< Ezekieli 45 >
1 Wakati mtakapogawanya nchi kama urithi, mtafanya sadakwa kwa Yahwe; sadaka hiyo itakuwa sehemu takatifu ya nchi, dhiraa elfu ishirini na tano urefu, na dhiraa elfu kumi upana. Patakuwa patakatifu, ndani ya mipaka yake yote.
Moreover, when ye shall divide by lot the land for inheritance, ye shall offer an oblation to Jehovah, a holy portion of the land; the length shall be five and twenty thousand reeds, and the breadth ten thousand. This shall be holy in all its borders round about.
2 Kutoka hapa kutakuwa na dhiraa mia tano kwa dhiraa mia tano za mraba kuzunguka mahali patakatifu, kwa kuuzunguka mpaka dhiraa hamsini upana.
And of this there shall be for the sanctuary five hundred in length and five hundred in breadth square round about; and fifty cubits round about for the suburbs thereof.
3 Kutoka hili eneo utapima fungu ambalo ni dhiraa elfu ishirini na tano urefu na elfu kumi upana; patakuwa patakatifu; mahali patakatifu palipo tukuka.
And of this measure shalt thou measure in length five and twenty thousand, and in breadth ten thousand; and in it shall be the sanctuary, the most holy place.
4 Patakuwa patakatifu katika nchi kwa ajili ya makuhani wanaomtumikia Yahwe, ajaye kwa Yahwe kumtumikia. Patakuwa mahali kwa ajili ya nyumba na eneo takatifu kwa ajili mahali patakatifu.
This is the holy portion of the land; it shall be for the priests, the ministers of the sanctuary, who come near to minister to Jehovah; and it shall be a place for their houses, and a holy place for the sanctuary.
5 Hivyo itakuwa dhiraa elfu ishirini na tano urefu na elfu kumi upana, patakuwa kwa ajili ya miji ya Walawi wanaotumika kwenye nyumba.
Five and twenty thousand in length, and ten thousand in breadth, shall the Levites, the ministers of the house, have for themselves for a possession, and twenty rooms.
6 Mtadhihirisha eneo moja kwa ajili ya mji, dhiraa elfu tano na urefu ishirini na tano, hapo patakuwa kando kando ya eneo lililohifadhiwa kwa ajili ya mahali patakatifu; huu mji utakuwa wa mali ya nyumba yote ya Israeli.
And ye shall appoint the possession of the city five thousand in breadth, and five and twenty thousand in length, over against the oblation of the holy portion; it shall be for all the house of Israel.
7 Nchi ya mwana mfalme itakuwa kwa pande zote za eneo lililohifadhiwa kwa ajili ya mahali patakatifu na mji. Patakuwa kwa upande wao wa magaharibi na upande wa mashariki. Urefu utalingana na urefu wa moja ya hayo mafungu, kutoka magaribi hata mashariki.
And a portion shall be for the prince on this side and on that side of the oblation of the holy portion and of the possession of the city, before the oblation of the holy portion and before the possession of the city, from the west side westward, and from the east side eastward; and the length shall be over against every one of the portions, from the west border to the east border.
8 Hii nchi itakuwa mali ya mwana mfalme katika Isaraeli. Wana wafalme hawatawakandamiza watu wangu; badala yake, watawapatia nchi kwa nyumba ya Israeli, kwa ajili ya makabila yao.
As for the land, it shall be to him a possession in Israel, that my princes may no more oppress my people, but give the rest of the land to the house of Israel according to their tribes.
9 Bwana Yahwe asema hivi: Inatosha kwa ajili yenu, mwana mfalme wa Israeli! Ondoa dhuluma na mgogoro; fanya hukumu na haki! Usiwafukuze wapangaji wa watu wangu! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
Thus saith the Lord Jehovah: Let it suffice you, O princes of Israel! Remove violence and spoil, and execute judgment and justice, and cease from your expulsions of my people, saith the Lord Jehovah.
10 Mtakuwa na mzani sahihi, efa sahihi, na bathi sahihi!
Ye shall have just balances, and a just ephah, and a just bath.
11 Efa na bathi zitakuwa kiasi kile kile, ili kwamba bathi iwe zaka ya homeri; efa itakuwa zaka ya hamori moja. Vipimo vyao vitakuwa vinafanana na homeri.
The ephah and the bath shall be of one measure; that the bath may contain the tenth part of a homer, and the ephah the tenth part of a homer; the measure thereof shall be according to the homer.
12 Shekeli zitakuwa gera ishirini, shekeli sita zitakuwa mane yenu.
And the shekel shall be twenty gerahs; twenty shekels, five and twenty shekels, and fifteen shekels shall be to you one maneh.
13 Hili ndilo toleo mtakalotoa: efa sita kwa kila homeri ya ngano, na mtatoa efa sita kwa kila homeri ya shayiri.
This is the heave-offering which ye shall offer: the sixth part of an ephah out of a homer of wheat, and the sixth part of an ephah out of a homer of barley.
14 Sadaka ya kawaida ya mafuta itakuwa zaka ya bathi kwa kila kori (ambazo ni bathi), au kwa kila hamori, kwa kuwa hamori moja ni bathi kumi pia.
And as for the statute concerning oil, the bath of oil, ye shall offer the tenth part of a bath out of a cor; a cor being ten baths; for a homer is ten baths.
15 Kondoo mmoja au mbuzi kutoka mifugo kwa kila wanyama mia mbili kutoka malisho ya maji ya mikoa ya Israeli yatatumika kwa sadaka ya kuteketezwa yoyote au sadaka ya amani kufanya upatanisho kwa ajili ya watu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
And ye shall offer one lamb out of the flock, out of two hundred, from the watered pastures of Israel, for the flour-offering and for the burnt-offering, and for the thank-offerings, to make reconciliation for them, saith the Lord Jehovah.
16 Watu wote wa nchi watatoa hii sadaka kwa mwana mfalme wa Israeli.
All the people of the land shall give this heave-offering for the prince in Israel.
17 Utakuwa wajibu wa mwana mfalme kutoa wanyama kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, sadaka ya unga, sadaka ya kinywaji, katika siku za sikukuu na sherehe za mwezi mpya, na katika siku za Sabato-sikukuu zote za kudumu za nyumba ya Israeli. Ataandaa kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za unga, sadaka za kuteketezwa, na sadaka za amani kwa ajili ya upatanisho badala ya nyumba ya Israeli.
And it shall be the duty of the prince to give burnt-offerings, and flour-offerings, and drink-offerings, in the feasts, and in the new moons, and in the sabbaths, and in all the solemn assemblies of the house of Israel; he shall present the sin-offering, and the flour-offering, and the burnt-offering, and the peace-offerings, to make reconciliation for the house of Israel.
18 Bwana Yahwe asema hivi: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, utachukua ng'ombe mmoja asiyekuwa na dosari kutoka kwenye kundi na kufanya sadaka ya dhambi kwa ajili ya patakatifu.
Thus saith the Lord Jehovah: In the first month, on the first day of the month, thou shalt take a young bullock without blemish, and shalt cleanse the sanctuary.
19 Kuhani atachukua baadhi ya damu ya sadaka ya dhambi na kuiweka juu ya miimo ya mlango na kwenye pembe nne za mpaka wa madhabahu, na miimo ya lango la uzio wa ndani.
And the priest shall take of the blood of the sin-offering, and put it upon the posts of the house, and upon the four corners of the ledge of the altar, and upon the posts of the gate of the inner court.
20 Utafanya hivyo siku ya saba ya mwezi kwa dhambi ya kila mtu kwa ajali au ujinga; katika njia hii mtaipatanisha hekalu.
And so shalt thou do on the seventh day for him that hath transgressed through error or simplicity; so shall ye make reconciliation for the house.
21 Katika siku ya mwezi siku ya kumi na nne ya mwezi, mtakuwa na sikukuu, sikukuu ya siku saba. Matakula makate usiotiwa chachu.
In the first month, on the fourteenth day of the month, ye shall have the passover, a feast of seven days; every one shall eat unleavened bread.
22 Siku hiyo, mwana mfalme ataandaa ng'ombe kwa ajili yake na kwa ajili ya watu wote wa nchi kama sadaka ya dhambi.
And upon that day shall the prince sacrifice for himself and for all the people of the land a bullock for a sin-offering.
23 Kwa siku saba za sikukuu, mwana wa mfalme ataandaa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Yahwe: ng'ombe saba na kondoo dume saba zisizokuwa na dosari kila siku kwa mda wa siku saba, na mbuzi dume kila siku kama sadaka ya dhambi.
And the seven days of the feast he shall sacrifice a burnt-offering to Jehovah, seven bullocks and seven rams without blemish daily the seven days; and a he-goat daily for a sin-offering.
24 Kisha mwana mfalme atatengeneza sadaka ya chakula ya efa moja kwa kila ng'ombe na efa moja kwa kila kondoo dume pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
And he shall present a flour-offering, an ephah for a bullock, and an ephah for a ram, and a hin of oil for an ephah.
25 Katika siku ya saba ya mwezi siku ya kumi na tano ya mwezi, katika sikukuu, mwana wa mfalme atafanya matoleo katika siku hizi saba: sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za chakula, na sadaka za mafuta.
In the seventh month, on the fifteenth day of the month, shall he do the like, in the feast, seven days, according to the sin-offering, and the burnt-offering, and the flour-offering, and the oil.