< Mwanzo 11 >
1 Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
And all the world was of one tonge and one language.
2 Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
And as they came from the east they founde a playne in the lande of Synear and there they dwelled.
3 Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
And they sayd one to a nother: come on let us make brycke ad burne it wyth fyre. So brycke was there stone and slyme was there morter
4 Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
And they sayd: Come on let vs buylde vs a cyte and a toure that the toppe may reach vnto heauen. And let vs make us a name for perauenture we shall be scatered abrode over all the erth.
5 Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
And the LORde came downe to see the cyte and the toure which the childern of Ada had buylded.
6 Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
And the LORde sayd: See the people is one and haue one tonge amonge them all. And thys haue they begon to do and wyll not leaue of from all that they haue purposed to do.
7 Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
Come on let vs descende and myngell theire tonge even there that one vnderstonde not what a nother sayeth.
8 Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
Thus ye LORde skatered them from thence vppon all the erth. And they left of to buylde the cyte.
9 Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
Wherfore the name of it is called Babell because that the LORDE there confounded the tonge of all the world. And because that the LORde from thence skatered them abrode vppon all the erth.
10 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
These are the generations of Sem: Se was an hundred yere olde and begat Arcphachsad ij. yere after the floude.
11 Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
And Se lyved after he had begot Arphachsad. v. hundred yere an begat sonnes and doughters.
12 Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
And Arphacsad lyued. xxxv. yere and begat Sala
13 Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
and lyved after he had begot Sala iiij. hudred yere and. iij and begat sonnes and doughters.
14 Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
And Sala was. xxx. yere old and begat Eber
15 Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
ad lyued after he had begot Eber. iiij. hudred and thre yere ad begat sonnes and doughters
16 Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
When Eber was. xxxiiij. yere olde he begat Peleg
17 Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
and lyued after he had begot Peleg foure hundred and. xxx. yere and begat sonnes and doughters.
18 Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
And Peleg when he was. xxx. yere olde begat Regu
19 Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
and lyued after he had begot Regu. ij. hundred and. ix. yere and begat sonnes and doughters.
20 Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
And Regu when he had lyued. xxxij. yere begat Serug
21 Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
and lyued after he had begot Serug. ij. hundred and. vij. yere and begat sonnes and doughters.
22 Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
And when Serug was. xxx. yere olde he begat Nahor
23 Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
and lyued after he had begot Nahor. ij. hundred yere and begat sonnes and doughters.
24 Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
And Nahor when he was. xxix. yere olde begat Terah
25 Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
and lyved after he had begot Terah an hundred and. xix. yere and begat sonnes and doughters.
26 Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
And when Terah was. lxx. yere olde he begat Abram Nahor and Haran.
27 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
And these are the generations of Terah. Terah begat Abram Nahor and Haran. And Haran begat Lot.
28 Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
And Haran dyed before Terah his father in the londe where he was borne at Vr in Chaldea.
29 Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
And Abram and Nahor toke them wyves. Abras wyfe was called Sarai. And Nahors wyfe Mylca the doughter of Haran which was father of Milca ad of Iisca.
30 Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
But Sarai was baren and had no childe.
31 Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
Than toke Terah Abram his sonne and Lot his sonne Harans sonne and Sarai his doughter in lawe his sone Abrams wyfe. And they went wyth hym from Vr in Chaldea to go in to the lade of Chanaan. And they came to Haran and dwelled there.
32 Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.
And when Terah was ij. hundred yere old and. v. he dyed in Haran.