< Wagalatia 5 >
1 Ni kwa sababu Kristo alitupa uhuru ili tuwe huru. Hivyo, simameni imara wala msinaswe tena katika kongwa la utumwa.
Stand firm therefore in the liberty in which Christ freed us, and be not entangled again in a yoke of bondage.
2 Tazama, Mimi Paulo, ninawaambia kwamba ikiwa mtatahiriwa, Kristo hatawafaidia kwa njia yoyote ile.
Behold, I Paul say to you, that if ye are circumcised, Christ will benefit you nothing.
3 Tena, namshuhudia kila mwanaume aliyetahiriwa kwamba anapaswa kuwajibika kwa sheria yote.
And I solemnly declare again to every man who is circumcised, that he is obligated to do the whole law.
4 Mmetengwa mbali na Kristo, wale wote “mnaohesabiwa haki” kwa sheria. Mmeanguka mbali na neema.
Ye were discharged from the Christ, ye who are made righteous by law. Ye have fallen from grace.
5 Maana kwa njia ya Roho, kwa imani tunasubiri ujasiri wa haki.
For we through Spirit, from faith, wait for a hope of righteousness.
6 Katika Kristo Yesu kutahiriwa au kutokutahiriwa hakuna maana yoyote. Ni imani pekee inayofanya kazi kupitia upendo ndiyo humaanisha kitu.
For in Christ Jesus neither circumcision avails anything nor uncircumcision, but faith working through love.
7 Mlikuwa mnapiga mbio vizuri. Nani aliwazuia kutokuitii kweli?
Ye were running well. Who hindered you, not to obey the truth?
8 Ushawishi wa kufanya hivyo hautoki kwake yeye anayewaita ninyi.
This persuasion is not from him who calls you.
9 Chachu kidogo huathiri donge zima.
A little leaven leavens the whole lump.
10 Nina matumaini na ninyi katika Bwana kwamba hamtafikiri kwa njia nyingine yoyote. Yeyote yule atakayewapotosha atabeba hukumu yake yeye mwenyewe, yeyote yule.
I have confidence toward you in the Lord, that ye will think no other thing. But the man who troubles you will bear the verdict, whoever he may be.
11 Ndugu, kama naendelea kutangaza tohara, kwanini bado ninateswa? Kwa suala hilo kile ambacho ni kizuizi cha msalaba kitaweza kuharibiwa.
But I, brothers, if I still preach circumcision, why am I still persecuted? Then the stumbling-block of the cross has been abolished.
12 Ni matakwa yangu kuwa wale wanaowaongoza vibaya watajihasi wenyewe.
O that those who trouble you would even cut it all off.
13 Mungu amewaiteni ninyi, ndugu, kwenye uhuru. Ila msiutumie uhuru wenu kama fursa kwa mwili. Badala yake kwa upendo mhudumiane ninyi kwa ninyi.
For ye, brothers, were called to liberty, only not liberty for an opportunity to the flesh, but be servants to each other through love.
14 Kwa kuwa sheria yote imekamilika katika amri moja; nayo ni “Ni lazima umpende jirani yako kama wewe mwenyewe.”
For the whole law is fulfilled in one word, in this: Thou shall love thy neighbor as thyself.
15 Lakini kama mkiumana na kulana, jiangalieni kwamba msijiharibu ninyi kwa ninyi.
But if ye bite and devour each other, watch out that ye be not consumed by each other.
16 Nasema, tembeeni kwa roho, na wala hamtazitimiza tamaa za mwili.
But I say, walk in Spirit and ye will, no, not fulfill a lust of flesh.
17 Kwa kuwa mwili una tamaa kubwa dhidi ya Roho, na Roho ina tamaa kubwa dhidi ya mwili. Hizi zinapingana kila moja na nyingine. Matokeo ni kwamba hamfanyi vitu mnavyotamani kuvifanya.
For the flesh desires against the Spirit, and the Spirit is against the flesh. For these are hostile to each other, so that whatever these things are ye may want, ye may not do.
18 Lakini kama Roho anawaongoza ninyi, hamko chini ya sheria.
But if ye are led by Spirit ye are not under law.
19 Sasa matendo ya mwili yanaonekana. Nayo ni uasherati, uchafu, ufisadi,
Now the works of the flesh are apparent, which are, adultery, fornication, uncleanness, licentiousness,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, husuda, kuwaka hasira, ushindani, faraka, mgawanyiko wa madhehebu,
idolatry, sorcery, hatreds, strifes, jealousies, wraths, selfish ambitions, dissensions, factions,
21 wivu, ulevi, ulafi na mambo mengine kama haya. Nawaonya ninyi, kama nilivyowaonya mwanzoni, kwamba wale wanaofanya mambo kama hayo hawataurithi ufalme wa Mungu.
envyings, murders, intoxications, revelings, and things like these, of which I forewarn you, as I also did forewarn, that those who practice such things will not inherit the kingdom of God.
22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, ukarimu, utu wema, imani,
But the fruit of the Spirit is love, joy, peace, longsuffering, kindness, goodness, faithfulness,
23 upole, na kiasi. Hakuna sheria dhidi ya mambo kama hayo.
meekness, self-control. Against such things there is no law.
24 Wale walio wa Kristo Yesu wameusulubisha mwili pamoja na shauku na tamaa zao mbaya.
And those of the Christ have crucified the flesh with its passions and the lusts.
25 Kama tukiishi kwa Roho, pia tutembee kwa Roho.
If we live in Spirit, we should also march in Spirit.
26 Tusiwe wa kujivuna, tusichokozane kila mmoja na mwenzake, wala tusioneane wivu.
Let us not become conceited, provoking each other, envying each other.