< Mwanzo 10 >

1 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya wana wa Nuhu, ambao ni, Shemu, Hamu, na Yafethi. Wana wa kiume walizaliwa kwao baada ya gharika.
Esta es la historia de las generaciones de los hijos de Noé y de Sem, Cam y Jafet. Les nacieron hijos después del diluvio.
2 Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Masheki, na Tirasi.
Los hijos de Jafet fueron: Gomer, Magog, Madai, Javan, Tubal, Mesec y Tiras.
3 Na wana wa Gomeri walikuwa Ashikenazi, Rifathi na Togama.
Los hijos de Gomer fueron: Askenaz, Rifat y Togarma.
4 Wana wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Dodanimu.
Los hijos de Javán fueron: Elisa, Tarsis, Quitim y Dodanim.
5 Kutoka kwa hawa watu wa pwani waligawanyika na kwenda kwenye ardhi zao, kila mtu na lugha yake, kufuatana na koo zao, kwa mataifa yao.
De éstos se dividieron las islas de las naciones en sus tierras, cada uno según su lengua, según sus familias, en sus naciones.
6 Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misraimu, Putu, na Kanaani.
Los hijos de Cam fueron: Cus, Mizraim, Put y Canaán.
7 Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabta, Raama, na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.
Los hijos de Cus fueron: Seba, Havila, Sabta, Raama y Sabteca. Los hijos de Raama fueron: Sabá y Dedán.
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikuwa hodari wa kwanza juu ya nchi.
Cus fue el padre de Nimrod. Él comenzó a ser un poderoso en la tierra.
9 Alikuwa mwindaji mkuu mbele ya Yahwe. Hii ndiyo sababu hunenwa, “Kama Nimrod mwindaji mkuu mbele za Yahwe.”
Fue un poderoso cazador ante Yahvé. Por eso se dice: “como Nimrod, un poderoso cazador ante Yahvé”.
10 Miji ya kwanza ya ufalme wake ilikuwa Babeli, Ereku, Akadi na Kalne, katika ichi ya Shinari.
El principio de su reino fue Babel, Erec, Acad y Calne, en la tierra de Sinar.
11 Kutoka katika nchi ile alikwenda Ashuru na akajenga Ninawi, Rehoboth- iri na Kala,
De esa tierra pasó a Asiria y construyó Nínive, Rehobot Ir, Cala,
12 na Raseni ambao ulikuwa kati ya Ninawi na Kala. Ulikuwa mji mkubwa.
y Resen entre Nínive y la gran ciudad Cala.
13 Misraimu akazaa Waludi, Waanami, Walehabi, na Wanaftuhi,
Mizraim fue el padre de Ludim, Anamim, Lehabim, Naftuhim,
14 Wapathrusi na Wakasluhi ( ambao kwao Wafilisti walitokea), na Wakaftori.
Patrusim, Casluhim (del que descienden los filisteos) y Caftorim.
15 Kanaani akamzaa Sidono, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
Canaán fue padre de Sidón (su primogénito), de Het, de
16 pia na Myebusi, na Mwamori, Mgirgashi,
de los jebuseos, de los amorreos, de los gergeseos, de
17 Mhivi, Mwarki, Msini,
de los heveos, de los arquitas, de los sinitas, de
18 Mwarvadi, Msemari, na Mhamathi. Baadaye koo za wakanaani zikasambaa.
de los arvaditas, de los zemaritas y de los hamateos. Después, las familias de los cananeos se extendieron por el mundo.
19 Mpaka wa Wakanaani ulianzia Sidoni, katika mwelekeo wa Gerari, hata Gaza, na kama kuelekea Sodoma, Gomora, Adma, na Seboimu hata Lasha.
La frontera de los cananeos iba desde Sidón — en dirección a Gerar — hasta Gaza — en dirección a Sodoma, Gomorra, Adma y Zeboiim — hasta Lasa.
20 Hawa walikuwa wana wa Ham, kwa koo zao, kwa lugha zao, katika ardhi zao na katika mataifa yao.
Estos son los hijos de Cam, por sus familias, según sus lenguas, en sus tierras y sus naciones.
21 Pia walizaliwa wana kwa Shemu, ndugu yake mkubwa wa Yafethi. Shemu pia alikuwa baba yao na watu wote wa Eberi.
También le nacieron hijos a Sem (el hermano mayor de Jafet), el padre de todos los hijos de Éber.
22 Wana wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuru, Alfaksadi, Ludi, na Aramu.
Los hijos de Sem fueron: Elam, Asur, Arfaxad, Lud y Aram.
23 Wana wa Aramu walikuwa ni Usi, Huli, Getheri, na Mashi.
Los hijos de Aram fueron: Uz, Hul, Geter y Mas.
24 Arfaksadi akamzaa Sela, na Sela akamzaa Eber.
Arfaxad fue el padre de Sala. Sala fue el padre de Heber.
25 Eberi akazaa wana wawili wa kiume. Jina la mmoja aliitwa Pelegi maana katika siku zake nchi iligawanyika. Jina la ndugu yake aliitwa Yoktani.
A Heber le nacieron dos hijos. El nombre de uno fue Peleg, porque en sus días la tierra fue dividida. El nombre de su hermano fue Joctán.
26 Yoktani akamzaa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
Joctán fue padre de Almodad, Selef, Hazarmavet, Jera,
27 Hadoram, Uzali, Dikla,
Adoram, Uzal, Dicla,
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
Obal, Abimael, Seba,
29 Ofiri, Havila, na Yobabi. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
Ofir, Havila y Jobab. Todos ellos eran hijos de Joctán.
30 Mpaka wao ulikuwa unaanzia Mesha, hadi Sefari, mlima wa mashariki.
Su morada se extendía desde Mesá, a medida que se avanza hacia Sefar, la montaña del oriente.
31 Hawa walikuwa wana wa Shemu, kulingana na koo zao na lugha zao, katika ardhi zao kulingana na mataifa yao.
Estos son los hijos de Sem, por sus familias, según sus lenguas, tierras y naciones.
32 Hizi zilikuwa koo za wana wa Nuhu, kulingana na vizazi vyao, kwa mataifa yao. Kutokea kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi baada ya gharika.
Estas son las familias de los hijos de Noé, por sus generaciones, según sus naciones. Las naciones se dividieron de éstas en la tierra después del diluvio.

< Mwanzo 10 >