< Mwanzo 11 >

1 Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
Toute la terre avait une seule langue et les mêmes mots.
2 Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
Comme ils étaient partis de l’orient, ils trouvèrent une plaine au pays de Schinear, et ils y habitèrent.
3 Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
Ils se dirent l’un à l’autre: Allons! Faisons des briques, et cuisons-les au feu. Et la brique leur servit de pierre, et le bitume leur servit de ciment.
4 Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
Ils dirent encore: Allons! Bâtissons-nous une ville et une tour dont le sommet touche au ciel, et faisons-nous un nom, afin que nous ne soyons pas dispersés sur la face de toute la terre.
5 Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
L’Éternel descendit pour voir la ville et la tour que bâtissaient les fils des hommes.
6 Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
Et l’Éternel dit: Voici, ils forment un seul peuple et ont tous une même langue, et c’est là ce qu’ils ont entrepris; maintenant rien ne les empêcherait de faire tout ce qu’ils auraient projeté.
7 Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
Allons! Descendons, et là confondons leur langage, afin qu’ils n’entendent plus la langue, les uns des autres.
8 Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
Et l’Éternel les dispersa loin de là sur la face de toute la terre; et ils cessèrent de bâtir la ville.
9 Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
C’est pourquoi on l’appela du nom de Babel, car c’est là que l’Éternel confondit le langage de toute la terre, et c’est de là que l’Éternel les dispersa sur la face de toute la terre.
10 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
Voici la postérité de Sem. Sem, âgé de cent ans, engendra Arpacschad, deux ans après le déluge.
11 Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
Sem vécut, après la naissance d’Arpacschad, cinq cents ans; et il engendra des fils et des filles.
12 Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
Arpacschad, âgé de trente-cinq ans, engendra Schélach.
13 Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Arpacschad vécut, après la naissance de Schélach, quatre cent trois ans; et il engendra des fils et des filles.
14 Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
Schélach, âgé de trente ans, engendra Héber.
15 Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Schélach vécut, après la naissance d’Héber, quatre cent trois ans; et il engendra des fils et des filles.
16 Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
Héber, âgé de trente-quatre ans, engendra Péleg.
17 Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Héber vécut, après la naissance de Péleg, quatre cent trente ans; et il engendra des fils et des filles.
18 Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
Péleg, âgé de trente ans, engendra Rehu.
19 Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Péleg vécut, après la naissance de Rehu, deux cent neuf ans; et il engendra des fils et des filles.
20 Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
Rehu, âgé de trente-deux ans, engendra Serug.
21 Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Rehu vécut, après la naissance de Serug, deux cent sept ans; et il engendra des fils et des filles.
22 Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
Serug, âgé de trente ans, engendra Nachor.
23 Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Serug vécut, après la naissance de Nachor, deux cents ans; et il engendra des fils et des filles.
24 Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
Nachor, âgé de vingt-neuf ans, engendra Térach.
25 Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Nachor vécut, après la naissance de Térach, cent dix-neuf ans; et il engendra des fils et des filles.
26 Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
Térach, âgé de soixante-dix ans, engendra Abram, Nachor et Haran.
27 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
Voici la postérité de Térach. Térach engendra Abram, Nachor et Haran. Haran engendra Lot.
28 Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
Et Haran mourut en présence de Térach, son père, au pays de sa naissance, à Ur en Chaldée.
29 Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
Abram et Nachor prirent des femmes: le nom de la femme d’Abram était Saraï, et le nom de la femme de Nachor était Milca, fille d’Haran, père de Milca et père de Jisca.
30 Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
Saraï était stérile: elle n’avait point d’enfants.
31 Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
Térach prit Abram, son fils, et Lot, fils d’Haran, fils de son fils, et Saraï, sa belle-fille, femme d’Abram, son fils. Ils sortirent ensemble d’Ur en Chaldée, pour aller au pays de Canaan. Ils vinrent jusqu’à Charan, et ils y habitèrent.
32 Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.
Les jours de Térach furent de deux cent cinq ans; et Térach mourut à Charan.

< Mwanzo 11 >