< Wagalatia 6 >

1 Ndugu, ikiwa mtu amekamatwa katika uovu, ninyi mlio wa kiroho, mnawiwa kumrejesha huyo ndugu katika roho ya upole. Huku mkijiangalia wenyewe ili msijaribiwe.
Brethren, even if a man be detected in a fault, do ye who are spiritual restore such a one in the spirit of meekness; considering thyself, lest thou also be tempted.
2 Mchukuliane mizigo, na kwa hiyo mtaikamilisha sheria ya Kristo.
Bear ye one another's burdens, and thus fulfill the law of Christ.
3 Ikiwa mtu yeyote anajiona ni bora wakati si kitu, anajidanganya mwenyewe.
For if a man thinketh himself to be something, when he is nothing, he deceiveth himself.
4 Kila mmoja na aipime kazi yake. Kisha atakuwa na kitu mwenyewe peke yake cha kujisifu, bila kujilinganisha mwenyewe na mtu yeyote.
But let each one prove his own work, and then will he have his ground for boasting in himself alone, and not in comparison with another;
5 Maana kila mtu atachukua mzigo wake mwenyewe.
for every one must bear his own load.
6 Mtu aliyefundishwa neno lazima amshirikishe mazuri yote mwalimu wake.
Let him that is taught in the word share with the teacher in all good things.
7 Msidanganyike. Mungu hadhihakiwi. Kila apandacho mtu, ndicho atakachovuna pia.
Be not deceived; God is not mocked; for whatever a man soweth, that shall he also reap;
8 Kila apandaye mbegu katika asili yake ya dhambi atavuna uharibifu, lakini yeye apandaye mbegu katika Roho, atavuna uzima wa milele kutoka kwa Roho. (aiōnios g166)
for he that soweth to his flesh, shall of the flesh reap corruption; but he that soweth to the Spirit, shall of the Spirit reap life everlasting. (aiōnios g166)
9 Tusichoke katika kutenda mema, maana kwa wakati wake tutavuna ikiwa hatutakata tamaa.
And let us not be faint-hearted in well-doing; for in due season we shall reap, if we faint not.
10 Hivyo basi, wakati tutakapokuwa na nafasi, tutende mema kwa kila mmoja. Tutende mema zaidi hasa kwa walio ndani ya imani.
So then, as we have opportunity, let us do good to all, especially to those who are of the household of faith.
11 Angalieni ukubwa wa barua nilizowaandikia kwa mkono wangu mwenyewe.
See in what large letters I have written to you with my own hand.
12 Wale wanaotaka kufanya mema kwa mtazamo wa mwili ndiyo wenye kuwalazimisha mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu wasiingie kwenye mateso ya msalaba wa Kristo.
As many as desire to make a fair show in the flesh, these are constraining you to be circumcised, only that they may not suffer persecution for the cross of Christ.
13 Maana hata hao waliotahiriwa wenyewe hawaishiki sheria. Badala yake wanataka ninyi mtahiriwe ili waweze kujivunia miili yenu.
For not even do they who become circumcised themselves keep the Law; but they desire to have you circumcised, that they may glory in your flesh.
14 Isitokee nikajivuna isipokuwa kwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Ni katika yeye ulimwengu umesulubiwa kwangu na mimi katika ulimwengu.
But God forbid that I should glory, save in the cross of our Lord Jesus Christ; through whom the world is crucified to me, and I to the world.
15 Kwa kuwa haijalishi kutahiriwa au kutokutahiriwa kuwa ni kitu. Badala yake uzao mpya ni muhimu.
For neither is circumcision anything, nor uncircumcision, but a new creation.
16 Kwa wote wenye kuishi kwa kanuni hii, wawe na amani na rehema iwe juu yao wote, na juu ya Israel ya Mungu.
And as many as walk by this rule, peace be upon them, and mercy, and upon the Israel of God.
17 Tangu sasa mtu yeyote asinitaabishe, maana nimebeba chapa za Yesu mwilini mwangu.
Henceforth let no one trouble me; for I bear the marks of Jesus on my body.
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe na roho zenu, ndugu. Amina.
The grace of our Lord Jesus Christ be with your spirit, brethren. Amen.

< Wagalatia 6 >