< Wagalatia 5 >

1 Ni kwa sababu Kristo alitupa uhuru ili tuwe huru. Hivyo, simameni imara wala msinaswe tena katika kongwa la utumwa.
khrIShTo. asmabhyaM yat svAtantryaM dattavAn yUyaM tatra sthirAstiShThata dAsatvayugena puna rna nibadhyadhvaM|
2 Tazama, Mimi Paulo, ninawaambia kwamba ikiwa mtatahiriwa, Kristo hatawafaidia kwa njia yoyote ile.
pashyatAhaM paulo yuShmAn vadAmi yadi Chinnatvacho bhavatha tarhi khrIShTena kimapi nopakAriShyadhve|
3 Tena, namshuhudia kila mwanaume aliyetahiriwa kwamba anapaswa kuwajibika kwa sheria yote.
aparaM yaH kashchit Chinnatvag bhavati sa kR^itsnavyavasthAyAH pAlanam IshvarAya dhArayatIti pramANaM dadAmi|
4 Mmetengwa mbali na Kristo, wale wote “mnaohesabiwa haki” kwa sheria. Mmeanguka mbali na neema.
yuShmAkaM yAvanto lokA vyavasthayA sapuNyIbhavituM cheShTante te sarvve khrIShTAd bhraShTA anugrahAt patitAshcha|
5 Maana kwa njia ya Roho, kwa imani tunasubiri ujasiri wa haki.
yato vayam AtmanA vishvAsAt puNyalAbhAshAsiddhaM pratIkShAmahe|
6 Katika Kristo Yesu kutahiriwa au kutokutahiriwa hakuna maana yoyote. Ni imani pekee inayofanya kazi kupitia upendo ndiyo humaanisha kitu.
khrIShTe yIshau tvakChedAtvakChedayoH kimapi guNaM nAsti kintu premnA saphalo vishvAsa eva guNayuktaH|
7 Mlikuwa mnapiga mbio vizuri. Nani aliwazuia kutokuitii kweli?
pUrvvaM yUyaM sundaram adhAvata kintvidAnIM kena bAdhAM prApya satyatAM na gR^ihlItha?
8 Ushawishi wa kufanya hivyo hautoki kwake yeye anayewaita ninyi.
yuShmAkaM sA mati ryuShmadAhvAnakAriNa IshvarAnna jAtA|
9 Chachu kidogo huathiri donge zima.
vikAraH kR^itsnashaktUnAM svalpakiNvena jasayate|
10 Nina matumaini na ninyi katika Bwana kwamba hamtafikiri kwa njia nyingine yoyote. Yeyote yule atakayewapotosha atabeba hukumu yake yeye mwenyewe, yeyote yule.
yuShmAkaM mati rvikAraM na gamiShyatItyahaM yuShmAnadhi prabhunAshaMse; kintu yo yuShmAn vichAralayati sa yaH kashchid bhavet samuchitaM daNDaM prApsyati|
11 Ndugu, kama naendelea kutangaza tohara, kwanini bado ninateswa? Kwa suala hilo kile ambacho ni kizuizi cha msalaba kitaweza kuharibiwa.
parantu he bhrAtaraH, yadyaham idAnIm api tvakChedaM prachArayeyaM tarhi kuta upadravaM bhu njiya? tatkR^ite krushaM nirbbAdham abhaviShyat|
12 Ni matakwa yangu kuwa wale wanaowaongoza vibaya watajihasi wenyewe.
ye janA yuShmAkaM chA nchalyaM janayanti teShAM Chedanameva mayAbhilaShyate|
13 Mungu amewaiteni ninyi, ndugu, kwenye uhuru. Ila msiutumie uhuru wenu kama fursa kwa mwili. Badala yake kwa upendo mhudumiane ninyi kwa ninyi.
he bhrAtaraH, yUyaM svAtantryArtham AhUtA Adhve kintu tatsvAtantryadvAreNa shArIrikabhAvo yuShmAn na pravishatu| yUyaM premnA parasparaM paricharyyAM kurudhvaM|
14 Kwa kuwa sheria yote imekamilika katika amri moja; nayo ni “Ni lazima umpende jirani yako kama wewe mwenyewe.”
yasmAt tvaM samIpavAsini svavat prema kuryyA ityekAj nA kR^itsnAyA vyavasthAyAH sArasaMgrahaH|
15 Lakini kama mkiumana na kulana, jiangalieni kwamba msijiharibu ninyi kwa ninyi.
kintu yUyaM yadi parasparaM daMdashyadhve. ashAshyadhve cha tarhi yuShmAkam eko. anyena yanna grasyate tatra yuShmAbhiH sAvadhAnai rbhavitavyaM|
16 Nasema, tembeeni kwa roho, na wala hamtazitimiza tamaa za mwili.
ahaM bravImi yUyam AtmikAchAraM kuruta shArIrikAbhilAShaM mA pUrayata|
17 Kwa kuwa mwili una tamaa kubwa dhidi ya Roho, na Roho ina tamaa kubwa dhidi ya mwili. Hizi zinapingana kila moja na nyingine. Matokeo ni kwamba hamfanyi vitu mnavyotamani kuvifanya.
yataH shArIrikAbhilASha Atmano viparItaH, AtmikAbhilAShashcha sharIrasya viparItaH, anayorubhayoH parasparaM virodho vidyate tena yuShmAbhi ryad abhilaShyate tanna karttavyaM|
18 Lakini kama Roho anawaongoza ninyi, hamko chini ya sheria.
yUyaM yadyAtmanA vinIyadhve tarhi vyavasthAyA adhInA na bhavatha|
19 Sasa matendo ya mwili yanaonekana. Nayo ni uasherati, uchafu, ufisadi,
aparaM paradAragamanaM veshyAgamanam ashuchitA kAmukatA pratimApUjanam
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, husuda, kuwaka hasira, ushindani, faraka, mgawanyiko wa madhehebu,
indrajAlaM shatrutvaM vivAdo. antarjvalanaM krodhaH kalaho. anaikyaM
21 wivu, ulevi, ulafi na mambo mengine kama haya. Nawaonya ninyi, kama nilivyowaonya mwanzoni, kwamba wale wanaofanya mambo kama hayo hawataurithi ufalme wa Mungu.
pArthakyam IrShyA vadho mattatvaM lampaTatvamityAdIni spaShTatvena shArIrikabhAvasya karmmANi santi| pUrvvaM yadvat mayA kathitaM tadvat punarapi kathyate ye janA etAdR^ishAni karmmANyAcharanti tairIshvarasya rAjye. adhikAraH kadAcha na lapsyate|
22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, ukarimu, utu wema, imani,
ki ncha premAnandaH shAntishchirasahiShNutA hitaiShitA bhadratvaM vishvAsyatA titikShA
23 upole, na kiasi. Hakuna sheria dhidi ya mambo kama hayo.
parimitabhojitvamityAdInyAtmanaH phalAni santi teShAM viruddhA kApi vyavasthA nahi|
24 Wale walio wa Kristo Yesu wameusulubisha mwili pamoja na shauku na tamaa zao mbaya.
ye tu khrIShTasya lokAste ripubhirabhilAShaishcha sahitaM shArIrikabhAvaM krushe nihatavantaH|
25 Kama tukiishi kwa Roho, pia tutembee kwa Roho.
yadi vayam AtmanA jIvAmastarhyAtmikAchAro. asmAbhiH karttavyaH,
26 Tusiwe wa kujivuna, tusichokozane kila mmoja na mwenzake, wala tusioneane wivu.
darpaH parasparaM nirbhartsanaM dveShashchAsmAbhi rna karttavyAni|

< Wagalatia 5 >