< Mwanzo 11 >

1 Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
Et toute la terre avait une seule langue et les mêmes paroles.
2 Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
Et il arriva que lorsqu’ils partirent de l’orient, ils trouvèrent une plaine dans le pays de Shinhar; et ils y habitèrent.
3 Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
Et ils se dirent l’un à l’autre: Allons, faisons des briques, et cuisons-les au feu. Et ils avaient la brique pour pierre, et ils avaient le bitume pour mortier.
4 Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
Et ils dirent: Allons, bâtissons-nous une ville, et une tour dont le sommet [atteigne] jusqu’aux cieux; et faisons-nous un nom, de peur que nous ne soyons dispersés sur la face de toute la terre.
5 Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
Et l’Éternel descendit pour voir la ville et la tour que bâtissaient les fils des hommes.
6 Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
Et l’Éternel dit: Voici, c’est un seul peuple, et ils n’ont, eux tous, qu’un seul langage, et ils ont commencé à faire ceci; et maintenant ils ne seront empêchés en rien de ce qu’ils pensent faire.
7 Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
Allons, descendons, et confondons là leur langage, afin qu’ils n’entendent pas le langage l’un de l’autre.
8 Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
Et l’Éternel les dispersa de là sur la face de toute la terre; et ils cessèrent de bâtir la ville.
9 Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
C’est pourquoi on appela son nom Babel, car là l’Éternel confondit le langage de toute la terre; et de là l’Éternel les dispersa sur la face de toute la terre.
10 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
Ce sont ici les générations de Sem: Sem était âgé de 100 ans, et il engendra Arpacshad, deux ans après le déluge.
11 Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
Et Sem, après qu’il eut engendré Arpacshad, vécut 500 ans; et il engendra des fils et des filles.
12 Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
Et Arpacshad vécut 35 ans, et engendra Shélakh.
13 Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Et Arpacshad, après qu’il eut engendré Shélakh, vécut 403 ans; et il engendra des fils et des filles.
14 Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
Et Shélakh vécut 30 ans, et engendra Héber.
15 Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Et Shélakh, après qu’il eut engendré Héber, vécut 403 ans; et il engendra des fils et des filles.
16 Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
Et Héber vécut 34 ans, et engendra Péleg.
17 Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Et Héber, après qu’il eut engendré Péleg, vécut 430 ans; et il engendra des fils et des filles.
18 Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
Et Péleg vécut 30 ans, et engendra Rehu.
19 Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Et Péleg, après qu’il eut engendré Rehu, vécut 209 ans; et il engendra des fils et des filles.
20 Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
Et Rehu vécut 32 ans, et engendra Serug.
21 Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Et Rehu, après qu’il eut engendré Serug, vécut 207 ans; et il engendra des fils et des filles.
22 Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
Et Serug vécut 30 ans, et engendra Nakhor.
23 Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Et Serug, après qu’il eut engendré Nakhor, vécut 200 ans; et il engendra des fils et des filles.
24 Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
Et Nakhor vécut 29 ans, et engendra Térakh.
25 Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Et Nakhor, après qu’il eut engendré Térakh, vécut 119 ans; et il engendra des fils et des filles.
26 Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
Et Térakh vécut 70 ans, et engendra Abram, Nakhor, et Haran.
27 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
Et ce sont ici les générations de Térakh: Térakh engendra Abram, Nakhor, et Haran. Et Haran engendra Lot.
28 Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
Et Haran mourut en la présence de Térakh, son père, au pays de sa naissance, à Ur des Chaldéens.
29 Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
– Et Abram et Nakhor prirent des femmes: le nom de la femme d’Abram était Saraï, et le nom de la femme de Nakhor, Milca, fille de Haran, père de Milca et père de Jisca.
30 Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
Et Saraï était stérile, elle n’avait pas d’enfants.
31 Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
Et Térakh prit Abram son fils, et Lot, fils de Haran, fils de son fils, et Saraï, sa belle-fille, femme d’Abram, son fils; et ils sortirent ensemble d’Ur des Chaldéens pour aller au pays de Canaan; et ils vinrent jusqu’à Charan, et habitèrent là.
32 Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.
Et les jours de Térakh furent 205 ans; et Térakh mourut à Charan.

< Mwanzo 11 >