< Mwanzo 11 >

1 Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
Now the whole earth used one language and had the same words.
2 Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
As they journeyed in the east, they found a plain in the land of Shinar and they settled there.
3 Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
They said to one another, “Come, let us make bricks and bake them thoroughly.” They had brick instead of stone and tar as mortar.
4 Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
They said, “Come, let us build ourselves a city and a tower whose top will reach to the sky, and let us make a name for ourselves. If we do not, we will be scattered across the surface of the whole earth.”
5 Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
So Yahweh came down to see the city and the tower which the descendants of Adam had built.
6 Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
Yahweh said, “Look, they are one people with the same language, and they are beginning to do this! Soon nothing that they intend to do will be impossible for them.
7 Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
Come, let us go down and confuse their language there, so that they may not understand each other.”
8 Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
So Yahweh scattered them from there across the surface of all the earth and they stopped building the city.
9 Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
Therefore, its name was called Babel, because there Yahweh confused the language of the whole earth and from there Yahweh scattered them abroad over the surface of all the earth.
10 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
These were the descendants of Shem. Shem was a hundred years old, and he became the father of Arphaxad two years after the flood.
11 Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
Shem lived five hundred years after he became the father of Arphaxad. He also became the father of other sons and daughters.
12 Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
When Arphaxad had lived thirty-five years, he became the father of Shelah.
13 Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Arphaxad lived 403 years after he became the father of Shelah. He also became the father of other sons and daughters.
14 Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
When Shelah had lived thirty years, he became the father of Eber.
15 Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Shelah lived 403 years after he became the father of Eber. He also became the father of other sons and daughters.
16 Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
When Eber had lived thirty-four years, he became the father of Peleg.
17 Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Eber lived 430 years after he became the father of Peleg. He also became the father of other sons and daughters.
18 Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
When Peleg had lived thirty years, he became the father of Reu.
19 Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Peleg lived 209 years after he became the father of Reu. He also became the father of other sons and daughters.
20 Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
When Reu had lived thirty-two years, he became the father of Serug.
21 Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Reu lived 207 years after he became the father of Serug. He also became the father of other sons and daughters.
22 Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
When Serug had lived thirty years, he became the father of Nahor.
23 Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Serug lived two hundred years after he became the father of Nahor. He also became the father of other sons and daughters.
24 Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
When Nahor had live twenty-nine years, he became the father of Terah.
25 Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Nahor lived 119 years after he became the father of Terah. He also became the father of other sons and daughters.
26 Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
After Terah had lived seventy years, he became the father of Abram, Nahor, and Haran.
27 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
Now these were the descendants of Terah. Terah became the father of Abram, Nahor, and Haran, and Haran became the father of Lot.
28 Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
Haran died in the presence of his father Terah in the land of his birth, in Ur of the Chaldeans.
29 Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
Abram and Nahor took wives. The name of Abram's wife was Sarai and the name of Nahor's wife was Milkah, a daughter of Haran, who was the father of Milkah and Iskah.
30 Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
Now Sarai was barren; she had no child.
31 Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
Terah took Abram his son, Lot the son of his son Haran, and Sarai his daughter-in-law, his son Abram's wife, and together they left Ur of the Chaldeans, to go into the land of Canaan. But they came to Haran and stayed there.
32 Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.
Terah lived 205 years and then died in Haran.

< Mwanzo 11 >