< Mwanzo 12 >

1 Kisha Yahwe akamwambia Abram, “Nenda utoke katika nchi yako, na toka kwa ndugu zako, na kwa jamaa za baba yako, uende katika nchi nitakayo kuonesha.
And YHWH says to Abram, “Go for yourself, from your land, and from your family, and from the house of your father, to the land which I show you.
2 Nitakufanya uwe taifa kubwa, na nitakubariki na kulifanya jinalako kuwa kubwa, na utafanyika baraka.
And I make you become a great nation, and bless you, and make your name great; and be a blessing.
3 Nitawabariki wakubarikio, lakini asiye kuheshimu nita mlaani. Kupitia kwako familia zote za nchi zitabarikiwa.
And I bless those blessing you, and I curse him who is cursing you, and all families of the ground have been blessed in you.”
4 Kwa hiyo Abram akaondoka kama vile Yahwe alivyo mwambia kufanya, na Lutu akaenda pamoja naye. Abram alikuwa na miaka sabini na mitano wakati alipotoka Harani.
And Abram goes on, as YHWH has spoken to him, and Lot goes with him, and Abram [is] a son of seventy-five years in his going out from Haran.
5 Abram akamchukua Sarai mkewe, Lutu, mtoto wa ndugu yake, na vyote walivyomiliki ambavyo wamevikusanya, na watu ambao wamewapata wakiwa huko Harani. Wakatoka kwenda katika nchi ya Kanaani, wakafika nchi ya Kanaani.
And Abram takes his wife Sarai, and his brother’s son Lot, and all their substance that they have gained, and the persons that they have obtained in Haran; and they go out to go toward the land of Canaan; and they come to the land of Canaan.
6 Abram akapitia katikati ya nchi hadi Shekemu, hadi mwaloni wa More. Wakati huo wakanaani waliishi katika nchi hiyo.
And Abram passes over into the land, to the place of Shechem, to the oak of Moreh; and the Canaanite [is] then in the land.
7 Yahwe akamtokea Abram, na kusema, “Nitawapa uzao wako nchi hii.” Kwa hiyo Abram akamjengea madhabahu, Yahwe ambaye alimtokea.
And YHWH appears to Abram and says, “To your seed I give this land”; and there he builds an altar to YHWH, who has appeared to him.
8 Kutoka pale akaenda kwenye nchi ya mlima mashariki mwa Betheli, ambapo alipiga hema yake, magaribi kukiwa na Betheli na mashariki kukiwa na mji wa Ai. Akajenga madhabahu ya Yahwe pale na kuliitia jina la Yahwe.
And he removes from there toward a mountain at the east of Beth-El, and stretches out the tent (Beth-El at the west, and Hai at the east), and he builds an altar to YHWH there, and preaches in the Name of YHWH.
9 Kisha Abram akaendelea kusafiri, akielekea upande wa Negebu.
And Abram journeys, going on and journeying toward the south.
10 Kulikuwa na njaa katika nchi, kwa hiyo Abram akaenda kukaa Misri, kwa kuwa njaa ilikua kali katika nchi.
And there is a famine in the land, and Abram goes down toward Egypt to sojourn there, for the famine [is] grievous in the land;
11 Wakati alipokaribia kuingia Misri, akamwambia Sarai mkewe, “tazama, najua kuwa wewe ni mwanamke mzuri.
and it comes to pass as he has drawn near to enter Egypt, that he says to his wife Sarai, “Now behold, I have known that you [are] a woman of beautiful appearance;
12 Wamisri watakapokuona watasema, huyu ni mke wake, na wataniua mimi, lakini watakuacha wewe hai.
and it has come to pass that the Egyptians see you, and they have said, This [is] his wife; and they have slain me, and you they keep alive:
13 Hivyo wewe sema kuwa ni dada yangu, ili kwamba niwe salama kwa sababu yako, na kumba maisha yangu yatasalimika kwa sababu yako.”
please say you [are] my sister, so that it is well with me because of you, and my soul has lived for your sake.”
14 Ikawa kwamba Abram alipoingia Misri, Wamisri wakaona kwamba Sarai ni mzuri sana.
And it comes to pass, at the entering of Abram into Egypt, that the Egyptians see the woman that she [is] exceedingly beautiful;
15 Wakuu wa Farao wakamuona, na kumsifia kwa Farao, na huyu mwanamke akachukuliwa kupelekwa nyumbani mwa Farao.
and princes of Pharaoh see her, and praise her to Pharaoh, and the woman is taken [to] Pharaoh’s house;
16 Farao akamtendea kwa wema Abram kwa ajili yake, na akampatia kondoo, maksai, punda waume watumishi wa kiume, watumishi wa kike, punda wake, na ngamia.
and to Abram he has done good because of her, and he has sheep and oxen, and male donkeys, and menservants, and handmaids, and female donkeys, and camels.
17 Kisha Yahwe akampiga Farao na nyumba yake kwa mapigo makuu kwa sababau ya Sarai, mke wa Abram.
And YHWH plagues Pharaoh and his house—great plagues—for the matter of Sarai, Abram’s wife.
18 Farao akamwita Abram na kusema, “Nini hiki ambacho umenifanyia? Kwa nini hukuniambia kuwa alikuwa mke wako?
And Pharaoh calls for Abram and says, “What [is] this you have done to me? Why have you not declared to me that she [is] your wife?
19 Kwa nini ulisema, 'ni dada yangu; na mimi nikamchukua kuwa mke wangu? Sasa kwa sababu hiyo huyu hapa mke wako. Mchukue na uende zako.”
Why have you said, She [is] my sister, and I take her to myself for a wife? And now, behold, your wife, take and go.”
20 Kisha Farao akatoa amri kwa watu wake kuhusiana naye, na wakamuondoa, yeye pamoja na mke wake na vyote alivyokuwa navyo.
And Pharaoh charges men concerning him, and they send him away, and his wife, and all that he has.

< Mwanzo 12 >