< Mwanzo 11 >
1 Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
erat autem terra labii unius et sermonum eorundem
2 Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
cumque proficiscerentur de oriente invenerunt campum in terra Sennaar et habitaverunt in eo
3 Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
dixitque alter ad proximum suum venite faciamus lateres et coquamus eos igni habueruntque lateres pro saxis et bitumen pro cemento
4 Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
et dixerunt venite faciamus nobis civitatem et turrem cuius culmen pertingat ad caelum et celebremus nomen nostrum antequam dividamur in universas terras
5 Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
descendit autem Dominus ut videret civitatem et turrem quam aedificabant filii Adam
6 Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
et dixit ecce unus est populus et unum labium omnibus coeperuntque hoc facere nec desistent a cogitationibus suis donec eas opere conpleant
7 Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
venite igitur descendamus et confundamus ibi linguam eorum ut non audiat unusquisque vocem proximi sui
8 Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
atque ita divisit eos Dominus ex illo loco in universas terras et cessaverunt aedificare civitatem
9 Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
et idcirco vocatum est nomen eius Babel quia ibi confusum est labium universae terrae et inde dispersit eos Dominus super faciem cunctarum regionum
10 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
hae generationes Sem Sem centum erat annorum quando genuit Arfaxad biennio post diluvium
11 Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
vixitque Sem postquam genuit Arfaxad quingentos annos et genuit filios et filias
12 Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
porro Arfaxad vixit triginta quinque annos et genuit Sale
13 Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
vixitque Arfaxad postquam genuit Sale trecentis tribus annis et genuit filios et filias
14 Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
Sale quoque vixit triginta annis et genuit Eber
15 Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
vixitque Sale postquam genuit Eber quadringentis tribus annis et genuit filios et filias
16 Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
vixit autem Eber triginta quattuor annis et genuit Faleg
17 Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
et vixit Eber postquam genuit Faleg quadringentis triginta annis et genuit filios et filias
18 Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
vixit quoque Faleg triginta annis et genuit Reu
19 Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
vixitque Faleg postquam genuit Reu ducentis novem annis et genuit filios et filias
20 Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
vixit autem Reu triginta duobus annis et genuit Sarug
21 Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
vixitque Reu postquam genuit Sarug ducentis septem annis et genuit filios et filias
22 Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
vixit vero Sarug triginta annis et genuit Nahor
23 Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
vixitque Sarug postquam genuit Nahor ducentos annos et genuit filios et filias
24 Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
vixit autem Nahor viginti novem annis et genuit Thare
25 Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
vixitque Nahor postquam genuit Thare centum decem et novem annos et genuit filios et filias
26 Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
vixitque Thare septuaginta annis et genuit Abram et Nahor et Aran
27 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
hae sunt autem generationes Thare Thare genuit Abram et Nahor et Aran porro Aran genuit Loth
28 Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
mortuusque est Aran ante Thare patrem suum in terra nativitatis suae in Ur Chaldeorum
29 Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
duxerunt autem Abram et Nahor uxores nomen autem uxoris Abram Sarai et nomen uxoris Nahor Melcha filia Aran patris Melchae et patris Ieschae
30 Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
erat autem Sarai sterilis nec habebat liberos
31 Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
tulit itaque Thare Abram filium suum et Loth filium Aran filium filii sui et Sarai nurum suam uxorem Abram filii sui et eduxit eos de Ur Chaldeorum ut irent in terram Chanaan veneruntque usque Haran et habitaverunt ibi
32 Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.
et facti sunt dies Thare ducentorum quinque annorum et mortuus est in Haran