< Wagalatia 1 >

1 Mimi ni Paulo mtume. Mimi sio mtume kutoka kwa wanadamu wala kupitia kwa mwanadamu, lakini kupitia kwa Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua kutoka kwa wafu.
Paul, an apostle, not of men, neither by man, but by Jesus Christ, and God the Father, who raised him from the dead,
2 Pamoja na ndugu wote na mimi, ninayaandikia makanisa ya Galatia.
And all the brethren who are with me, to the churches of Galatia.
3 Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo,
Grace be to you, and peace from God the Father, and from our Lord Jesus Christ,
4 aliyejitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu ili kwamba atukomboe na nyakati hizi za uovu, kutokana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba. (aiōn g165)
Who gave himself for our sins, that he might deliver us from this present wicked world, according to the will of God and our Father: (aiōn g165)
5 Kwake uwe utukufu milele na milele. (aiōn g165)
To whom is glory for ever and ever. Amen. (aiōn g165)
6 Ninashangaa kwamba mnageukia haraka kwenye injili nyingine. Ninashangaa kwamba mnageukia mbali kutoka kwake yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo.
I wonder that you are so soon removed from him that called you into the grace of Christ, unto another gospel.
7 Hakuna injili nyingine, lakini kuna baadhi ya watu wanao wasababishieni nyinyi matatizo na kutaka kubadilisha injili ya Kristo.
Which is not another, only there are some that trouble you, and would pervert the gospel of Christ.
8 Lakini hata kama ni sisi au malaika kutoka mbinguni atatangaza kwenu injili tofauti na ile tuliyoitangaza kwenu, na alaaniwe.
But though we, or an angel from heaven, preach a gospel to you besides that which we have preached to you, let him be anathema.
9 Kama tulivyo sema mwanzoni, na sasa nasema tena, “Kama kuna mtu atawatangazia kwenu injili tofauti na mliyoipokea, na alaaniwe.”
As we said before, so now I say again: If any one preach to you a gospel, besides that which you have received, let him be anathema.
10 Kwani sasa hivi ninatafuta uthibitisho wa watu au Mungu? Ninatafuta kuwafurahisha wanadamu? Kama ninaendelea kujaribu kuwafurahisha wanadamu, mimi sio mtumishi wa Kristo.
For do I now persuade men, or God? Or do I seek to please men? If I yet pleased men, I should not be the servant of Christ.
11 Ndugu, ninataka ninyi mjue kwamba injili niliyoitangaza haitokani na wanadamu.
For I give you to understand, brethren, that the gospel which was preached by me is not according to man.
12 Sikuipokea kutoka kwa mtu, wala sikufundishwa. Badala yake, ilikuwa ni kwa ufunuo wa Yesu Kristo kwangu.
For neither did I receive it of man, nor did I learn it; but by the revelation of Jesus Christ.
13 Mmekwisha sikia juu ya maisha yangu ya nyuma katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyokuwa nikilitesa kwa ukali kanisa la Mungu zaidi ya kipimo na kuliteketeza.
For you have heard of my conversation in time past in the Jews’ religion: how that, beyond measure, I persecuted the church of God, and wasted it.
14 Nilikuwa nimeendelea katika Dini ya Kiyahudi zaidi ya ndugu zangu wengi Wayahudi. Nilikuwa na bidii sana katika tamaduni za baba zangu.
And I made progress in the Jews’ religion above many of my equals in my own nation, being more abundantly zealous for the traditions of my fathers.
15 Lakini Mungu alipendezwa kunichagua mimi kutoka tumboni mwa mama. Aliniita mimi kupitia neema yake
But when it pleased him, who separated me from my mother’s womb, and called me by his grace,
16 kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili kwamba nimtangaze yeye miongoni mwa watu wa mataifa. Wala sikutafuta ushauri wa mwili na damu
To reveal his Son in me, that I might preach him among the Gentiles, immediately I condescended not to flesh and blood.
17 na sikupanda kwenda Yerusalem kwa wale waliokuwa mitume kabla yangu. Badala yake nilienda Uarabuni na baadae kurudi Damesiki.
Neither went I to Jerusalem, to the apostles who were before me: but I went into Arabia, and again I returned to Damascus.
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kumtembelea Kefa, nikakaa naye kwa siku kumi na tano.
Then, after three years, I went to Jerusalem, to see Peter, and I tarried with him fifteen days.
19 Lakini sikuona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndungu yake na Bwana.
But other of the apostles I saw none, saving James the brother of the Lord.
20 Tazama, mbele za Mungu, sidanganyi kwa kile niandikacho kwenu.
Now the things which I write to you, behold, before God, I lie not.
21 Kisha nilikwenda mikoa ya Shamu na Kilikia.
Afterwards I came into the regions of Syria and Cilicia.
22 Sikuwa najulikana kwa macho kwa makanisa ya Uyahudi yale yaliyokuwa katika Kristo,
And I was unknown by face to the churches of Judea, which were in Christ:
23 lakini walikuwa wakisikia tu, “Yeye aliyekuwa akitutesa sasa anatangaza imani aliyokuwa akiiharibu.”
But they had heard only: He, who persecuted us in times past, doth now preach the faith which once he impugned:
24 Walikuwa wakimtukuza Mungu kwa ajili yangu.
And they glorified God in me.

< Wagalatia 1 >