< Mwanzo 14 >
1 Ikiwa katika siku za Amrafeli, mfalme wa shinari, Arioko, mfalme wa Elasari, Kedorlaoma, mfalme wa Elam na Tidali, mfalme wa Goimu,
Or, il arriva que pendant les règnes d'Amarphal, roi de Sennaar, et d'Arioch, roi d'Ellasar, Chodollogomor, roi d'Élam, et Thargal, roi des nations.
2 walifanya vita dhidi ya Bera mfalme wa Sodoma, Birsha, mfalme wa Gomora, Shinabu, mfalme wa Adma, Shemeberi, mfalme wa Seboim, na mfalme wa Bela(pia ikiitwa Soari).
Firent la guerre contre Balla, roi de Sodome, et Barsa, roi de Gomorrhe, et Sennaar, roi d'Adama, et Symobor, roi de Séboïm, et le roi de Balac (aujourd'hui Ségor).
3 Hawa wafalme watano wa mwisho waliungana pamoja katika bonde la Sidim (pia likiitwa bahari ya chumvi).
Tous ces derniers se confédérèrent dans le vallon Salé (aujourd'hui mer des Sels).
4 Kwa miaka kumi na mbili walimtumikia Kedorlaoma, lakini katika mwaka wa kumi na tatu waliasi.
Pendant douze ans ils avaient servi Chodollogomor; mais dans la treizième année ils se révoltèrent.
5 Kisha katika mwaka wa kumi na nne, Kedorlaoma na wafalme waliokuwa pamoja nae walikuja na kuwashambulia Warefai katika Ashteroth Karnaimu, na Wazuzi katika Hamu, Waemi katika Shawe Kiriathaimu,
Et, en la quatorzième année, Chodollogomor arriva avec les rois ses alliés; ils vainquirent les géants d'Asvaroth et de Carnaï, ainsi que les nations puissantes leurs alliées, et les Omméens de la ville de Savé,
6 na Wahori katika mlima wao wa Seiri, mpaka El Parani iliyo karibu na jangwa.
Et les Horrhéens qui habitent les montagnes de Séir, jusqu'au térébinthe de Phara, dans le désert.
7 Kisha wakarudi wakaja En Misifati (Pia ikiitwa Kadeshi), na kuishinda nchi yote ya Waamaleki, na pia Waamori ambao waliishi Hasasoni Tamari.
Puis, s'étant retournés, ils vinrent vers la fontaine du jugement, aujourd'hui Cadès, et ils vainquirent tous les chefs d'Amalec ainsi que les Amorrhéens qui habitent Asason-Thamar.
8 Kisha mfalme wa Sodoma, mfalme wa Gomora, mfalme wa Adma, mfalme wa Seboim, na mfalme wa Bela (pia ikiitwa Soari) walikwenda na kuandaa vita
Mais le roi de Sodome sortit, et avec lui le roi de Gomorrhe, le roi d'Adama, le roi de Séboïm, le roi de Balac, aujourd'hui Ségor, et ils se rangèrent en bataille dans le vallon Salé.
9 dhidi ya Kadorlaoma, mfalme wa Elam, Tidali mfalme wa Goim, Amrafeli, mfalme wa Shinari, Arioki, mfalme wa Elasari; wafme wanne dhidi ya wale watano.
Contre Chodollogomor, roi d'Élam, Thargal, roi des nations, Amarphal, roi de Sennaar, et Arioch, roi d'Ellabar; cinq rois contre quatre.
10 Na sasa bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami, na wafalme wa Sodoma na Gomora walipokimbia, wakaanguka pale. Wale waliosalia wakakimbilia milimani.
Or, le vallon Salé n'était que puits de bitume; bientôt le roi de Sodome s'enfuit avec le roi de Gomorrhe; ils furent vaincus, et ceux qui survécurent s'enfuirent dans les montagnes.
11 Kwa hiyo adui akachukua mali zote za Sodoma na Gomora na vyakula vyao vyote, na wakaenda zao,
Les vainqueurs prirent tous les chevaux de ceux de Sodome, tous leurs vivres; et ils partirent.
12 walipoondoka, wakamchukua pia Lutu, mtoto wa ndugu yake na Abram ambaye aliishi Sodoma, pamoja na mali zake zote.
Ils prirent aussi, avec tout son avoir, Lot, fils du frère d'Abram, car il habitait Sodome; et ils s'éloignèrent.
13 Mmoja ambaye alitoroka alikuja na kumwambia Abram mwebrania. Alikuwa anaishi katika mialoni ya Mamre, mwamori ambaye alikuwa ni ndugu wa Eshkoli na Aneri ambao walikuwa washirika wa Abram.
Or, l'un de ceux qui s'étaient sauvés, survenant, apprit ces choses à Abram, le passager sur cette terre, qui demeurait auprès du chêne de l'Amorrhéen Membré, frère d'Eschol, et frère d'Onan, tous alliés d'Abram.
14 Abram aliposikia kuwa maadui wamemteka ndugu yake, akawaongoza wanaume waliofunzwa na kuzaliwa nyumbani mwake 318 na akawaongoza hadi Dani.
Celui-ci, ayant appris que son neveu Lot était captif, compta ses serviteurs au nombre de trois cent dix-huit, et il poursuivit les ravisseurs jusqu'à Dan.
15 Akawagawanya watu wake dhidi yao usiku na kuwavamia, na kuwafukuza mpaka Hoba, ambayo iko kaskazini mwa Dameski.
La nuit venue, il tomba sur eux, avec ses serviteurs, les battit, et les chassa jusqu'à Hoba, qui est à la gauche de Damas.
16 Kisha akarudisha mali zote, pia akamrudisha ndugu yake Lutu na mali zake, pamoja na wanawake na watu wengine.
Il ramena tous les chevaux de Sodome, Lot son neveu, tous ses serviteurs, les femmes, et le peuple.
17 Baada ya Abram kurudi kutoka kumpiga Kadorlaoma na wafalme waliokuwa pamoja nae, mfalme wa Sodoma akatoka kuonana nae katika bonde la Shawe (pia iliitwa bonde la mfalme).
Le roi de Sodome sortit alors à sa rencontre, après avoir échappé au carnage fait par Chodollogomor et les rois ses alliés, dans la vallée de Saby (c'était le champ de bataille des rois).
18 Melkizedeki, mfalme wa Salem, akaleta mkate na divai. Alikuwa ni kuhani wa Mungu aliye juu sana.
Et Melchisédech, roi de Salem (Jérusalem), offrit des pains et du vin; car il était prêtre du Dieu Très-Haut.
19 Alimbariki akisema, “Abarikiwea Abram na Mungu aliye juu sana, muumba wa mbingu na nchi.
Il bénit Abram, en disant: Béni soit Abram du Dieu Très-Haut qui a créé le ciel et la terre.
20 Abarikiwe Mungu aliye juu sana, ambaye amekupatia adui zako katika mikono yako.” Kisha Abram akampatia sehemu ya kumi ya kila kitu.
Béni soit le Dieu Très -Haut qui t'a soumis tes ennemis. Et Abram lui donna la dîme de toutes choses.
21 Mfalme wa Sodama akamwambia Abram, “Nipatie watu, na ujichukulie wewe mwenyewe mali.”
Le roi de Sodome dit à Abram: Donne-moi les hommes, et prends pour toi les chevaux.
22 Abram akamwambia mfalme wa Sodoma, “Nimeinua juu mkono wangu kwa Yahwe, Mungu aliye juu sana, muumbaji wa mbingu na nchi,
Abram dit au roi de Sodome: J'étendrai la main vers le Seigneur Dieu, le Très-Haut qui a créé le ciel et la terre,
23 kwamba sitachukua uzi wala gidamu ya kiatu, au kitu chochote ambacho ni chako, 'ili kwamba usiseme, nimemfanya Abram kuwa tajiri.'
Pour attester que je ne veux pour moi rien de ce qui t'appartient, depuis la corde jusqu'à la courroie de la sandale, de peur que tu ne puisses dire: J'ai enrichi Abram.
24 Sitachukua chochote isipokuwa kile ambacho vijana wamekula na sehemu za watu waliokwenda nami. Aneri, Eskoli, na Mamre na wachukue sehemu zao.”
J'excepte ce que les jeunes gens ont mangé, et la part de mes alliés Eschol, Onan et Membré, qui prendront ce qui leur revient.