< Mwanzo 12 >
1 Kisha Yahwe akamwambia Abram, “Nenda utoke katika nchi yako, na toka kwa ndugu zako, na kwa jamaa za baba yako, uende katika nchi nitakayo kuonesha.
Yahvé dit à Abram: « Quitte ton pays, ta famille et la maison de ton père, et va dans le pays que je te montrerai.
2 Nitakufanya uwe taifa kubwa, na nitakubariki na kulifanya jinalako kuwa kubwa, na utafanyika baraka.
Je ferai de toi une grande nation. Je te bénirai et je rendrai ton nom grand. Tu seras une bénédiction.
3 Nitawabariki wakubarikio, lakini asiye kuheshimu nita mlaani. Kupitia kwako familia zote za nchi zitabarikiwa.
Je bénirai ceux qui te béniront, et je maudirai celui qui te traitera avec mépris. Toutes les familles de la terre seront bénies par toi. »
4 Kwa hiyo Abram akaondoka kama vile Yahwe alivyo mwambia kufanya, na Lutu akaenda pamoja naye. Abram alikuwa na miaka sabini na mitano wakati alipotoka Harani.
Et Abram partit, comme Yahvé le lui avait dit. Lot partit avec lui. Abram était âgé de soixante-quinze ans lorsqu'il partit de Haran.
5 Abram akamchukua Sarai mkewe, Lutu, mtoto wa ndugu yake, na vyote walivyomiliki ambavyo wamevikusanya, na watu ambao wamewapata wakiwa huko Harani. Wakatoka kwenda katika nchi ya Kanaani, wakafika nchi ya Kanaani.
Abram prit Saraï, sa femme, Lot, le fils de son frère, tous les biens qu'ils avaient rassemblés, et le peuple qu'ils avaient acquis à Haran, et ils partirent pour aller au pays de Canaan. Ils entrèrent dans le pays de Canaan.
6 Abram akapitia katikati ya nchi hadi Shekemu, hadi mwaloni wa More. Wakati huo wakanaani waliishi katika nchi hiyo.
Abram traversa le pays jusqu'au lieu-dit Sichem, au chêne de Moreh. En ce temps-là, les Cananéens étaient dans le pays.
7 Yahwe akamtokea Abram, na kusema, “Nitawapa uzao wako nchi hii.” Kwa hiyo Abram akamjengea madhabahu, Yahwe ambaye alimtokea.
Yahvé apparut à Abram et dit: « Je donnerai ce pays à ta descendance. » Il y bâtit un autel à Yahvé, qui lui était apparu.
8 Kutoka pale akaenda kwenye nchi ya mlima mashariki mwa Betheli, ambapo alipiga hema yake, magaribi kukiwa na Betheli na mashariki kukiwa na mji wa Ai. Akajenga madhabahu ya Yahwe pale na kuliitia jina la Yahwe.
Il partit de là pour aller sur la montagne à l'est de Béthel et planta sa tente, ayant Béthel à l'ouest et Aï à l'est. Là, il bâtit un autel à Yahvé et invoqua le nom de Yahvé.
9 Kisha Abram akaendelea kusafiri, akielekea upande wa Negebu.
Abram voyagea, toujours en direction du sud.
10 Kulikuwa na njaa katika nchi, kwa hiyo Abram akaenda kukaa Misri, kwa kuwa njaa ilikua kali katika nchi.
Il y eut une famine dans le pays. Abram descendit en Égypte pour y vivre comme un étranger, car la famine sévissait dans le pays.
11 Wakati alipokaribia kuingia Misri, akamwambia Sarai mkewe, “tazama, najua kuwa wewe ni mwanamke mzuri.
Lorsqu'il fut sur le point d'entrer en Égypte, il dit à Saraï, sa femme: « Voici, je sais que tu es une femme belle à regarder.
12 Wamisri watakapokuona watasema, huyu ni mke wake, na wataniua mimi, lakini watakuacha wewe hai.
Quand les Égyptiens te verront, ils diront: « C'est sa femme ». Ils me tueront, mais ils te laisseront la vie sauve.
13 Hivyo wewe sema kuwa ni dada yangu, ili kwamba niwe salama kwa sababu yako, na kumba maisha yangu yatasalimika kwa sababu yako.”
Dis, je t'en prie, que tu es ma sœur, afin que je sois heureux à cause de toi et que mon âme vive grâce à toi. »
14 Ikawa kwamba Abram alipoingia Misri, Wamisri wakaona kwamba Sarai ni mzuri sana.
Quand Abram fut arrivé en Égypte, les Égyptiens virent que la femme était très belle.
15 Wakuu wa Farao wakamuona, na kumsifia kwa Farao, na huyu mwanamke akachukuliwa kupelekwa nyumbani mwa Farao.
Les princes de Pharaon la virent et la louèrent à Pharaon; et la femme fut emmenée dans la maison de Pharaon.
16 Farao akamtendea kwa wema Abram kwa ajili yake, na akampatia kondoo, maksai, punda waume watumishi wa kiume, watumishi wa kike, punda wake, na ngamia.
Il traita bien Abram à cause d'elle. Il eut des moutons, du bétail, des ânes mâles, des serviteurs mâles, des servantes, des ânesses et des chameaux.
17 Kisha Yahwe akampiga Farao na nyumba yake kwa mapigo makuu kwa sababau ya Sarai, mke wa Abram.
Yahvé affligea Pharaon et sa maison de grandes plaies à cause de Saraï, la femme d'Abram.
18 Farao akamwita Abram na kusema, “Nini hiki ambacho umenifanyia? Kwa nini hukuniambia kuwa alikuwa mke wako?
Pharaon appela Abram et dit: « Qu'est-ce que tu m'as fait? Pourquoi ne m'as-tu pas dit qu'elle était ta femme?
19 Kwa nini ulisema, 'ni dada yangu; na mimi nikamchukua kuwa mke wangu? Sasa kwa sababu hiyo huyu hapa mke wako. Mchukue na uende zako.”
Pourquoi as-tu dit: « C'est ma sœur », pour que je la prenne pour femme? Maintenant donc, va voir ta femme, prends-la, et va-t'en. »
20 Kisha Farao akatoa amri kwa watu wake kuhusiana naye, na wakamuondoa, yeye pamoja na mke wake na vyote alivyokuwa navyo.
Pharaon donna des ordres aux hommes à son sujet, et ils l'emmenèrent avec sa femme et tout ce qui lui appartenait.