< Wagalatia 6 >
1 Ndugu, ikiwa mtu amekamatwa katika uovu, ninyi mlio wa kiroho, mnawiwa kumrejesha huyo ndugu katika roho ya upole. Huku mkijiangalia wenyewe ili msijaribiwe.
Brothers, even if someone is caught in some wrongdoing, you who are spiritual must restore such a one in a spirit of gentleness; looking to yourself so that you also are not tempted.
2 Mchukuliane mizigo, na kwa hiyo mtaikamilisha sheria ya Kristo.
Bear one another's burdens, and so you will fulfill the law of Christ.
3 Ikiwa mtu yeyote anajiona ni bora wakati si kitu, anajidanganya mwenyewe.
For if anyone thinks himself to be something when he is nothing, he deceives himself.
4 Kila mmoja na aipime kazi yake. Kisha atakuwa na kitu mwenyewe peke yake cha kujisifu, bila kujilinganisha mwenyewe na mtu yeyote.
But let each one test his own work, and then he will take pride in himself and not in his neighbor.
5 Maana kila mtu atachukua mzigo wake mwenyewe.
For every person will bear his own load.
6 Mtu aliyefundishwa neno lazima amshirikishe mazuri yote mwalimu wake.
But let him who is taught in the word share all good things with him who teaches.
7 Msidanganyike. Mungu hadhihakiwi. Kila apandacho mtu, ndicho atakachovuna pia.
Do not be deceived. God is not mocked, for whatever a person sows, that he will also reap.
8 Kila apandaye mbegu katika asili yake ya dhambi atavuna uharibifu, lakini yeye apandaye mbegu katika Roho, atavuna uzima wa milele kutoka kwa Roho. (aiōnios )
For he who sows to his own flesh will from the flesh reap corruption. But he who sows to the Spirit will from the Spirit reap everlasting life. (aiōnios )
9 Tusichoke katika kutenda mema, maana kwa wakati wake tutavuna ikiwa hatutakata tamaa.
Let us not be weary in doing good, for we will reap in due season, if we do not give up.
10 Hivyo basi, wakati tutakapokuwa na nafasi, tutende mema kwa kila mmoja. Tutende mema zaidi hasa kwa walio ndani ya imani.
So then, as we have opportunity, let us do what is good toward all people, and especially toward those who are of the household of the faith.
11 Angalieni ukubwa wa barua nilizowaandikia kwa mkono wangu mwenyewe.
See with what large letters I write to you with my own hand.
12 Wale wanaotaka kufanya mema kwa mtazamo wa mwili ndiyo wenye kuwalazimisha mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu wasiingie kwenye mateso ya msalaba wa Kristo.
As many as desire to make a good showing in the flesh, they compel you to be circumcised; only that they may not be persecuted for the cross of Christ.
13 Maana hata hao waliotahiriwa wenyewe hawaishiki sheria. Badala yake wanataka ninyi mtahiriwe ili waweze kujivunia miili yenu.
For even they who receive circumcision do not keep the law themselves, but they desire to have you circumcised, that they may boast in your flesh.
14 Isitokee nikajivuna isipokuwa kwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Ni katika yeye ulimwengu umesulubiwa kwangu na mimi katika ulimwengu.
But far be it from me to boast, except in the cross of our Lord Jesus Christ, through which the world has been crucified to me, and I to the world.
15 Kwa kuwa haijalishi kutahiriwa au kutokutahiriwa kuwa ni kitu. Badala yake uzao mpya ni muhimu.
For neither is circumcision anything, nor uncircumcision, but a new creation.
16 Kwa wote wenye kuishi kwa kanuni hii, wawe na amani na rehema iwe juu yao wote, na juu ya Israel ya Mungu.
As many as walk by this rule, peace and mercy be on them, and on God's Israel.
17 Tangu sasa mtu yeyote asinitaabishe, maana nimebeba chapa za Yesu mwilini mwangu.
From now on, let no one cause me any trouble, for I bear the marks of Jesus branded on my body.
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe na roho zenu, ndugu. Amina.
The grace of our Lord Jesus Christ be with your spirit, brothers. Amen.