< Wagalatia 1 >
1 Mimi ni Paulo mtume. Mimi sio mtume kutoka kwa wanadamu wala kupitia kwa mwanadamu, lakini kupitia kwa Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua kutoka kwa wafu.
[I], Paul, [write this letter to you. I remind you that I am] an apostle. That is not because a group of people [appointed me], nor because a human being [sent me to be an apostle]. Instead, Jesus Christ and God [our heavenly] Father, who caused Jesus to become alive again after he died, have [appointed and] sent [me to be an apostle].
2 Pamoja na ndugu wote na mimi, ninayaandikia makanisa ya Galatia.
All the fellow believers [who are here] with me [approve of this message that I am writing. I am sending this letter] to the congregations that [are] in Galatia [province].
3 Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo,
[I pray that] God, our Father, and the Lord Jesus Christ will kindly [help] you and enable [you to have inner] peace.
4 aliyejitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu ili kwamba atukomboe na nyakati hizi za uovu, kutokana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba. (aiōn )
Christ offered himself [as a sacrifice] in order that [he might remove the guilt for] our sins. He did that in order that he might enable us to not [do the evil things that people who do not know him] do. [He did this] because God, who is our Father, wanted it. (aiōn )
5 Kwake uwe utukufu milele na milele. (aiōn )
[I pray that people will] praise God forever. (May it be so!/Amen!) (aiōn )
6 Ninashangaa kwamba mnageukia haraka kwenye injili nyingine. Ninashangaa kwamba mnageukia mbali kutoka kwake yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo.
I am very disappointed [IRO] that so soon [after you trusted in Christ] you have turned away from [God]. He chose you in order that [you might have what] Christ freely/kindly gives. I am also disappointed that so soon you are believing a different [message which some say is] “good news.”
7 Hakuna injili nyingine, lakini kuna baadhi ya watu wanao wasababishieni nyinyi matatizo na kutaka kubadilisha injili ya Kristo.
Their message is not a true message. [What is happening is that] certain persons are confusing your [minds]. They are desiring to change the good message (that Christ [revealed/about] Christ) [and are creating another message].
8 Lakini hata kama ni sisi au malaika kutoka mbinguni atatangaza kwenu injili tofauti na ile tuliyoitangaza kwenu, na alaaniwe.
But even if we [(exc) apostles] or an angel from heaven would tell you a message that is different from the good message that we told you [before], I [appeal to God] that [he] punish such a person [forever].
9 Kama tulivyo sema mwanzoni, na sasa nasema tena, “Kama kuna mtu atawatangazia kwenu injili tofauti na mliyoipokea, na alaaniwe.”
As I told you previously, so now I tell you this once more: Someone is telling you [what he says is] a good message, but it is a message that is different from [the good message] that I gave you. So I [appeal to God] that [he] severely punish that person.
10 Kwani sasa hivi ninatafuta uthibitisho wa watu au Mungu? Ninatafuta kuwafurahisha wanadamu? Kama ninaendelea kujaribu kuwafurahisha wanadamu, mimi sio mtumishi wa Kristo.
[I said that] because [RHQ] I do not desire that people approve me, [contrary to what some have said about me]. It is God whom I desire to approve me. [Specifically, I do not say and do] [RHQ] things just to please people. If it were still people whom I was trying to please, then I would not be one who [willingly and completely] serves Christ.
11 Ndugu, ninataka ninyi mjue kwamba injili niliyoitangaza haitokani na wanadamu.
My fellow believers, I want you to know that the message about Christ that I proclaim to people is not one that some person [created/thought up].
12 Sikuipokea kutoka kwa mtu, wala sikufundishwa. Badala yake, ilikuwa ni kwa ufunuo wa Yesu Kristo kwangu.
I did not receive this message from a human [messenger], and no [human being] taught it to me. Instead, Jesus Christ revealed it to me.
13 Mmekwisha sikia juu ya maisha yangu ya nyuma katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyokuwa nikilitesa kwa ukali kanisa la Mungu zaidi ya kipimo na kuliteketeza.
People have told you how I used to behave when [I practiced] the Jewish religion. They told you that I continually did very harmful things to the groups of believers that God [established], and they told you that I tried to get rid of those people.
14 Nilikuwa nimeendelea katika Dini ya Kiyahudi zaidi ya ndugu zangu wengi Wayahudi. Nilikuwa na bidii sana katika tamaduni za baba zangu.
I practiced the Jewish religion more thoroughly than many [other Jews] who were my age practiced it. I much more enthusiastically tried to get others to obey the traditions that my ancestors [kept].
15 Lakini Mungu alipendezwa kunichagua mimi kutoka tumboni mwa mama. Aliniita mimi kupitia neema yake
Nevertheless, before I was born, [God] (set me apart/selected me). He chose me [to live eternally], something that I did not deserve.
16 kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili kwamba nimtangaze yeye miongoni mwa watu wa mataifa. Wala sikutafuta ushauri wa mwili na damu
He wanted me to know that Jesus is (his Son/the man who is also God), so that I would tell others the message about him in regions where non-Jews live. But I did not immediately go to any human beings [SYN] in order to gain [an understanding of that message. I received it directly from Christ!]!
17 na sikupanda kwenda Yerusalem kwa wale waliokuwa mitume kabla yangu. Badala yake nilienda Uarabuni na baadae kurudi Damesiki.
I did not [immediately] leave Damascus and go to Jerusalem [for that purpose] to those who were apostles before I was. Instead, I went away to Arabia [region, a desert area]. Later I returned once more to Damascus [city].
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kumtembelea Kefa, nikakaa naye kwa siku kumi na tano.
Then three years after [God revealed this good message to me], I went up to Jerusalem in order that I might meet Peter. But I stayed with him for [only] 15 days, [which was not long enough for him to teach me thoroughly about Christ].
19 Lakini sikuona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndungu yake na Bwana.
I also saw James, the brother of our Lord [Jesus and the leader of the believers there, but] I did not see any other apostle.
20 Tazama, mbele za Mungu, sidanganyi kwa kile niandikacho kwenu.
God knows that what I am writing to you is completely true [LIT]!
21 Kisha nilikwenda mikoa ya Shamu na Kilikia.
After [I left Jerusalem], I went to [the regions of] Syria and Cilicia.
22 Sikuwa najulikana kwa macho kwa makanisa ya Uyahudi yale yaliyokuwa katika Kristo,
[At that time, people in] the Christian congregations that are in Judea [province] still had not met me [SYN] personally.
23 lakini walikuwa wakisikia tu, “Yeye aliyekuwa akitutesa sasa anatangaza imani aliyokuwa akiiharibu.”
They only heard [others say about me] repeatedly, “[Paul], the one who was formerly doing harmful things to us, is now telling the [same message] which we believe and which formerly he was trying (to destroy/to cause people to stop believing)!”
24 Walikuwa wakimtukuza Mungu kwa ajili yangu.
And they praised God because of [what had happened to] me.