< Wagalatia 6 >
1 Ndugu, ikiwa mtu amekamatwa katika uovu, ninyi mlio wa kiroho, mnawiwa kumrejesha huyo ndugu katika roho ya upole. Huku mkijiangalia wenyewe ili msijaribiwe.
Brethren, if a man also may be overtaken in any trespass, ye who [are] spiritual restore such a one in a spirit of meekness, considering thyself — lest thou also may be tempted;
2 Mchukuliane mizigo, na kwa hiyo mtaikamilisha sheria ya Kristo.
of one another the burdens bear ye, and so fill up the law of the Christ,
3 Ikiwa mtu yeyote anajiona ni bora wakati si kitu, anajidanganya mwenyewe.
for if any one doth think [himself] to be something — being nothing — himself he doth deceive;
4 Kila mmoja na aipime kazi yake. Kisha atakuwa na kitu mwenyewe peke yake cha kujisifu, bila kujilinganisha mwenyewe na mtu yeyote.
and his own work let each one prove, and then in regard to himself alone the glorying he shall have, and not in regard to the other,
5 Maana kila mtu atachukua mzigo wake mwenyewe.
for each one his own burden shall bear.
6 Mtu aliyefundishwa neno lazima amshirikishe mazuri yote mwalimu wake.
And let him who is instructed in the word share with him who is instructing — in all good things.
7 Msidanganyike. Mungu hadhihakiwi. Kila apandacho mtu, ndicho atakachovuna pia.
Be not led astray; God is not mocked; for what a man may sow — that also he shall reap,
8 Kila apandaye mbegu katika asili yake ya dhambi atavuna uharibifu, lakini yeye apandaye mbegu katika Roho, atavuna uzima wa milele kutoka kwa Roho. (aiōnios )
because he who is sowing to his own flesh, of the flesh shall reap corruption; and he who is sowing to the Spirit, of the Spirit shall reap life age-during; (aiōnios )
9 Tusichoke katika kutenda mema, maana kwa wakati wake tutavuna ikiwa hatutakata tamaa.
and in the doing good we may not be faint-hearted, for at the proper time we shall reap — not desponding;
10 Hivyo basi, wakati tutakapokuwa na nafasi, tutende mema kwa kila mmoja. Tutende mema zaidi hasa kwa walio ndani ya imani.
therefore, then, as we have opportunity, may we work the good to all, and especially unto those of the household of the faith.
11 Angalieni ukubwa wa barua nilizowaandikia kwa mkono wangu mwenyewe.
Ye see in how large letters I have written to you with my own hand;
12 Wale wanaotaka kufanya mema kwa mtazamo wa mwili ndiyo wenye kuwalazimisha mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu wasiingie kwenye mateso ya msalaba wa Kristo.
as many as are willing to make a good appearance in the flesh, these constrain you to be circumcised — only that for the cross of the Christ they may not be persecuted,
13 Maana hata hao waliotahiriwa wenyewe hawaishiki sheria. Badala yake wanataka ninyi mtahiriwe ili waweze kujivunia miili yenu.
for neither do those circumcised themselves keep the law, but they wish you to be circumcised, that in your flesh they may glory.
14 Isitokee nikajivuna isipokuwa kwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Ni katika yeye ulimwengu umesulubiwa kwangu na mimi katika ulimwengu.
And for me, let it not be — to glory, except in the cross of our Lord Jesus Christ, through which to me the world hath been crucified, and I to the world;
15 Kwa kuwa haijalishi kutahiriwa au kutokutahiriwa kuwa ni kitu. Badala yake uzao mpya ni muhimu.
for in Christ Jesus neither circumcision availeth anything, nor uncircumcision, but a new creation;
16 Kwa wote wenye kuishi kwa kanuni hii, wawe na amani na rehema iwe juu yao wote, na juu ya Israel ya Mungu.
and as many as by this rule do walk — peace upon them, and kindness, and on the Israel of God!
17 Tangu sasa mtu yeyote asinitaabishe, maana nimebeba chapa za Yesu mwilini mwangu.
Henceforth, let no one give me trouble, for I the scars of the Lord Jesus in my body do bear.
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe na roho zenu, ndugu. Amina.
The grace of our Lord Jesus Christ [is] with your spirit, brethren! Amen.