< Mwanzo 12 >
1 Kisha Yahwe akamwambia Abram, “Nenda utoke katika nchi yako, na toka kwa ndugu zako, na kwa jamaa za baba yako, uende katika nchi nitakayo kuonesha.
Jahve reče Abramu: “Idi iz zemlje svoje, iz zavičaja i doma očinskog, u krajeve koje ću ti pokazati.
2 Nitakufanya uwe taifa kubwa, na nitakubariki na kulifanya jinalako kuwa kubwa, na utafanyika baraka.
Velik ću narod od tebe učiniti, blagoslovit ću te, ime ću ti uzveličati, i sam ćeš biti blagoslov.
3 Nitawabariki wakubarikio, lakini asiye kuheshimu nita mlaani. Kupitia kwako familia zote za nchi zitabarikiwa.
Blagoslivljat ću one koji te blagoslivljali budu, koji te budu kleli, njih ću proklinjati; sva plemena na zemlji tobom će se blagoslivljati.”
4 Kwa hiyo Abram akaondoka kama vile Yahwe alivyo mwambia kufanya, na Lutu akaenda pamoja naye. Abram alikuwa na miaka sabini na mitano wakati alipotoka Harani.
Abram se zaputi kako mu je Jahve rekao. S njime krenu i Lot. Abramu je bilo sedamdeset i pet godina kad je otišao iz Harana.
5 Abram akamchukua Sarai mkewe, Lutu, mtoto wa ndugu yake, na vyote walivyomiliki ambavyo wamevikusanya, na watu ambao wamewapata wakiwa huko Harani. Wakatoka kwenda katika nchi ya Kanaani, wakafika nchi ya Kanaani.
Abram uze sa sobom svoju ženu Saraju, svoga bratića Lota, svu imovinu što su je namakli i svu čeljad koju su stekli u Haranu te svi pođu u zemlju kanaansku. Kad su stigli u Kanaan,
6 Abram akapitia katikati ya nchi hadi Shekemu, hadi mwaloni wa More. Wakati huo wakanaani waliishi katika nchi hiyo.
Abram prođe zemljom do mjesta Šekema - do hrasta More. Kanaanci su onda bili u zemlji.
7 Yahwe akamtokea Abram, na kusema, “Nitawapa uzao wako nchi hii.” Kwa hiyo Abram akamjengea madhabahu, Yahwe ambaye alimtokea.
Jahve se javi Abramu pa mu reče: “Tvome ću potomstvu dati ovu zemlju.” Abram tu podigne žrtvenik Jahvi koji mu se objavio.
8 Kutoka pale akaenda kwenye nchi ya mlima mashariki mwa Betheli, ambapo alipiga hema yake, magaribi kukiwa na Betheli na mashariki kukiwa na mji wa Ai. Akajenga madhabahu ya Yahwe pale na kuliitia jina la Yahwe.
Odatle prijeđe u brdoviti kraj, na istok od Betela. Svoj šator postavi između Betela na zapadu i Aja na istoku. Ondje podigne žrtvenik Jahvi i zazva ime Jahvino.
9 Kisha Abram akaendelea kusafiri, akielekea upande wa Negebu.
Od postaje do postaje Abram se pomicao prema Negebu.
10 Kulikuwa na njaa katika nchi, kwa hiyo Abram akaenda kukaa Misri, kwa kuwa njaa ilikua kali katika nchi.
Ali kad je zemljom zavladala glad, Abram se spusti u Egipat da ondje proboravi, jer je velika glad harala zemljom.
11 Wakati alipokaribia kuingia Misri, akamwambia Sarai mkewe, “tazama, najua kuwa wewe ni mwanamke mzuri.
Kad je bio na ulazu u Egipat, reče svojoj ženi Saraji: “Znam da si lijepa žena.
12 Wamisri watakapokuona watasema, huyu ni mke wake, na wataniua mimi, lakini watakuacha wewe hai.
Kad te Egipćani vide, reći će: 'To je njegova žena', i mene će ubiti, a tebe na životu ostaviti.
13 Hivyo wewe sema kuwa ni dada yangu, ili kwamba niwe salama kwa sababu yako, na kumba maisha yangu yatasalimika kwa sababu yako.”
Nego reci da si mi sestra, tako da i meni bude zbog tebe dobro i da, iz obzira prema tebi, poštede moj život.”
14 Ikawa kwamba Abram alipoingia Misri, Wamisri wakaona kwamba Sarai ni mzuri sana.
Zbilja, kad je Abram ušao u Egipat, Egipćani vide da je žena veoma lijepa.
15 Wakuu wa Farao wakamuona, na kumsifia kwa Farao, na huyu mwanamke akachukuliwa kupelekwa nyumbani mwa Farao.
Vide je faraonovi dvorani pa je pohvale faraonu i odvedu ženu na faraonov dvor.
16 Farao akamtendea kwa wema Abram kwa ajili yake, na akampatia kondoo, maksai, punda waume watumishi wa kiume, watumishi wa kike, punda wake, na ngamia.
Abramu pođe dobro zbog nje; steče on stoke i goveda, magaraca, slugu i sluškinja, magarica i deva.
17 Kisha Yahwe akampiga Farao na nyumba yake kwa mapigo makuu kwa sababau ya Sarai, mke wa Abram.
Ali Jahve udari faraona i njegov dom velikim nevoljama zbog Abramove žene Saraje.
18 Farao akamwita Abram na kusema, “Nini hiki ambacho umenifanyia? Kwa nini hukuniambia kuwa alikuwa mke wako?
I faraon pozva Abrama pa reče: “Što si mi to učinio? Zašto mi nisi kazao da je ona tvoja žena?
19 Kwa nini ulisema, 'ni dada yangu; na mimi nikamchukua kuwa mke wangu? Sasa kwa sababu hiyo huyu hapa mke wako. Mchukue na uende zako.”
Zašto si rekao: 'Ona mi je sestra', pa je ja uzeh sebi za ženu? A sad, evo ti žene; uzmi je i hajde!”
20 Kisha Farao akatoa amri kwa watu wake kuhusiana naye, na wakamuondoa, yeye pamoja na mke wake na vyote alivyokuwa navyo.
Faraon ga onda preda momcima, a oni ga otprave s njegovom ženom i sa svime što bijaše njegovo.