< Wagalatia 6 >
1 Ndugu, ikiwa mtu amekamatwa katika uovu, ninyi mlio wa kiroho, mnawiwa kumrejesha huyo ndugu katika roho ya upole. Huku mkijiangalia wenyewe ili msijaribiwe.
Brethren, even if a man be overtaken in any trespass, ye which are spiritual, restore such a one in a spirit of meekness; looking to thyself, lest thou also be tempted.
2 Mchukuliane mizigo, na kwa hiyo mtaikamilisha sheria ya Kristo.
Bear ye one another’s burdens, and so fulfill the law of Christ.
3 Ikiwa mtu yeyote anajiona ni bora wakati si kitu, anajidanganya mwenyewe.
For if a man thinketh himself to be something, when he is nothing, he deceiveth himself.
4 Kila mmoja na aipime kazi yake. Kisha atakuwa na kitu mwenyewe peke yake cha kujisifu, bila kujilinganisha mwenyewe na mtu yeyote.
But let each man prove his own work, and then shall he have his glorying in regard of himself alone, and not of his neighbour.
5 Maana kila mtu atachukua mzigo wake mwenyewe.
For each man shall bear his own burden.
6 Mtu aliyefundishwa neno lazima amshirikishe mazuri yote mwalimu wake.
But let him that is taught in the word communicate unto him that teacheth in all good things.
7 Msidanganyike. Mungu hadhihakiwi. Kila apandacho mtu, ndicho atakachovuna pia.
Be not deceived; God is not mocked: for whatsoever a man soweth, that shall he also reap.
8 Kila apandaye mbegu katika asili yake ya dhambi atavuna uharibifu, lakini yeye apandaye mbegu katika Roho, atavuna uzima wa milele kutoka kwa Roho. (aiōnios )
For he that soweth unto his own flesh shall of the flesh reap corruption; but he that soweth unto the Spirit shall of the Spirit reap eternal life. (aiōnios )
9 Tusichoke katika kutenda mema, maana kwa wakati wake tutavuna ikiwa hatutakata tamaa.
And let us not be weary in well-doing: for in due season we shall reap, if we faint not.
10 Hivyo basi, wakati tutakapokuwa na nafasi, tutende mema kwa kila mmoja. Tutende mema zaidi hasa kwa walio ndani ya imani.
So then, as we have opportunity, let us work that which is good toward all men, and especially toward them that are of the household of the faith.
11 Angalieni ukubwa wa barua nilizowaandikia kwa mkono wangu mwenyewe.
See with how large letters I have written unto you with mine own hand.
12 Wale wanaotaka kufanya mema kwa mtazamo wa mwili ndiyo wenye kuwalazimisha mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu wasiingie kwenye mateso ya msalaba wa Kristo.
As many as desire to make a fair show in the flesh, they compel you to be circumcised; only that they may not be persecuted for the cross of Christ.
13 Maana hata hao waliotahiriwa wenyewe hawaishiki sheria. Badala yake wanataka ninyi mtahiriwe ili waweze kujivunia miili yenu.
For not even they who receive circumcision do themselves keep the law; but they desire to have you circumcised, that they may glory in your flesh.
14 Isitokee nikajivuna isipokuwa kwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Ni katika yeye ulimwengu umesulubiwa kwangu na mimi katika ulimwengu.
But far be it from me to glory, save in the cross of our Lord Jesus Christ, through which the world hath been crucified unto me, and I unto the world.
15 Kwa kuwa haijalishi kutahiriwa au kutokutahiriwa kuwa ni kitu. Badala yake uzao mpya ni muhimu.
For neither is circumcision anything, nor uncircumcision, but a new creature.
16 Kwa wote wenye kuishi kwa kanuni hii, wawe na amani na rehema iwe juu yao wote, na juu ya Israel ya Mungu.
And as many as shall walk by this rule, peace [be] upon them, and mercy, and upon the Israel of God.
17 Tangu sasa mtu yeyote asinitaabishe, maana nimebeba chapa za Yesu mwilini mwangu.
From henceforth let no man trouble me: for I bear branded on my body the marks of Jesus.
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe na roho zenu, ndugu. Amina.
The grace of our Lord Jesus Christ be with your spirit, brethren. Amen.