< Ezekieli 7 >

1 Neno la Yahwe likanijia, likisema,
And there is a word of YHWH to me, saying, “And you, son of man, Thus said Lord YHWH to the ground of Israel:
2 Wewe, mwanadamu-Bwana Yahwe asema hivi kwa nchi ya Israeli.”'Mwisho! Mwisho umekuja kwenye mipaka minne ya nchi.
An end, the end has come on the four corners of the land.
3 Sasa mwisho uko juu yako, kwa kuwa natuma ghadhabu yangu juu yako, nitakuhukumu kulingana na njia zako; nitaleta machukizo yako yote juu yako.
Now [is] the end for you, And I have sent My anger on you, And judged you according to your ways, And set all your abominations against you.
4 Kwa kuwa macho yangu hayatakuhurumia, na sitakuharibu. Badala yake, nitaleta njia zako zote juu yako, na machukizo yako yote yatakuwa katikati yako, hivyo utajua kwamba mimi ni Yahwe.
And My eye has no pity on you, nor do I spare, For I set your ways against you, And your abominations are in your midst, And you have known that I [am] YHWH.
5 Bwana Yahwe asema hivi: Msiba! Msiba wa pekee! Tazama, unakuja.
Thus said Lord YHWH: Calamity, a single calamity, behold, it has come.
6 Mwisho unakuja hakika. Mwisho umeamsha dhidi yenu. Tazama! unakuja!
An end has come, the end has come, It has awoken for you, behold, it has come.
7 Kifo chako kinakuja kwako ukaaye kwenye nchi. Mda umefika; siku ya uharibifu iko karibu, na milima haitakuwa na shangwe tena.
The circlet has come to you, O inhabitant of the land! The time has come, a day of trouble [is] near, And not the shouting of mountains.
8 Sasa baada ya mda mfupi nitamwaga dhahabu yangu juu yako na kujaza hasira yangu juu yako wakati nitakapokuhukumu kulingana na njia zako na kuleta machukizo yako yote juu yako.
Now shortly I pour out My fury on you, And have completed My anger against you, And judged you according to your ways, And set all your abominations against you.
9 Kwa kuwa jicho langu halitaona kwa huruma, sitakuharibu, kama ulivyofanya, nitafanya kwako; na machukizo yako yatakuwa katikati yako hivyo utajua kwamba ni mimi Yahwe, anayekuadhibu.
And My eye does not pity, nor do I spare, I give to you according to your ways, And your abominations are in your midst, And you have known that [it is] I, YHWH, striking.
10 Tazama, siku! Tazama, inakuja! Kifo kimetoka! fimbo ya kuadhibia imechanua, kiburi kimechipua!
Behold, the day, behold, it has come, The circlet has gone forth, The rod has blossomed, the pride has flourished.
11 Udhalimu umekua kwenye fimbo ya udhaifu-hakuna kati yao, na hakuna katika ya kundi lao, hakuna katika utajiri wao, na hakuna wa muhimu wao atakaye baki!
The violence has risen to a rod of wickedness, There is none of them, nor of their multitude, Nor of their noise, nor is there wailing for them.
12 Muda unakuja; siku imekaribia. Usimuache anayenunua shangwe, wala asihuzunike auzaye, kwa kuwa hasira yangu iko juu ya kikundi kizima!
The time has come, the day has arrived, The buyer does not rejoice, And the seller does not become a mourner, For wrath [is] to all its multitude.
13 Kwa kuwa muuzaji hatarudia kile kilichouzwa, kadiri wanapoendelea kuishi, kwa kuwa maono yako juu yako kikundi kizima. Hawatarudi, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi kwenye dhambi atakayejitia nguvu!
For the seller does not turn to the sold thing, And yet their life [is] among the living, For the vision [is] to all its multitude, It does not turn back, And none strengthens his life by his iniquity.
14 Wamepiga tarumbeta na kufanya kila kitu tayari, lakini hakuna mtu anayeenda kupigana; kwa kuwa hasira yangu iko juu ya kundi zima.
They have blown with a horn to prepare the whole, And none is going to battle, For My wrath [is] to all its multitude.
15 Upanga uko nje, na tauni na njaa viko nje kwenye jengo. Wale walioko shambani watakufa kwa upanga, wakati njaa na tauni zitakapowala wale waliopo kwenye mji.
The sword [is] outside, And the pestilence and the famine within, He who is in a field dies by sword, And he who is in a city—Famine and pestilence devour him.
16 Lakini watakao salia watatoroka kutoka miongoni mwao, na watakwenda kwenye milima. Kama hua wa mabondeni, wote watalia-kila mtu kwa ajili ya uovu wake.
And their fugitives have escaped away, And they have been on the mountains As doves of the valleys, All of them making a noise—each for his iniquity.
17 Kila mkono utasita na kila goti litakuwa dhaifu kama maji, na watavaa nguo za magunia, na hofu kuu itawafunika,
All the hands are feeble, and all knees go [as] waters.
18 na aibu itakuwa juu ya kila uso, na upara juu ya vichwa vyao vyote.
And they have girded on sackcloth, And trembling has covered them, And shame [is] on all faces, And baldness on all their heads.
19 Watatupa fedha yao kwenye mitaa na dhahabu yao itakuwa kama jalala. Fedha yao na dhahabu yao haitaweza kuwaokoa katika siku ya ghadhabu ya Yahwe. Maisha yao hayataokolewa, na njaa yao haitashiba, kwa sababu uovu wao umekuwa kizuizi.
They cast their silver into out-places, And their gold becomes impurity. Their silver and gold are not able to deliver them, In a day of the wrath of YHWH, They do not satisfy their soul, And they do not fill their bowels, For it has been the stumbling-block of their iniquity.
20 Kwenye fahari yao walichukua kito yake nzuri za mapambo, pamoja nao wakatengeza sanamu zao za vinyago, na vitu vyao vichukizavyo. Kwa hiyo, nayabadilisha haya kuwa kitu najisi kwao.
As for the beauty of his ornament, He set it for excellence, And the images of their abominations, Their detestable things—they made in it, Therefore I have given it to them for impurity,
21 Kisha nitawapatia hivyo vitu kwenye mikono ya wageni kama mateka na kwa waovu wa dunia kama mateka, na watapanajisi.
And I have given it into the hand of the strangers for a prey, And to the wicked of the land for a spoil, And they have defiled it.
22 Kisha nitaugeuza uso wangu mbali kutoka kwao watakapo najisi mahali pangu pa siri; maharamia wataingia humo na kupanajisi.
And I have turned My face from them, And they have defiled My hidden place, Indeed, destroyers have come into it, and defiled it.
23 Tengeneza mnyororo, kwa sababu nchi imejaa hukumu ya damu, na mji umejaa udhalimu.
Make the chain; for the land Has been full of bloody judgments, And the city has been full of violence.
24 Hivyo nitaleta waovu wengi wa mataifa, na watamilki nyumba zao, na nitaleta mwisho kwenye fahari ya uweza, kwenda mahali pao patakatifu patanajisiwa!
And I have brought in the wicked of the nations, And they have possessed their houses, And I have caused the excellence of the strong to cease, And those sanctifying them have been defiled.
25 Hofu itakuja! Wataitafuta amani, lakini haitakuwepo.
Destruction has come, And they have sought peace, and there is none.
26 Majanga juu ya majanga yatakuja juu yangu, na kutakuwa na tetesi juu ya tetesi. Kisha watatafuta ono moja kutoka kwa nabii, lakini sheria itawaangamiza kutoka kwa kuhani na shauri kutoka kwa wazee.
Disaster comes on disaster, and report is on report, And they have sought a vision from a prophet, And law perishes from [the] priest, And counsel from [the] elderly,
27 Mfalme ataomboleza na mwana wa mfalme atakata tamaa, wakati mikono ya watu wa nchi itatetemeka kwa hofu. Kulingana na njia zao wenyewe nitafanya hivi kwao! Nitawahukumu sawa sawa na wanavyostahili hadi watakapojua yakwamba mimi ni Yahwe.'”
The king becomes a mourner, And a prince puts on desolation, And the hands of the people of the land are troubled, I deal with them from their own way, And I judge them with their own judgments, And they have known that I [am] YHWH!”

< Ezekieli 7 >