< Mwanzo 13 >

1 Kwa hiyo Abram akaondoka akatoka Misri na akaenda Negebu, Yeye, mke wake, na vyote alivyokuwa navyo. Lutu pia akaenda pamoja naye.
Than Abram departed out of Egipte both he and his wyfe and all that he had and Lot wyth hym vnto the south.
2 Na sasa Abram alikuwa tajiri wa mifugo, fedha na dhahabu.
Abram was very rych in catell syluer and gold.
3 Aliendelea na safari yake kutoka Negebu hadi Betheli, mahali ambapo hema yake ilikuwa tangu mwanzo, kati ya Betheli na mji wa Ai.
And he went on his iourney fro the south even vnto BETHEL ad vnto the place where his tente was at the fyrst tyme betwene BETHEL and Ay
4 Akaenda mahali ambapo madhabahu ilikuwa imejengwa mwanzoni. Hapa akaliitia jina la Yahwe.
and vnto the place of the aulter which he made before. And there called Abram vpon the name of the LORde.
5 aliyekuwa anasafiri na Abram, alikuwa pia na ngo'mbe, makundi ya mifugo, na mahema.
Lot also which went wyth hym had shepe catell and tentes:
6 Nchi haikuwatosha wote kukaa pamoja karibu kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana, kiasi kwamba hawakuweza kukaa pamoja.
so that the londe was not abill to receaue them that they myght dwell together for the substance of their riches was so greate that they coude not dwell together
7 Pia, kulikuwa na ugomvi kati ya wachunga wanyama wa Abram na wachunga wanyama wa Lutu. Wakanaani pamoja na Waperizi walikuwa wakiishi katika nchi ile wakati huo.
And there fell a stryfe betwene the herdmen of Abrams catell and the herdmen of Lots catell. Moreouer the Cananytes and the Pherysites dwelled at that tyme in the lande.
8 Kwa hiyo Abram akamwambia Lutu, “Pasiwe na ugomvi kati yako na mimi, na kati ya wachunga wanyama wako na wachunga wanyama wangu; licha ya hayo sisi ni familia.
Than sayd Abram vnto Lot: let there be no stryfe I praye the betwene the and me and betwene my herdmen and thyne for we be brethren.
9 Je nchi hii yote haiko mbele yako? Nenda na ujitenge na mi. Ikiwa utakwenda kushoto, mimi nitakwenda kulia. au ikiwa utakwenda kulia, mimi nitakwenda kushoto.”
Ys not all the hole lande before the? Departe I praye the fro me. Yf thou wylt take the lefte hande I wyll take the right: Or yf thou take the right hande I wyll take the left.
10 Kwa hiyo Lutu akatazama, na akaona kuwa nchi yote tambarare ya Yorodani ilikuwa na maji kila mahali hadi Zoari, kama vile bustani ya Yahwe, na kama nchi ya Misri. Hii ilikuwa ni kabla Yahwe hajaiangamiza Sodoma na Gomora.
And Lot lyft vp hys eyes and beheld all the contre aboute Iordane which was a plenteous contre of water every where before the LORde destroyed Sodoma and Gomorra. Even as the garden of the LORde and as the lande of Egipte tyll thou come to Zoar.
11 Kwa hiyo Lutu akajichagulia yeye mwenyewe nchi tambarare ya Yorodani na akasafiri mashariki, na ndugu hawa wakatengana wao kwa wao.
Than Lot chose all the costes of Iordane ad toke hys iourney from the east. And so departed the one brother from the other.
12 Abram akaishi katika nchi ya Kanaani, na Lutu akaishi katika miji ya tambarare. Akatandaza hema zake hadi Sodoma.
Abram dwelled in the lande of Canaan. And lot in the cytes of the playne and tented tyll he came to Sodome.
13 Na sasa watu wa Sodoma walikuwa waovu na wenye dhambi nyingi dhidi ya Yahwe.
But the men of sodome were wyked and synned exceadyngly agenst the LORde.
14 Yahwe akamwambia Abram baada ya Lutu kuondoka kwake, “Angalia kuanzia mahali ulipo simama hadi kaskazini, kusini, mashariki, na magharibi.
And the LORde sayed vnto Abram after that Lot was departed from hym: lyfte vp thyne eyes and loke from ye place where thou art northward southward eastward and westward
15 Nchi yote hii uionayo, nitakupatia wewe pamoja na uzao wako milele.
for all the lande which thou seiste wyll I gyue vnto the and to thy seed for ever.
16 Nitawafanya uzao wako kuwa wengi kama mavumbi ya nchi, kiasi kwamba kama kuna mtu anaweza kuhesabu mavumbi ya nchi, ndipo na uzao wako pia utahesabika.
And I wyll make thy seed as the dust of the erth: so that yf a ma can nombre the dust of the erth than shall thy seed also be nombred.
17 Inuka, tembea katika urefu na upana wa nchi hii, kwa kuwa nitakupatia.”
Aryse and walke aboute in the lande in the length of it ad in the bredth for I wyll geue it vnto the.
18 Kwa hiyo Abram akachukua hema yake, akaja na kukaa katika mwaloni wa Mamre, ambao uko Hebroni, na pale akajenga Madhabahu ya Yahwe.
Than Abra toke downe hys tente and went and dwelled in the okegrove of Mamre which is in Ebron and buylded there an altar to the LORde.

< Mwanzo 13 >