< Wagalatia 2 >

1 Baada ya miaka kumi na nne nilienda tena Yerusalemu pamoja na Barnaba. Pia nilimchukua Tito pamoja nami.
Fourteen years later I went up to Jerusalem again, with Barnabas, and took Titus also with me
2 Nilienda kwa sababu Mungu alijidhihirisha kwangu kwamba nilipaswa kwenda. Niliweka mbele yao Injili ambayo niliitangaza kwa watu wa mataifa. (Lakini niliongea kwa siri kwa waliosemekana kuwa viongozi muhimu). Nilifanya hivi ili kuhakikisha kwamba nilikuwa sikimbii, au nilikimbia bure.
(I went up at that time in obedience to a revelation). And I laid before them the gospel which I am wont to preach among the Gentiles. I did this privately before those in authority, lest by any means I should be running, or should already have run, in vain.
3 Lakini hata Tito, aliyekuwa pamoja nami, aliyekuwa Myunani, alilazimishwa kutahiriwa.
But although Titus, my companion, was a Greek, they did not compel even him to be circumcised.
4 Jambo hili lilitokea kwa sababu ya ndugu wa uongo waliokuja kwa siri kupeleleza uhuru tuliokuwa nao katika Kristo Yesu. Walitamani kutufanya sisi kuwa watumwa wa sheria.
Yet there were false brethren who had crept in to spy out the freedom we enjoy in Christ Jesus, in order to enslave us again.
5 Hatukujitoa kuwatii hata kwa saa moja, ili kwamba injili ya kweli ibaki bila kubadilika kwenu.
To them we did not yield submission even for an hour, in order that the truth of the gospel might abide unshaken among you.
6 Lakini wale waliosemwa kuwa walikuwa viongozi hawakuchangia chochote kwangu. Chochote walichokuwa wakikifanya hakikuwa na maana kwangu. Mungu hakubali upendeleo wa wanadamu.
But those in authority - what they once were makes no difference to me; God is no respecter of persons - those I say who were in authority had no additions to make my message.
7 Badala yake, waliniona kwamba nimeaminiwa kuitangaza injili kwa wale ambao hawakutahiriwa. Ilikuwa kama Petro atangaze injili kwa waliotahiriwa.
On the contrary, when they saw that I had been entrusted with the gospel for the uncircumcised, just as Peter has with the gospel for the circumcised
8 Kwa maana Mungu, aliyefanya kazi ndani ya Petro kwa ajili ya utume kwa wale waliotahiriwa, pia alifanya kazi ndani yangu kwa watu wa mataifa.
(for he who has equipped Peter for the apostleship to the circumcised, equipped me also for the apostleship to the Gentiles),
9 Wakati Yakobo, Kefa, na Yohana, waliotambulika kuwa waliojenga Kanisa, walifahamu neema niliyopewa mimi, walitupokea katika ushirika mimi na Barnaba. Walifanya hivi ili kwamba twende kwa watu wa mataifa, na ili kwamba waweze kwenda kwa wale waliotahiriwa.
and when they recognized the grace which had been given to me, James and Cephas and John, then thought to be pillars, gave to Barnabas and to me the right hand of fellowship. They agreed that we should go to the Gentiles and they to the Jews.
10 Pia walitutaka sisi kuwakumbuka masikini. Mimi pia nilikuwa natamani kufanya jambo hili.
They stipulated only that we should remember the poor, which very thing indeed I was quite eager to do.
11 Wakati Kefa alipokuja Antiokia, nilimpinga waziwazi kwa sababu alikuwa amekosea.
But when Cephas came to Antioch I resisted him to his face, because he stood self-condemned.
12 Kabla ya watu kadhaa kuja kutoka kwa Yakobo, Kefa alikuwa akila pamoja na watu wa mataifa. Lakini hawa watu walipokuja, aliacha na kuondoka kutoka kwa watu wa mataifa. Alikuwa anaogopa watu ambao walihitaji tohara.
For until certain men came from James he used to eat with the Gentile Christians, but when they came, he began to draw back and to separate himself, because he was afraid of the circumcision party.
13 Vilevile Wayahudi wengine waliungana na unafiki huu pamoja na Kefa. Matokeo yake yalikuwa kwamba hata Barnaba alichukuliwa na unafiki wao.
And the rest of the Jewish Christians also dissimulated with him, so that even Barnabas was carried away by their hypocrisy.
14 Lakini nilipoona kwamba walikuwa hawafuati injili ya kweli, nilimwambia Kefa mbele yao wote, “Kama ninyi ni Wayahudi lakini mnaishi tabia za watu wa mataifa badala ya tabia za Kiyahudi, kwa nini mnawalazimisha watu wa mataifa kuishi kama Wayahudi?”
But when I saw that they were not walking a straight path, in the presence of the truth of the gospel, I said to Cephas before them all. "If you, although you are a Jew, live like the Gentiles and not like the Jews, why do you try to compel the Gentiles to become Jews?
15 Sisi ambao ni Wayahudi kwa kuzaliwa na siyo “Watu wa mataifa wenye dhambi “
"We are Jews by birth, and not ‘Gentile sinners’;
16 fahamu kwamba hakuna anayehesabiwa haki kwa matendo ya sheria. Badala yake, wanahesabiwa haki kwa imani ndani ya Yesu Kristo. Tulikuja kwa imani ndani ya Kristo Yesu ili kwamba tunahesabiwa haki kwa imani ndani ya Kristo na siyo kwa matendo ya sheria. Kwa matendo ya sheria hakuna mwili utakao hesabiwa haki.
"yet because we know that no man is justified by the works of the Law, but by the faith of Jesus Christ, we ourselves also have put our faith in Jesus Christ, that we might be justified by the faith of Christ, and not by the works of the Law; for "By the works of the Law shall no flesh be justified."
17 Lakini kama tunapomtafuta Mungu kwa kutuhesabia haki ndani ya Kristo, tunajikuta wenyewe pia kuwa wenye dhambi, je Kristo alifanywa mtumwa wa dhambi? Siyo hivyo!
But if while seeking to be justified in Christ we ourselves also have been found to be sinners, is Christ then a minister of sin? Far from it!
18 Maana kama nikijenga tegemeo langu juu ya kutunza sheria, tegemeo ambalo nilikwisha liondoa, najionesha mwenyewe kuwa mvunja sheria.
For if I am rebuilding the very things which I destroyed, I am proving myself a transgressor.
19 Kupitia sheria nilikufa kwa sheria, kwa hiyo napaswa kuishi kwa ajili ya Mungu.
For it is through law I died to law, in order to live to God.
20 Nimesulubiwa pamoja na Kristo. Si mimi tena ninayeishi, bali Kristo anaishi ndani yangu. Maisha ninayoishi katika mwili ninaishi kwa imani ndani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda na akajitoa kwa ajili yangu.
I have been crucified with Christ, so it is no longer I who am living, but it is Christ who is living in me; and the life I am now living in the flesh, I am living in faith of the Son of God who loved me and gave himself up for me.
21 Siikani neema ya Mungu, maana kama haki ilikuwepo kupitia sheria, basi Kristo angekuwa amekufa bure.
I do not annul the grace of God; for if righteousness comes by way of the Law, then indeed Christ died Christ for nothing.

< Wagalatia 2 >