< Mwanzo 16 >

1 Kisha Sarai mke wa Abram, alikuwa hajamzalia mtoto, lakini alikuwa na mtumishi wa kike, Mmisri ambaye jina lake aliitwa Hajiri.
Abrams Hustru Saraj fødte ham intet Barn. Men Saraj havde en Ægyptisk Trælkvinde ved Navn Hagar;
2 Kwa hiyo Sarai akamwambia Abram, “Tazama, Yahwe hajanifanya mimi kuwa na watoto. Nenda na ulale na mtumishi wangu. Ili kwamba niweze kupata watoto kupitia yeye.” Abram akasikiliza sauti ya Sarai.
og Saraj sagde til Abram: »HERREN har jo nægtet mig Børn; gaa derfor ind til min Trælkvinde, maaske kan jeg faa en Søn ved hende!« Og Abram adlød Saraj.
3 Ilikuwa baada ya Abram kuishi miaka kumi katika nchi ya Kanaani ndipo Sarai, mke wa Abram, alimtoa Hajiri yule mmisri mtumishi wake kwa mume wake awe kama mke wake.
Saa tog Abrams Hustru Saraj sin Trælkvinde, Ægypterinden Hagar, efter at Abram havde boet ti Aar i Kana'ans Land, og gav sin Mand Abram hende til Hustru;
4 Kwa hiyo akawa na mahusiano na Hajiri, na akabeba mimba. Na alipoona kuwa amebeba mimba, akamdharau bibi yake.
og han gik ind til Hagar, og hun blev frugtsommelig. Men da hun saa, at hun var frugtsommelig, lod hun haant om sin Herskerinde.
5 Kisha Sarai akamwambia Abram, “Jambo hili baya kwangu ni kwa sababu yako. Nilimtoa mtumishi wangu wa kike katika kumbatio lako. Na alipoona kuwa amebeba mimba, nilidharaulika machoni pake. Na sasa acha Yahwe aamuwe kati yangu na wewe.”
Da sagde Saraj til Abram: »Min Krænkelse komme over dig! Jeg lagde selv min Trælkvinde i din Favn, og nu hun ser, at hun skal føde, lader hun haant om mig; HERREN være Dommer mellem mig og dig!«
6 Lakini Abram akamwambia Sarai, “Tazama, hapa, mtumishi wako yuko katika uwezo wako, fanya unachofikiri ni kizuri sana kwake.” Kwa hiyo Sarai akakabiliana naye kwa ukatili, na akatoroka.
Abram svarede Saraj: »Din Trælkvinde er i din Haand, gør med hende, hvad du finder for godt!« Da plagede Saraj hende, saa hun flygtede for hende.
7 Malaika wa Yahwe akamkuta karibu na chemichemi ya maji katika jangwa, chemichemi iliyo katika njia kuelekea Shuri.
Men HERRENS Engel fandt hende ved Vandkilden i Ørkenen, ved Kilden paa Vejen til Sjur;
8 Akasema, Hajiri, mtumishi wa Sarai, umetoka wapi na unakwenda wapi?” Na akasema, ninamtoroka bibi yangu Sarai.”
og han sagde: »Hvorfra kommer du, Hagar, Sarajs Trælkvinde, og hvor gaar du hen?« Hun svarede: »Jeg flygter for min Herskerinde Saraj!«
9 Malaika wa Yahwe akamwambia, “Rudi kwa bibi yako, na unyenyekee chini ya mamlaka yake.”
Da sagde HERRENS Engel til hende: »Vend tilbage til din Herskerinde og find dig i hendes Mishandling!«
10 Kisha Malaika wa Yahwe akamwambia, “Nitazidisha uzao wako maradufu, kiasi kwamba watakuwa wengi wasioweza kuhesabika.”
Og HERRENS Engel sagde til hende: »Jeg vil gøre dit Afkom saa talrigt, at det ikke kan tælles.«
11 Malaika wa Yahwe pia akamwambia, “Tazama, wewe unamimba, na utazaa mtoto kiume, na utamwita jina lake Ishmaeli, kwasabab Yahwe amesikia mateso yako.
Og HERRENS Engel sagde til hende: »Se, du er frugtsommelig, og du skal føde en Søn, som du skal kalde Ismael, thi HERREN har hørt, hvad du har lidt;
12 Atakuwa punda mwitu wa mtu. Atakuwa adui dhidi ya kila mtu, na kila mtu atakuwa adui yake, na ataishi kando na ndugu zake wote.”
og han skal blive et Menneske-Vildæsel, hvis Haand er mod alle, og alles Haand mod ham, og han skal ligge i Strid med alle sine Frænder!«
13 Kisha akamwita jina hili Yahwe aliye zungumza naye, “Wewe ni Mungu unionaye mimi,” kwa kuwa alisema, “je ninaendelea kweli kuona, hata baada ya kuwa ameniona?”
Saa gav hun HERREN, der havde talet til hende, Navnet: Du er en Gud, som ser; thi hun sagde: »Har jeg virkelig her set et Glimt af ham, som ser mig?«
14 Kwa hiyo kisima kiliitwa Beerlahairori; Tazama, kiko kati ya Kadeshi na Beredi.
Derfor kaldte man Brønden Be'er-lahaj-ro'i; den ligger mellem Kadesj og Bered.
15 Hajiri akamzalia Abram mwana wa kiume, na Abram akamwita mwanawe, ambaye Hajiri amemzaa jina, Ishmaeli.
Og Hagar fødte Abram en Søn, og Abram kaldte Sønnen, Hagar fødte ham, Ismael.
16 Abram alikuwa na umri wa miaka themanini na sita wakati Hajiri alipomzaa Ishmaeli kwa Abram.
Abram var seks og firsindstyve Aar gammel, da Hagar fødte ham Ismael.

< Mwanzo 16 >