< Mwanzo 11 >
1 Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
And it was all the earth language one and words one.
2 Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
And it was when set out they from [the] east and they found a plain in [the] land of Shinar and they dwelt there.
3 Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
And they said each to neighbor his give! let us make bricks bricks and let us burn [them] to burning and became for them brick to stone and bitumen became for them to mortar.
4 Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
And they said give! - let us build for ourselves a city and a tower and top its [will be] in the heavens and we may make for ourselves a name lest we should be scattered over [the] surface of all the earth.
5 Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
And he came down Yahweh to see the city and the tower which they had built [the] children of humankind.
6 Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
And he said Yahweh here! a people one and a language one [belongs] to all of them and this [is] beginning they to do and now not it will be withheld from them all that they will plan to do.
7 Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
Give! let us go down and let us confuse there language their that not they will hear each [the] language of neighbor his.
8 Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
And he scattered Yahweh them from there over [the] surface of all the earth and they ceased to build the city.
9 Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
There-fore someone called name its Babel for there he confused Yahweh [the] language of all the earth and from there he scattered them Yahweh over [the] surface of all the earth.
10 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
These [are] [the] accounts of Shem Shem [was] a son of one hundred year[s] and he fathered Arphaxad two years after the flood.
11 Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
And he lived Shem after fathered he Arphaxad five hundred year[s] and he fathered sons and daughters.
12 Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
And Arphaxad he lived five and thirty year[s] and he fathered Shelah.
13 Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
And he lived Arphaxad after fathered he Shelah three years and four hundred year[s] and he fathered sons and daughters.
14 Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
And Shelah he lived thirty year[s] and he fathered Eber.
15 Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
And he lived Shelah after fathered he Eber three years and four hundred year[s] and he fathered sons and daughters.
16 Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
And he lived Eber four and thirty year[s] and he fathered Peleg.
17 Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
And he lived Eber after fathered he Peleg thirty year[s] and four hundred year[s] and he fathered sons and daughters.
18 Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
And he lived Peleg thirty year[s] and he fathered Reu.
19 Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
And he lived Peleg after fathered he Reu nine years and two hundred year[s] and he fathered sons and daughters.
20 Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
And he lived Reu two and thirty year[s] and he fathered Serug.
21 Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
And he lived Reu after fathered he Serug seven years and two hundred year[s] and he fathered sons and daughters.
22 Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
And he lived Serug thirty year[s] and he fathered Nahor.
23 Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
And he lived Serug after fathered he Nahor two hundred year[s] and he fathered sons and daughters.
24 Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
And he lived Nahor nine and twenty year[s] and he fathered Terah.
25 Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
And he lived Nahor after fathered he Terah nine-teen year[s] and one hundred year[s] and he fathered sons and daughters.
26 Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
And he lived Terah seventy year[s] and he fathered Abram Nahor and Haran.
27 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
And these [are] [the] accounts of Terah Terah he fathered Abram Nahor and Haran and Haran he fathered Lot.
28 Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
And he died Haran on [the] face of Terah father his in [the] land of kindred his in Ur of [the] Chaldeans.
29 Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
And he took Abram and Nahor for themselves wives [the] name of [the] wife of Abram [was] Sarai and [the] name of [the] wife of Nahor [was] Milcah [the] daughter of Haran [the] father of Milcah and [the] father of Iscah.
30 Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
And she was Sarai barren not [belonged] to her a child.
31 Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
And he took Terah Abram son his and Lot [the] son of Haran [the] son of son his and Sarai daughter-in-law his [the] wife of Abram son his and they went out with them from Ur of [the] Chaldeans to go [the] land of towards Canaan and they came to Haran and they dwelt there.
32 Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.
And they were [the] days of Terah five years and two hundred year[s] and he died Terah in Haran.