< Ezekieli 5 >

1 “Kisha wewe mwana wa adamu, chukua upanga mkali kama wembe wa kinyozi kwa ajili yako mwenyewe, na pitisha hayo makali juu ya kichwa chako na ndevu zako, kisha chukua mizani za kupimia uzito na uzigawanye nywele zako.
“Then you, son of man, take a sharp sword as a barber's razor for yourself, and pass the razor over your head and your beard, then take scales to weigh and divide your hair.
2 Choma theluthi ya tatu ya hiyo kwa moto katikati ya mji wakati siku za kuzingirwa zitakapokamilika, na chukua theluthi ya nywele na uipige kwa panga na kuuzunguka mji. Kisha tawanya theluthi yake kwenye upepo, na nitasogeza panga karibu ili kufukuza watu.
Burn a third of it with fire in the midst of the city when the days of the siege are completed, and take a third of the hair and strike it with the sword all around the city. Then scatter a third of it to the wind, and I will draw out a sword to chase after the people.
3 Lakini chukua kiasi kidogo cha nywele na zifunge kwenye pindo za nguo yako.
But take a small number of hairs from them and tie them into the folds of your robe.
4 Kisha chukua tena zile nyewele na zitupe katikati ya moto; na zichome kwenye moto; kutoka hapo utatoka nje kwenda nyumba zote za Israeli.”
Then take more of the hair and throw it into the midst of the fire; and burn it in the fire; from there a fire will go out to all the house of Israel.”
5 Bwana Yahwe asema hivi, “Hii ndio Yerusalemu katikati ya mataifa, nilipomuweka, na ambapo nilipomzunguka kwa nchi zingine.
The Lord Yahweh says this, “This is Jerusalem in the midst of the nations, where I have placed her, and where I have surrounded her with other lands.
6 Lakini anaudhaifu wa kukataa amri zangu zaidi kuliko mataifa yalivyo, na sheria yangu zaidi kuliko mataifa ambayo yanayomzunguka. Watu wamezikataa humuku zangu na kuacha kutembea katika sheria zangu.”
But she has in wickedness rejected my decrees more than the nations have, and my statutes more than the countries that surround her. The people have rejected my judgments and have not walked in my statutes.”
7 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, “Kwa sababu mmekuwa kikwazo kuliko mataifa ambayo yanayowazunguka na kuacha kutembea kwenye amri zangu wala kutenda kulingana na amri zangu, wala hata kutenda kulingana na amri za mataifa yanayowazunguka,”
Therefore the Lord Yahweh says this, “Because you are more troublesome than the nations that surround you and have not walked in my statutes or acted according to my decrees, or even acted according to the decrees of the nations that surround you,”
8 kwa hiyo Bwana asema hivi, “Tazama! Mimi mwenyewe nitatenda juu yenu. Nitato hukumu kati yenu ili mataifa waone.
therefore the Lord Yahweh says this, “Behold! I myself will act against you. I will execute judgments within your midst for the nations to see.
9 Nitawafanyia yale ambayo sijawahi kuyafanya na kile ambacho sintokifanya tena, kwa sababu ya matendo yenu ya kuchukiza.
I will do to you what I have not done and the like of which I will not do again, because of all your disgusting actions.
10 Kwa hiyo baba watawala watoto kati yenu, na watoto watawala baba zao, kwa kuwa nitafanya hukumu juu yenu na kuwatawanya kila mahali wote ninyi mliobaki.
Therefore fathers will eat the children in your midst, and sons will eat their fathers, since I will execute judgment on you and scatter to every direction all of you who are left.
11 Kwa hiyo, kama niishivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-bila shaka hii ilikuwa kwa sababu umapanajisi patakatifu pangu kwa mambo ya machukizo yako yote na kwa matendo yako yote niyachukiayo, kwamba mimi mwenyewe nitakupunguza katika hesabu; jicho langu halitakuhurumia, na sintoacha kukuharibu.
Therefore, as I live—this is the Lord Yahweh's declaration—it is certainly because you have defiled my sanctuary with all your hateful things and with all your disgusting deeds, that I myself will reduce you in number; my eye will not have pity on you, and I will not spare you.
12 Theluthi yenu mtakufa kwa tauni, na wataliwa na njaa katikati yenu. Theluthi wataanguka kwa upanga likiwazunguka. Kisha nitawatawanya theluthi katika mahali pote, na nitafuatisha upanga kuwafukuza pia.
A third of you will die by plague, and they will be consumed by famine in your midst. A third will fall by the sword surrounding you. Then I will scatter a third in every direction, and draw out a sword to chase after them as well.
13 Hivi ndivyo ghadhabu yangu itavyokamilika, na nitasababisha ghadhabu yangu juu yao hata kulala. Nitajiridhisha, na watajua kwamba, mimi Yahwe, nimenena kwa ghadhabu yangu wakati nitakapo kamilisha ghadhabu yangu dhidi yao.
Then my wrath will be completed, and I will cause my fury toward them to rest. I will be satisfied, and they will know that I, Yahweh, have spoken in my wrath when I have completed my fury against them.
14 Nitakufanya mkiwa kwa mataifa yanayokuzunguka kwenye uso wa kila mtu apitaye karibu.
I will make you a desolation and a reproach to the nations that surround you in the sight of everyone who passes by.
15 Hivyo Yerusalemu itakuwa jambo kwa watu wengine kushutumu na kufanya mzaha, na chukizo kwa mataifa ambayo yanayowazunguka. Nitafanya hukumu dhidi yenu kwa ghadhabu na hasira, na kwa kukemea kwa hasira-Mimi, Yahwe nimesema hivi!
So Jerusalem will become something for other people to condemn and to mock, a warning and a horror to the nations that surround you. I will execute judgments against you in wrath and fury, and with a furious rebuke—I, Yahweh have declared this!
16 Nitatuma mishale mikali ya njaa juu yenu ambayo itakuwa na maana ya kwamba nitawaharibu. Kwa kuwa nitaongeza njaa juu yenu na kuvunja tegemeo lenu la mkate.
I will send out harsh arrows of famine against you that will become the means with which I will destroy you. For I will increase the famine on you and break your staff of bread.
17 Nitaleta njaa na majanga dhidi yenu hivyo mtakuwa wagumba. Tauni na damu zitapita kati yako, na nitaleta upanga dhidi yenu-Mimi Yahwe, nimesema hivi.”
I will send a famine and disasters against you so you will be childless. Plague and blood will pass through you, and I will bring a sword against you—I, Yahweh, have declared this.”

< Ezekieli 5 >