< Wagalatia 2 >
1 Baada ya miaka kumi na nne nilienda tena Yerusalemu pamoja na Barnaba. Pia nilimchukua Tito pamoja nami.
Then, fourteen years after, I went up again to Jerusalem with Barnabas, and took Titus also with me.
2 Nilienda kwa sababu Mungu alijidhihirisha kwangu kwamba nilipaswa kwenda. Niliweka mbele yao Injili ambayo niliitangaza kwa watu wa mataifa. (Lakini niliongea kwa siri kwa waliosemekana kuwa viongozi muhimu). Nilifanya hivi ili kuhakikisha kwamba nilikuwa sikimbii, au nilikimbia bure.
And I went up by revelation, and communicated to them that gospel which I preach among the gentiles; but privately to those who were of reputation, lest by any means I should run, or had run, in vain.
3 Lakini hata Tito, aliyekuwa pamoja nami, aliyekuwa Myunani, alilazimishwa kutahiriwa.
But not even Titus, who was with me, though he was a Greek, was compelled to be circumcised;
4 Jambo hili lilitokea kwa sababu ya ndugu wa uongo waliokuja kwa siri kupeleleza uhuru tuliokuwa nao katika Kristo Yesu. Walitamani kutufanya sisi kuwa watumwa wa sheria.
and that because of the false brethren stealthily brought in, who crept in to spy out our liberty which we have in Christ Jesus, that they might bring into bondage;
5 Hatukujitoa kuwatii hata kwa saa moja, ili kwamba injili ya kweli ibaki bila kubadilika kwenu.
to whom not even for an hour did we yield by the required subjection, that the truth of the gospel might still remain with you.
6 Lakini wale waliosemwa kuwa walikuwa viongozi hawakuchangia chochote kwangu. Chochote walichokuwa wakikifanya hakikuwa na maana kwangu. Mungu hakubali upendeleo wa wanadamu.
But from those who were reputed to be somewhat—whatever they were, it matters not to me, (God accepteth no man's person, ) for to me those in reputation communicated nothing new.
7 Badala yake, waliniona kwamba nimeaminiwa kuitangaza injili kwa wale ambao hawakutahiriwa. Ilikuwa kama Petro atangaze injili kwa waliotahiriwa.
But on the contrary, when they saw that I was intrusted with the gospel to the uncircumcised, as Peter was with that to the circumcised,
8 Kwa maana Mungu, aliyefanya kazi ndani ya Petro kwa ajili ya utume kwa wale waliotahiriwa, pia alifanya kazi ndani yangu kwa watu wa mataifa.
(for he who wrought for Peter in behalf of the apostleship to the circumcised, wrought also for me in behalf of the gentiles, )
9 Wakati Yakobo, Kefa, na Yohana, waliotambulika kuwa waliojenga Kanisa, walifahamu neema niliyopewa mimi, walitupokea katika ushirika mimi na Barnaba. Walifanya hivi ili kwamba twende kwa watu wa mataifa, na ili kwamba waweze kwenda kwa wale waliotahiriwa.
and when they knew the grace that was given to me, James and Cephas and John, who were reputed to be pillars, gave to me and Barnabas the right hand of fellowship, that we should go to the gentiles, and they to the circumcised;
10 Pia walitutaka sisi kuwakumbuka masikini. Mimi pia nilikuwa natamani kufanya jambo hili.
only they wished us to remember the poor; which very thing I also was earnest to do.
11 Wakati Kefa alipokuja Antiokia, nilimpinga waziwazi kwa sababu alikuwa amekosea.
But when Cephas came to Antioch, I withstood him to the face; for he was condemned.
12 Kabla ya watu kadhaa kuja kutoka kwa Yakobo, Kefa alikuwa akila pamoja na watu wa mataifa. Lakini hawa watu walipokuja, aliacha na kuondoka kutoka kwa watu wa mataifa. Alikuwa anaogopa watu ambao walihitaji tohara.
For before certain persons came from James, he used to eat with the gentiles; but when they came, he withdrew, and separated himself, fearing those who were of the circumcision.
13 Vilevile Wayahudi wengine waliungana na unafiki huu pamoja na Kefa. Matokeo yake yalikuwa kwamba hata Barnaba alichukuliwa na unafiki wao.
And the other Jews also dissembled with him; so that even Barnabas was carried away with their dissimulation.
14 Lakini nilipoona kwamba walikuwa hawafuati injili ya kweli, nilimwambia Kefa mbele yao wote, “Kama ninyi ni Wayahudi lakini mnaishi tabia za watu wa mataifa badala ya tabia za Kiyahudi, kwa nini mnawalazimisha watu wa mataifa kuishi kama Wayahudi?”
But when I saw that they were not walking uprightly according to the truth of the gospel, I said to Cephas in the presence of all, If thou, being a Jew, livest after the manner of gentiles, and not that of the Jews, how is it that thou compellest the gentiles to keep the customs of the Jews?
15 Sisi ambao ni Wayahudi kwa kuzaliwa na siyo “Watu wa mataifa wenye dhambi “
We are Jews by nature, and not sinners of the gentiles;
16 fahamu kwamba hakuna anayehesabiwa haki kwa matendo ya sheria. Badala yake, wanahesabiwa haki kwa imani ndani ya Yesu Kristo. Tulikuja kwa imani ndani ya Kristo Yesu ili kwamba tunahesabiwa haki kwa imani ndani ya Kristo na siyo kwa matendo ya sheria. Kwa matendo ya sheria hakuna mwili utakao hesabiwa haki.
but knowing that a man is not accepted as righteous by the works of the Law, but by faith in Christ Jesus, we also have believed in Christ Jesus, that we might be accepted as righteous by faith in Christ, and not by the works of the Law; for by the works of the Law shall no flesh be accepted as righteous.
17 Lakini kama tunapomtafuta Mungu kwa kutuhesabia haki ndani ya Kristo, tunajikuta wenyewe pia kuwa wenye dhambi, je Kristo alifanywa mtumwa wa dhambi? Siyo hivyo!
But while seeking to be accepted as righteous in Christ, we ourselves also are found sinners, is Christ therefore a minister of sin? Far be it!
18 Maana kama nikijenga tegemeo langu juu ya kutunza sheria, tegemeo ambalo nilikwisha liondoa, najionesha mwenyewe kuwa mvunja sheria.
For if I again build up what I pulled down, I make myself a transgressor.
19 Kupitia sheria nilikufa kwa sheria, kwa hiyo napaswa kuishi kwa ajili ya Mungu.
For I through the Law died to the Law, that I might live to God.
20 Nimesulubiwa pamoja na Kristo. Si mimi tena ninayeishi, bali Kristo anaishi ndani yangu. Maisha ninayoishi katika mwili ninaishi kwa imani ndani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda na akajitoa kwa ajili yangu.
I have been crucified with Christ, and no longer do I live, but Christ liveth in me; and the life which I now live in the flesh I live in faith in the Son of God, who loved me, and gave himself for me.
21 Siikani neema ya Mungu, maana kama haki ilikuwepo kupitia sheria, basi Kristo angekuwa amekufa bure.
I do not set aside the grace of God; for if righteousness come through the Law, then did Christ die for nought.