29Ofiri, Havila, na Yobabi. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30Mpaka wao ulikuwa unaanzia Mesha, hadi Sefari, mlima wa mashariki.
31Hawa walikuwa wana wa Shemu, kulingana na koo zao na lugha zao, katika ardhi zao kulingana na mataifa yao.
32Hizi zilikuwa koo za wana wa Nuhu, kulingana na vizazi vyao, kwa mataifa yao. Kutokea kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi baada ya gharika.