataifa, na wafalme watatoka kwako.
Je te rendrai extrêmement fécond, et je ferai de toi des nations. Des rois sortiront de toi.
7 Nitaimarisha agao langu kati yangu mimi na wewe na uzao wako baada yako, katika vizazi vyao vyote kwa agano la milele, nitakuwa Mungu kwako na kwa wazao wako baada yako.
J'établirai mon alliance entre moi et toi, et tes descendants après toi, de génération en génération, comme une alliance éternelle, pour être un Dieu pour toi et pour tes descendants après toi.
8 Nitakupa wewe, na wazao wako baada yako, nchi ambayo ulikuwa unaishi, nchi yote ya Kanaani, kuwa miliki ya milele, na nitakuwa Mungu wao.”
Je vous donnerai, à vous et à votre postérité après vous, le pays où vous voyagez, tout le pays de Canaan, comme une possession éternelle. Je serai leur Dieu. »
9 Kisha Mungu akamwambia Abraham, “nawe lazima ulishike agano langu, wewe pamoja na uzao wako baada yako kwa vizazi vyao.
Dieu dit à Abraham: « Pour toi, tu garderas mon alliance, toi et ta postérité après toi, de génération en génération.
10 Hili ndilo agano langu, ambalo utalishika, kati yangu na wewe na wazao wako baada yako: Kila mwanaume wa kwenu lazima atahiriwe.
Voici mon alliance, que tu garderas, entre moi et toi, et ta postérité après toi. Tout mâle parmi vous sera circoncis.
11 Lazima mtatahiriwa katika nyama ya govi la ngozi ya mbele, na hii itakuwa ishara ya agano kati yangu mimi na ninyi.
Vous serez circoncis dans la chair de votre prépuce. Ce sera un signe de l'alliance entre moi et vous.
12 Kila mwanaume wa kwenu aliye na umri wa siku nane lazima atahiriwe, katika vizazi ya watu wenu. Hii ni pamoja na yule azaliwaye katika nyumba yako na yeye ambaye amenunuliwa kwa fedha kutoka kwa mgeni yeyote ambaye si mmoja wa wazao wako.
Celui qui aura huit jours sera circoncis parmi vous, tout mâle, de génération en génération, qu'il soit né dans la maison ou acheté à prix d'argent à un étranger qui n'est pas de votre race.
13 Mtu ambaye amezaliwa katika nyumba yako na yule aliye nunuliwa kwa fedha yako lazima atahiriwe. Hivyo agano langu litakuwa katika mwili wenu kuwa agano la milele.
Celui qui est né dans ta maison, et celui qui a été acheté avec ton argent, doit être circoncis. Mon alliance sera dans ta chair pour une alliance éternelle.
14 Mwanaume yeyote asiye tahiriwa katika mwili govi la ngozi yake ya mbele atatengwa na watu wake. Amevunja agano langu.”
Le mâle incirconcis qui n'est pas circoncis dans la chair de son prépuce, cette âme sera retranchée de son peuple. Il a rompu mon alliance. »
15 Mungu akamwambia Abraham, “kwa habari ya Sarai mkeo, usimuite tena Sarai. Badala yake jina lake litakuwa Sara.
Dieu dit à Abraham: « Pour ce qui est de Saraï, ta femme, tu ne l'appelleras pas Saraï, mais son nom sera Sara.
16 Nitambariki, na nitakupatia mtoto wa kiume kwake. Nitambariki, na atakuwa mama wa mataifa. Wafalme wa watu wa mataifa watapatikana kutokana na yeye.
Je la bénirai, et en plus je te donnerai un fils par elle. Oui, je la bénirai, et elle sera une mère de nations. Les rois des peuples viendront d'elle. »
17 Kisha Abraham akainama uso wake hadi ardhini, na akacheka, akasema moyoni mwake, Je yawezekana mtoto azaliwe kwa mwanaume ambaye ana umri wa miaka miamoja? na Je Sara, ambaye ana umri wa miaka tisini anaweza kuzaa mwana?”
Alors Abraham tomba sur sa face et se mit à rire, et il dit en son cœur: « Naîtra-t-il un enfant à celui qui est âgé de cent ans? Sara, qui a quatre-vingt-dix ans, accouchera-t-elle? »
18 Abraham akamwambia Mungu, “Lau Ishmaeli angeweza kuishi kabla yako!”
Abraham dit à Dieu: « Oh, si Ismaël pouvait vivre devant toi! »
19 Mungu akasema, Hapana, Sarai mkeo atakuzalia mtoto wa kiume na utamwita jina lake Isaka. Nita imarisha agano langu na yeye kama agano la milele pamoja na uzao wake baada yake.
Dieu dit: « Non, mais Sara, ta femme, t'enfantera un fils. Tu lui donneras le nom d'Isaac. J'établirai mon alliance avec lui comme une alliance éternelle pour sa descendance après lui.
20 Na kwa habari ya Ishmaeli nimekusikia. Tazama, ninambariki, na nitamfanya kuwa na uzao na kumzidisha maradufu. Atakuwa baba wa viongozi kumi na mbili wa makabila, na nitamfanya kuwa taifa kuu.
Quant à Ismaël, je t'ai entendu. Voici, je l'ai béni, je le rendrai fécond et je le multiplierai à l'infini. Il sera le père de douze princes, et je ferai de lui une grande nation.
21 Lakini agano langu nitalifanya imara na Isaka, ambaye Sarai atazaa kwako majira haya mwakani.”
Mais j'établirai mon alliance avec Isaac, que Sarah t'enfantera l'année prochaine à cette époque précise. »
22 Alipo kuwa amemaliza kuzungumza naye, Mungu akaondoka kwa Abraham.
Quand il eut fini de parler avec lui, Dieu s'éloigna d'Abraham.
23 Kisha Abraham akamtwaa Ishmaeli mwanawe, na wote ambao walizaliwa katika nyumba yake, na wote ambao walinunuliwa kwa fedha yake, kila mwanaume miongoni mwa watu wa nyumba ya Abraham, walitahiriwa mwili wa magovi ya ngozi ya mbele katika siku iyo hiyo, kama Mungu alivyo kuwa amesema.
Abraham prit son fils Ismaël, tous ceux qui étaient nés dans sa maison et tous ceux qu'il avait achetés avec son argent, tous les mâles parmi les hommes de la maison d'Abraham, et il circoncit la chair de leur prépuce le même jour, comme Dieu le lui avait dit.
24 Abraham alikuwa na umri wa miaka tisini na tisa alipotahiriwa katika mwili wa govi la ngozi yake ya mbele.
Abraham était âgé de quatre-vingt-dix-neuf ans lorsqu'il fut circoncis dans la chair de son prépuce.
25 Na Ishmaeli mwanawe alikuwa na umri wa miaka kumi na tatu alipotahiriwa katika mwili wa govi la ngozi yake ya mbele.
Ismaël, son fils, avait treize ans lorsqu'il fut circoncis dans la chair de son prépuce.
26 Siku ile ile ambayo wote wawili Abraham na Ishmael mwanawe walipotahiriwa, ndipo
Le même jour, Abraham et Ismaël, son fils, furent circoncis.
27 wanaume wote wa nyumba yake walitahiriwa pia, hawa ni pamoja na wale waliozaliwa katika nyumba ile na wale walionunuliwa kwa fedha kutoka kwa mgeni.
Tous les hommes de sa maison, ceux qui étaient nés dans la maison et ceux qui avaient été achetés à prix d'argent à un étranger, furent circoncis avec lui.