< Wagalatia 5 >
1 Ni kwa sababu Kristo alitupa uhuru ili tuwe huru. Hivyo, simameni imara wala msinaswe tena katika kongwa la utumwa.
Christ has set us free in freedom; stand fast therefore, and be not held again in a yoke of bondage.
2 Tazama, Mimi Paulo, ninawaambia kwamba ikiwa mtatahiriwa, Kristo hatawafaidia kwa njia yoyote ile.
Behold, I, Paul, say to you, that if ye are circumcised, Christ shall profit you nothing.
3 Tena, namshuhudia kila mwanaume aliyetahiriwa kwamba anapaswa kuwajibika kwa sheria yote.
And I witness again to every man [who is] circumcised, that he is debtor to do the whole law.
4 Mmetengwa mbali na Kristo, wale wote “mnaohesabiwa haki” kwa sheria. Mmeanguka mbali na neema.
Ye are deprived of all profit from the Christ as separated [from him], as many as are justified by law; ye have fallen from grace.
5 Maana kwa njia ya Roho, kwa imani tunasubiri ujasiri wa haki.
For we, by [the] Spirit, on the principle of faith, await the hope of righteousness.
6 Katika Kristo Yesu kutahiriwa au kutokutahiriwa hakuna maana yoyote. Ni imani pekee inayofanya kazi kupitia upendo ndiyo humaanisha kitu.
For in Christ Jesus neither circumcision has any force, nor uncircumcision; but faith working through love.
7 Mlikuwa mnapiga mbio vizuri. Nani aliwazuia kutokuitii kweli?
Ye ran well; who has stopped you that ye should not obey the truth?
8 Ushawishi wa kufanya hivyo hautoki kwake yeye anayewaita ninyi.
The persuasibleness [is] not of him that calls you.
9 Chachu kidogo huathiri donge zima.
A little leaven leavens the whole lump.
10 Nina matumaini na ninyi katika Bwana kwamba hamtafikiri kwa njia nyingine yoyote. Yeyote yule atakayewapotosha atabeba hukumu yake yeye mwenyewe, yeyote yule.
I have confidence as to you in [the] Lord, that ye will have no other mind; and he that is troubling you shall bear the guilt [of it], whosoever he may be.
11 Ndugu, kama naendelea kutangaza tohara, kwanini bado ninateswa? Kwa suala hilo kile ambacho ni kizuizi cha msalaba kitaweza kuharibiwa.
But I, brethren, if I yet preach circumcision, why am I yet persecuted? Then the scandal of the cross has been done away.
12 Ni matakwa yangu kuwa wale wanaowaongoza vibaya watajihasi wenyewe.
I would that they would even cut themselves off who throw you into confusion.
13 Mungu amewaiteni ninyi, ndugu, kwenye uhuru. Ila msiutumie uhuru wenu kama fursa kwa mwili. Badala yake kwa upendo mhudumiane ninyi kwa ninyi.
For ye have been called to liberty, brethren; only [do] not [turn] liberty into an opportunity to the flesh, but by love serve one another.
14 Kwa kuwa sheria yote imekamilika katika amri moja; nayo ni “Ni lazima umpende jirani yako kama wewe mwenyewe.”
For the whole law is fulfilled in one word, in Thou shalt love thy neighbour as thyself;
15 Lakini kama mkiumana na kulana, jiangalieni kwamba msijiharibu ninyi kwa ninyi.
but if ye bite and devour one another, see that ye are not consumed one of another.
16 Nasema, tembeeni kwa roho, na wala hamtazitimiza tamaa za mwili.
But I say, Walk in [the] Spirit, and ye shall no way fulfil flesh's lust.
17 Kwa kuwa mwili una tamaa kubwa dhidi ya Roho, na Roho ina tamaa kubwa dhidi ya mwili. Hizi zinapingana kila moja na nyingine. Matokeo ni kwamba hamfanyi vitu mnavyotamani kuvifanya.
For the flesh lusts against the Spirit, and the Spirit against the flesh: and these things are opposed one to the other, that ye should not do those things which ye desire;
18 Lakini kama Roho anawaongoza ninyi, hamko chini ya sheria.
but if ye are led by the Spirit, ye are not under law.
19 Sasa matendo ya mwili yanaonekana. Nayo ni uasherati, uchafu, ufisadi,
Now the works of the flesh are manifest, which are fornication, uncleanness, licentiousness,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, husuda, kuwaka hasira, ushindani, faraka, mgawanyiko wa madhehebu,
idolatry, sorcery, hatred, strifes, jealousies, angers, contentions, disputes, schools of opinion,
21 wivu, ulevi, ulafi na mambo mengine kama haya. Nawaonya ninyi, kama nilivyowaonya mwanzoni, kwamba wale wanaofanya mambo kama hayo hawataurithi ufalme wa Mungu.
envyings, murders, drunkennesses, revels, and things like these; as to which I tell you beforehand, even as I also have said before, that they who do such things shall not inherit God's kingdom.
22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, ukarimu, utu wema, imani,
But the fruit of the Spirit is love, joy, peace, long-suffering, kindness, goodness, fidelity,
23 upole, na kiasi. Hakuna sheria dhidi ya mambo kama hayo.
meekness, self-control: against such things there is no law.
24 Wale walio wa Kristo Yesu wameusulubisha mwili pamoja na shauku na tamaa zao mbaya.
But they that [are] of the Christ have crucified the flesh with the passions and the lusts.
25 Kama tukiishi kwa Roho, pia tutembee kwa Roho.
If we live by the Spirit, let us walk also by the Spirit.
26 Tusiwe wa kujivuna, tusichokozane kila mmoja na mwenzake, wala tusioneane wivu.
Let us not become vain-glorious, provoking one another, envying one another.