< Ezekieli 46 >

1 Bwana Yahwe asema hivi: Lango la uzio wa ndani, linaloelekea mashariki, litafungwa kwa mda wa siku sita za kazi, lakini katika siku za Sabato litakuwa wazi, na katika siku ya mwezi mpya litafunguliwa.
Thus he says [the] Lord Yahweh [the] gate of the courtyard inner which faces east it will be shut [the] six [the] days of work and on [the] day of the sabbath it will be opened and on [the] day of the new moon it will be opened.
2 Mwana wa mfalme ataingia kwa kutumia lango la njia ya nyuma ya varanda upande wa nje, na atasimama mbele ya muhimili wa mwimo wa lango la ndani wakati makuhani wakiwa wakitengeza sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya amani. Kisha ataabudu kwenye kizingiti cha lango la ndani na kutoka nje, lakini lango halitakuwa linafungwa hadi jioni.
And he will go the prince [the] way of [the] porch of the gate from outside and he will stand at [the] doorpost of the gate and they will offer the priests burnt offering his and peace offerings his and he will bow down at [the] threshold of the gate and he will go out and the gate not it will be shut until the evening.
3 Watu wa nchi pia wataabudu mbele ya Yahwe kwenye hili lango la kuingilia katika siku ya Sabato na siku mpya za mwezi.
And they will bow down [the] people of the land [the] entrance of the gate that on the sabbaths and on the new moons before Yahweh.
4 Sadaka ya kuteketezwa ambayo mwana wa mfalme aitoayo kwa Yahwe katika siku ya Sabato itakuwa wanakondoo sita wasiokuwa na dosari na kondoo dume asiyekuwa na dosari.
And the burnt offering which he will bring near the prince to Yahweh on [the] day of the sabbath [will be] six lambs unblemished and a ram unblemished.
5 Sadaka ya unga pamoja na kondoo dume itakuwa efa moja, na sadaka ya unga pamoja na wanakondoo kiasi awezacho kutoa, na hini moja ya mafuta pamoja na kila efa ya unga.
And a grain offering [will be] an ephah for the ram and for the lambs a grain offering [will be] [the] gift of hand his and oil a hin to the ephah.
6 Katika siku ya mwezi mpya atatoa ng'ombe mchanga asiyekuwa na dosari kutoka kuchungwa, wanakondoo sita, na kondoo asyekuwa na dosari.
And on [the] day of the new moon a young bull a young one of cattle unblemished and six lambs and a ram unblemished they will be.
7 Atatengeneza sadaka ya unga ya efa moja kwa ajili ya ng'ombe na efa moja kwa ajili ya kondoo, na kwa kiasi awezacho kukitoa kwa ajili ya wanakondoo, na hini ya mafuta kwa kila efa ya unga.
And an ephah for the young bull and an ephah for the ram he will provide a grain offering and for the lambs just as it will reach hand his and oil a hin to the ephah.
8 Wakati mwana wa mfalme atakapokuwa anaingia kwa njia ya lango lenye varanda, ataondoka kwa njia hiyo hiyo.
And when comes the prince [the] way of [the] porch of the gate he will come and by way its he will go out.
9 Lakini wakati watu wa nchi watakakuja kwa Yahwe katika sikukuu zilizoteuliwa, kila mmoja kuingia kupitia kwenye lango la kaskazini kuabudu ataondoka kupitia lango la kusini; na kila atakayeingillia kupitia lango la kusini atatoka kupitia lango la kaskazini. Hakuna atakayerudia kwa lile lango aliloingilia, kwa kuwa atatoka nje moja kwa moja.
And when comes [the] people of the land before Yahweh at the appointed times the [one who] comes [the] way of [the] gate of [the] north to bow down he will go out [the] way of [the] gate of [the] south and the [one who] comes [the] way of [the] gate of [the] south he will go out [the] way of [the] gate north-ward not he will return [the] way of the gate which he came by it for opposite it (he will go out. *Q(K)*)
10 Mwana wa mfalme atakuwa kati yao; watakapoingia, ataingia ndani, na watakapoondoka, atatoka nao.
And the prince [will be] in midst of them when come they he will come and when go out they they will go out.
11 Kwenye sikukuu hizo, sadaka ya unga itakuwa efa moja ya unga kwa ng'ombe mmoja na efa moja kwa kondoo dume, na chochote atakacho kitoa pamoja na wanakondoo, na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
And at the festivals and at the appointed times it will be the grain offering an ephah for the young bull and an ephah for the ram and for the lambs [the] gift of hand his and oil a hin to the ephah.
12 Wakati mwana wa mfalme atakapotoa sadaka atakayojisikia kutoa, labda sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani kwa Yahwe, lango la kuelekea mashariki litafunguliwa kwa ajili yake. Atatoa sadaka yake ya kuteketezwa au sadaka ya amani kama afanyavyo siku ya Sabato. Kisha atatoka nje, na baada ya kutoka lango litafungwa.
And if he will provide the prince a freewill offering a burnt offering or peace offerings a freewill offering to Yahweh and someone will open for him the gate which faces east and he will offer burnt offering his and peace offerings his just as he will offer on [the] day of the sabbath and he will go out and someone will shut the gate after has gone out he.
13 Kwa kuongeza, utatoa mwanakondoo asiyekuwa na dosari mwenye umri wa mwaka mmoja kama sadaka ya kuteketezwa kwa Yahwe kila siku; utafanya hivi kila asubuhi.
And a lamb [the] son of year its unblemished you will offer a burnt offering to the day to Yahweh in the morning in the morning you will offer it.
14 Utatoa sadaka ya unga pamoja nayo kila asubuhi, efa sita na sehemu ya tatu ya hini ya mafuta kuchanganya na sadaka ya unga kwa ajili ya Yahwe, kulingana na sheria ilivyo.
And a grain offering you will offer with it in the morning in the morning sixth of ephah and oil third of hin to moisten the fine flour a grain offering to Yahweh statutes of perpetuity continually.
15 Watandaa mwanakondoo, sadaka ya kuteketezwa, na mafuta kila asubuhi, sadaka ya kuteketezwa ya kudumu.
(They will offer *Q(K)*) the lamb and the grain offering and the oil in the morning in the morning a burnt offering of continuity.
16 Bwana Yahwe asema hivi: Kama mwana wa mfalme akitoa zawadi kwa mmoja wa watoto wake, imekuwa urithi wake. Itakuwa mali ya mtoto wake, imekuwa urithi.
Thus he says [the] Lord Yahweh if he will give the prince a gift to anyone from sons his [will be] inheritance his it to sons his it will belong [will be] possession their it an inheritance.
17 Lakini kama akimpatia zawadi kutoka urithi wake kwa mmoja wa watumishi wake, kisha itakuwa ya huyo mtumishi mpaka mwaka wa uhuru, na kisha itarudi kwa mwana wa mfalme. Urithi wake yamkini ukawa kwa ajili ya watoto wake.
And if he will give a gift from inheritance his to one of servants his and it will belong to him until [the] year of liberty and it will return to the prince surely inheritance his sons his to them it will belong.
18 Mwana wa mfalme hatawaondolea urithi wa watu kutoka kwenye mali zao wenyewe; ataandaa kwa ajili ya watoto wake mali ili kwamba watu wangu wasitawanyike, kila mtu kutoka mali kwenye yake mwenyewe.”
And not he will take away the prince any of [the] inheritance of the people to oppress them from possession their some of own possession his he will cause to inherit sons his so that that not they will be scattered people my anyone from possession his.
19 Kisha yule mtu akaniletea kwenye lango la kutokea hata kwenye vyumba vitakatifu kwa ajili ya makuhani, vilivyokuwa vimeelekea kaskazini na tazama! Kulikuwa na sehemu mbele magharibi.
And he brought me in the entrance which [was] at [the] side of the gate to the rooms of holiness to the priests which were facing north-ward and there! [was] there a place (in the remotest parts *Q(K)*) west-ward.
20 Akanambia, “Hii ndio sehemu ambayo makuhani watakapo chemshia sadaka ya hatia na sadaka ya dhambi na walipookea sadaka ya unga. Wasilete sadaka nje ya uzio, kwa kuwa watu watatakaswa.”
And he said to me this [is] the place where they will boil there the priests the guilt offering and the sin offering where they will bake the grain offering to not to take [them] out into the courtyard outer to make holy the people.
21 Kisha akanileta kwenye uzio wa nje akaniongoza kuzunguka pembe nne za uzio, nikaona kwamba katika kila pembe ya uzio kulikuwa na uwanja.
And he brought out me into the courtyard outer and he made pass me to [the] four [the] corners of the courtyard and there! a courtyard [was] in [the] corner of the courtyard a courtyard [was] in [the] corner of the courtyard.
22 Katika hizo pembe nne za nje ya uzio kulikuwa na nzio nne ndogo, dhiraa arobaini urefu na thelathini upana. Ukubwa ule ule kwa nzio zote nne.
[were] in [the] four [the] corners of The courtyard courtyards enclosed [was] forty [cubits] [the] length and [was] thirty [cubits] [the] breadth measurement one [belonged] to [the] four of them set in corners.
23 Kulikuwa na safu zilizokuwa zimetengenezwa kwa mawe kuzizunguka zote nne, na meko ya kupikia ilikuwa chini ya safu ya jiwe.
And a row of stones [was] all around in them around to [the] four of them and boiling places [was] made under the rows of stones all around.
24 Yule mtu akanambia, “Hizi ndizo sehemu ambazo watumishi watachemshia dhabihu za watu.”
And he said to me these [are] [the] house of those [who] boil where they will boil there [those who] serve the house [the] sacrifice of the people.

< Ezekieli 46 >