< Mwanzo 13 >
1 Kwa hiyo Abram akaondoka akatoka Misri na akaenda Negebu, Yeye, mke wake, na vyote alivyokuwa navyo. Lutu pia akaenda pamoja naye.
Abram remonta d’Égypte vers le Midi, lui, sa femme et tout ce qui lui appartenait, et Lot avec lui.
2 Na sasa Abram alikuwa tajiri wa mifugo, fedha na dhahabu.
Or Abram était fort riche en troupeaux, en argent et en or.
3 Aliendelea na safari yake kutoka Negebu hadi Betheli, mahali ambapo hema yake ilikuwa tangu mwanzo, kati ya Betheli na mji wa Ai.
Puis il alla, de campement en campement, du Midi jusqu’à Béthel, jusqu’au lieu où il avait la première fois dressé sa tente, entre Béthel et Haï,
4 Akaenda mahali ambapo madhabahu ilikuwa imejengwa mwanzoni. Hapa akaliitia jina la Yahwe.
à l’endroit où était l’autel qu’il avait précédemment élevé. Et là Abram invoqua le nom de Yahweh.
5 aliyekuwa anasafiri na Abram, alikuwa pia na ngo'mbe, makundi ya mifugo, na mahema.
Lot, qui voyageait avec Abram, avait aussi des brebis, des bœufs et des tentes,
6 Nchi haikuwatosha wote kukaa pamoja karibu kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana, kiasi kwamba hawakuweza kukaa pamoja.
et la contrée ne leur suffisait pas pour habiter ensemble; car leurs biens étaient trop considérables pour qu’ils pussent demeurer ensemble.
7 Pia, kulikuwa na ugomvi kati ya wachunga wanyama wa Abram na wachunga wanyama wa Lutu. Wakanaani pamoja na Waperizi walikuwa wakiishi katika nchi ile wakati huo.
Il y eut une querelle entre les bergers des troupeaux d’Abram et les bergers des troupeaux de Lot. — Les Chananéens et les Phérézéens étaient alors établis dans le pays. —
8 Kwa hiyo Abram akamwambia Lutu, “Pasiwe na ugomvi kati yako na mimi, na kati ya wachunga wanyama wako na wachunga wanyama wangu; licha ya hayo sisi ni familia.
Abram dit à Lot: « Qu’il n’y ait pas, je te prie, de débat entre moi et toi, ni entre mes bergers et tes bergers; car nous sommes des frères.
9 Je nchi hii yote haiko mbele yako? Nenda na ujitenge na mi. Ikiwa utakwenda kushoto, mimi nitakwenda kulia. au ikiwa utakwenda kulia, mimi nitakwenda kushoto.”
Tout le pays n’est-il pas devant toi? Sépare-toi donc de moi. Si tu vas à gauche, je prendrai la droite; et si tu vas à droite, je prendrai la gauche. »
10 Kwa hiyo Lutu akatazama, na akaona kuwa nchi yote tambarare ya Yorodani ilikuwa na maji kila mahali hadi Zoari, kama vile bustani ya Yahwe, na kama nchi ya Misri. Hii ilikuwa ni kabla Yahwe hajaiangamiza Sodoma na Gomora.
Lot, levant les yeux, vit toute la plaine du Jourdain qui était entièrement arrosée: c’était, avant que Yahweh eût détruit Sodome et Gomorrhe, comme le jardin de Yahweh, comme la terre d’Égypte du côté de Tsoar.
11 Kwa hiyo Lutu akajichagulia yeye mwenyewe nchi tambarare ya Yorodani na akasafiri mashariki, na ndugu hawa wakatengana wao kwa wao.
Lot choisit pour lui toute la plaine du Jourdain, et il s’avança vers l’orient; c’est ainsi qu’ils se séparèrent l’un de l’autre.
12 Abram akaishi katika nchi ya Kanaani, na Lutu akaishi katika miji ya tambarare. Akatandaza hema zake hadi Sodoma.
Abram habitait dans le pays de Chanaan, et Lot habitait dans les villes de la plaine, et il dressa ses tentes jusqu’à Sodome.
13 Na sasa watu wa Sodoma walikuwa waovu na wenye dhambi nyingi dhidi ya Yahwe.
Or les gens de Sodome étaient fort mauvais et grands pécheurs contre Yahweh.
14 Yahwe akamwambia Abram baada ya Lutu kuondoka kwake, “Angalia kuanzia mahali ulipo simama hadi kaskazini, kusini, mashariki, na magharibi.
Yahweh dit à Abram, après que Lot se fut séparé de lui: « Lève les yeux et, du lieu où tu es, regarde vers le septentrion et vers le midi, vers l’orient, et vers le couchant:
15 Nchi yote hii uionayo, nitakupatia wewe pamoja na uzao wako milele.
tout le pays que tu vois, je le donnerai à toi et à ta postérité pour toujours.
16 Nitawafanya uzao wako kuwa wengi kama mavumbi ya nchi, kiasi kwamba kama kuna mtu anaweza kuhesabu mavumbi ya nchi, ndipo na uzao wako pia utahesabika.
Je rendrai ta postérité nombreuse comme la poussière de la terre; si l’on peut compter la poussière de la terre, on comptera aussi ta postérité.
17 Inuka, tembea katika urefu na upana wa nchi hii, kwa kuwa nitakupatia.”
Lève-toi, parcours le pays en long et en large, car je te le donnerai. »
18 Kwa hiyo Abram akachukua hema yake, akaja na kukaa katika mwaloni wa Mamre, ambao uko Hebroni, na pale akajenga Madhabahu ya Yahwe.
Abram leva ses tentes et vint habiter aux chênes de Mambré, qui sont en Hébron; et il bâtit là un autel à Yahweh.