< Wagalatia 1 >
1 Mimi ni Paulo mtume. Mimi sio mtume kutoka kwa wanadamu wala kupitia kwa mwanadamu, lakini kupitia kwa Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua kutoka kwa wafu.
Paul, Apôtre (non par la grâce des hommes, ni par l'intermédiaire d'un homme, mais par l'intermédiaire de Jésus-Christ et par la grâce de Dieu le Père, qui a ressuscité Jésus d'entre les morts),
2 Pamoja na ndugu wote na mimi, ninayaandikia makanisa ya Galatia.
ainsi que tous les frères qui sont avec moi, aux églises de Galatie:
3 Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo,
que la grâce et la paix vous soient données par Dieu notre Père et par notre Seigneur Jésus-Christ,
4 aliyejitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu ili kwamba atukomboe na nyakati hizi za uovu, kutokana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba. (aiōn )
qui s'est donné lui-même pour nos péchés, afin de nous arracher à la corruption du siècle présent, conformément à la volonté de Dieu notre Père, (aiōn )
5 Kwake uwe utukufu milele na milele. (aiōn )
à qui appartient la gloire aux siècles des siècles. Amen! (aiōn )
6 Ninashangaa kwamba mnageukia haraka kwenye injili nyingine. Ninashangaa kwamba mnageukia mbali kutoka kwake yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo.
Je suis surpris que si vite vous vous laissiez détourner de Celui qui vous a appelés à la grâce de Christ, pour passer à un autre évangile;
7 Hakuna injili nyingine, lakini kuna baadhi ya watu wanao wasababishieni nyinyi matatizo na kutaka kubadilisha injili ya Kristo.
non qu'il y ait un autre évangile, mais il y a certaines gens qui vous troublent, et qui veulent renverser l'évangile de Christ.
8 Lakini hata kama ni sisi au malaika kutoka mbinguni atatangaza kwenu injili tofauti na ile tuliyoitangaza kwenu, na alaaniwe.
Mais, quand nous-même, quand un ange venu du ciel vous annoncerait un autre évangile que celui que nous avons annoncé, qu'il soit anathème!
9 Kama tulivyo sema mwanzoni, na sasa nasema tena, “Kama kuna mtu atawatangazia kwenu injili tofauti na mliyoipokea, na alaaniwe.”
Nous l'avons déjà dit, et nous vous le répétons à cette heure: si quelqu'un vous annonce un autre évangile que celui que vous avez reçu, qu'il soit anathème!
10 Kwani sasa hivi ninatafuta uthibitisho wa watu au Mungu? Ninatafuta kuwafurahisha wanadamu? Kama ninaendelea kujaribu kuwafurahisha wanadamu, mimi sio mtumishi wa Kristo.
Est-ce la faveur des hommes que je me concilie en ce moment, ou celle de Dieu? Est-ce aux hommes que je cherche à plaire? Si je plaisais encore aux hommes, je ne serais pas serviteur de Dieu.
11 Ndugu, ninataka ninyi mjue kwamba injili niliyoitangaza haitokani na wanadamu.
Je vous le déclare, mes frères: l'évangile que j'ai prêché n'a rien qui soit de l'homme,
12 Sikuipokea kutoka kwa mtu, wala sikufundishwa. Badala yake, ilikuwa ni kwa ufunuo wa Yesu Kristo kwangu.
car ce n'est pas d'un homme que je le tiens ni que je l'ai appris; je l'ai appris par une révélation de Jésus-Christ.
13 Mmekwisha sikia juu ya maisha yangu ya nyuma katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyokuwa nikilitesa kwa ukali kanisa la Mungu zaidi ya kipimo na kuliteketeza.
Vous avez entendu parler de ma conduite quand j'étais dans le judaïsme; vous savez que je persécutais à outrance et ravageais l'Église de Dieu,
14 Nilikuwa nimeendelea katika Dini ya Kiyahudi zaidi ya ndugu zangu wengi Wayahudi. Nilikuwa na bidii sana katika tamaduni za baba zangu.
et que je surpassais par mes progrès dans le judaïsme bon nombre de ceux de mon âge et de ma race, à cause de mon zèle excessif pour les traditions de mes pères.
15 Lakini Mungu alipendezwa kunichagua mimi kutoka tumboni mwa mama. Aliniita mimi kupitia neema yake
Mais, quand Celui qui m'a choisi dès le sein de ma mère et qui m'a appelé par sa grâce,
16 kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili kwamba nimtangaze yeye miongoni mwa watu wa mataifa. Wala sikutafuta ushauri wa mwili na damu
daigna me révéler son Fils, afin que je l'annonçasse parmi les Gentils, sur le champ, sans consulter ni la chair ni le sang,
17 na sikupanda kwenda Yerusalem kwa wale waliokuwa mitume kabla yangu. Badala yake nilienda Uarabuni na baadae kurudi Damesiki.
sans même aller à Jérusalem vers ceux qui étaient apôtres avant moi, je me rendis en Arabie, puis je retournai à Damas.
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kumtembelea Kefa, nikakaa naye kwa siku kumi na tano.
Ensuite, trois ans après, je montai à Jérusalem pour faire connaissance avec Céphas, et je restai quinze jours avec lui;
19 Lakini sikuona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndungu yake na Bwana.
mais je ne vis aucun des autres apôtres, si ce n’est Jacques, le frère du Seigneur.
20 Tazama, mbele za Mungu, sidanganyi kwa kile niandikacho kwenu.
Je déclare devant Dieu que je ne mens point dans tout ce que je vous dis.
21 Kisha nilikwenda mikoa ya Shamu na Kilikia.
J'allai ensuite dans les parages de la Syrie et de la Cilicie;
22 Sikuwa najulikana kwa macho kwa makanisa ya Uyahudi yale yaliyokuwa katika Kristo,
mais mon visage était inconnu aux églises de Christ qui sont en Judée.
23 lakini walikuwa wakisikia tu, “Yeye aliyekuwa akitutesa sasa anatangaza imani aliyokuwa akiiharibu.”
Seulement, elles avaient entendu dire que celui qui les persécutait autrefois, prêchait maintenant la foi, qu'il s'efforçait alors de détruire;
24 Walikuwa wakimtukuza Mungu kwa ajili yangu.
et elles glorifiaient Dieu à mon sujet.