< Ezekieli 45 >

1 Wakati mtakapogawanya nchi kama urithi, mtafanya sadakwa kwa Yahwe; sadaka hiyo itakuwa sehemu takatifu ya nchi, dhiraa elfu ishirini na tano urefu, na dhiraa elfu kumi upana. Patakuwa patakatifu, ndani ya mipaka yake yote.
And when ye divide the land by lot for an inheritance, shall ye offer an oblation unto the Lord, as a holy portion of the land, five and twenty thousand rods in length, and in breadth ten thousand. This shall be holy in all its extent round about.
2 Kutoka hapa kutakuwa na dhiraa mia tano kwa dhiraa mia tano za mraba kuzunguka mahali patakatifu, kwa kuuzunguka mpaka dhiraa hamsini upana.
Of this there shall be for the sanctuary five hundred [rods] by five hundred, square round about; and fifty cubits as an open space for it round about.
3 Kutoka hili eneo utapima fungu ambalo ni dhiraa elfu ishirini na tano urefu na elfu kumi upana; patakuwa patakatifu; mahali patakatifu palipo tukuka.
And of this measure shalt thou measure, in length five and twenty thousand, and in breadth ten thousand [rods]: and in it shall be the sanctuary [and] the holy of holies.
4 Patakuwa patakatifu katika nchi kwa ajili ya makuhani wanaomtumikia Yahwe, ajaye kwa Yahwe kumtumikia. Patakuwa mahali kwa ajili ya nyumba na eneo takatifu kwa ajili mahali patakatifu.
The holy portion of the land shall it be, for the priests the ministers of the sanctuary shall it be, who come near to minister unto the Lord; and it shall be unto them a place for houses, and a holy place for the sanctuary.
5 Hivyo itakuwa dhiraa elfu ishirini na tano urefu na elfu kumi upana, patakuwa kwa ajili ya miji ya Walawi wanaotumika kwenye nyumba.
And five and twenty thousand [rods] in length, and ten thousand in breadth, shall also belong unto the Levites, the servants of the house, for themselves, as a possession, with twenty chambers.
6 Mtadhihirisha eneo moja kwa ajili ya mji, dhiraa elfu tano na urefu ishirini na tano, hapo patakuwa kando kando ya eneo lililohifadhiwa kwa ajili ya mahali patakatifu; huu mji utakuwa wa mali ya nyumba yote ya Israeli.
And as the possession of the city shall ye assign five thousand rods broad, and five and twenty thousand long, alongside the holy oblation: unto the whole house of Israel shall it belong.
7 Nchi ya mwana mfalme itakuwa kwa pande zote za eneo lililohifadhiwa kwa ajili ya mahali patakatifu na mji. Patakuwa kwa upande wao wa magaharibi na upande wa mashariki. Urefu utalingana na urefu wa moja ya hayo mafungu, kutoka magaribi hata mashariki.
And the prince shall have that on the one side and on the other side of the holy oblation, and of the possession of the city, in front of the holy oblation, and in front of the possession of the city, on the west side westward, and on the east side eastward; and in length alongside one of the portions, both on the west border and on the east border.
8 Hii nchi itakuwa mali ya mwana mfalme katika Isaraeli. Wana wafalme hawatawakandamiza watu wangu; badala yake, watawapatia nchi kwa nyumba ya Israeli, kwa ajili ya makabila yao.
As landed property shall it be his possession in Israel: and my princes shall no more wrong my people; but the land shall they give to the house of Israel according to their tribes.
9 Bwana Yahwe asema hivi: Inatosha kwa ajili yenu, mwana mfalme wa Israeli! Ondoa dhuluma na mgogoro; fanya hukumu na haki! Usiwafukuze wapangaji wa watu wangu! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
Thus hath said the Lord Eternal, Ye have done enough wrong, O princes of Israel: remove violence and robbery, and execute justice and righteousness; take away your exactions from my people, saith the Lord Eternal.
10 Mtakuwa na mzani sahihi, efa sahihi, na bathi sahihi!
Just balances, and a just ephah, and a just bath shall ye have.
11 Efa na bathi zitakuwa kiasi kile kile, ili kwamba bathi iwe zaka ya homeri; efa itakuwa zaka ya hamori moja. Vipimo vyao vitakuwa vinafanana na homeri.
The ephah and the bath shall contain the same quantity, that the bath may contain the tenth part of a chomer, and the ephah the tenth part of a chomer: after the chomer shall the measure of contents be.
12 Shekeli zitakuwa gera ishirini, shekeli sita zitakuwa mane yenu.
And the shekel shall be twenty gerahs: [in pieces of] twenty shekels, five and twenty shekels, fifteen shekels, shall be your maneh.
13 Hili ndilo toleo mtakalotoa: efa sita kwa kila homeri ya ngano, na mtatoa efa sita kwa kila homeri ya shayiri.
This is the heave-offering that ye shall offer; The sixth part of an ephah of a chomer of wheat; and ye shall give the sixth part of an ephah of a chomer of barley;
14 Sadaka ya kawaida ya mafuta itakuwa zaka ya bathi kwa kila kori (ambazo ni bathi), au kwa kila hamori, kwa kuwa hamori moja ni bathi kumi pia.
And the fixed portion of oil shall be after the bath of oil, the tenth part of a bath out of the cor, ten baths reckoned to the chomer; for ten baths are a chomer;
15 Kondoo mmoja au mbuzi kutoka mifugo kwa kila wanyama mia mbili kutoka malisho ya maji ya mikoa ya Israeli yatatumika kwa sadaka ya kuteketezwa yoyote au sadaka ya amani kufanya upatanisho kwa ajili ya watu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
And one lamb out of the flock, out of two hundred, out of the fat pastures of Israel, for meat-offerings, and for burnt-offerings, and for peace-offerings, to make an atonement for them, saith the Lord Eternal.
16 Watu wote wa nchi watatoa hii sadaka kwa mwana mfalme wa Israeli.
All the people of the land shall be held bound for this heave-offering for the prince in Israel.
17 Utakuwa wajibu wa mwana mfalme kutoa wanyama kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, sadaka ya unga, sadaka ya kinywaji, katika siku za sikukuu na sherehe za mwezi mpya, na katika siku za Sabato-sikukuu zote za kudumu za nyumba ya Israeli. Ataandaa kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za unga, sadaka za kuteketezwa, na sadaka za amani kwa ajili ya upatanisho badala ya nyumba ya Israeli.
And upon the prince shall be the duty to furnish the burnt-offerings, the meat-offerings, and the drink-offerings, on the feasts, and on the new-moon days, and on the sabbaths, on all the festive seasons of the house of Israel: he himself shall prepare the sin-offering, and the meat-offering, and the burnt-offering, and the peace-offerings, to make an atonement in behalf of the house of Israel.
18 Bwana Yahwe asema hivi: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, utachukua ng'ombe mmoja asiyekuwa na dosari kutoka kwenye kundi na kufanya sadaka ya dhambi kwa ajili ya patakatifu.
Thus hath said the Lord Eternal, In the first month, on the first of the month, shalt thou take a young bullock without blemish, and make an expiation for the sanctuary.
19 Kuhani atachukua baadhi ya damu ya sadaka ya dhambi na kuiweka juu ya miimo ya mlango na kwenye pembe nne za mpaka wa madhabahu, na miimo ya lango la uzio wa ndani.
And the priest shall take some of the blood of the sin-offering, and put it upon the door-post of the house, and upon the four corners of the projection of the altar, and upon the door-post of the gate of the inner court.
20 Utafanya hivyo siku ya saba ya mwezi kwa dhambi ya kila mtu kwa ajali au ujinga; katika njia hii mtaipatanisha hekalu.
And so shalt thou do on the seventh day of the month for every one that erreth, and for him that hath sinned unawares; so shall ye atone for the house.
21 Katika siku ya mwezi siku ya kumi na nne ya mwezi, mtakuwa na sikukuu, sikukuu ya siku saba. Matakula makate usiotiwa chachu.
In the first month, on the fourteenth day of the month, shall ye have the passover: a feast of seven days; unleavened bread shall be eaten.
22 Siku hiyo, mwana mfalme ataandaa ng'ombe kwa ajili yake na kwa ajili ya watu wote wa nchi kama sadaka ya dhambi.
And the prince shall prepare on that day in behalf of himself and in behalf of all the people of the land a bullock for a sin-offering.
23 Kwa siku saba za sikukuu, mwana wa mfalme ataandaa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Yahwe: ng'ombe saba na kondoo dume saba zisizokuwa na dosari kila siku kwa mda wa siku saba, na mbuzi dume kila siku kama sadaka ya dhambi.
And on the seven days of the feast shall he prepare a burnt-offering to the Lord, seven bullocks and seven rams without blemish on every day of the seven days; and for a sin-offering a he-goat on every day.
24 Kisha mwana mfalme atatengeneza sadaka ya chakula ya efa moja kwa kila ng'ombe na efa moja kwa kila kondoo dume pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
And as a meat-offering an ephah for a bullock, and an ephah for a ram shall he prepare, and a hin of oil for each ephah.
25 Katika siku ya saba ya mwezi siku ya kumi na tano ya mwezi, katika sikukuu, mwana wa mfalme atafanya matoleo katika siku hizi saba: sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za chakula, na sadaka za mafuta.
In the seventh month, on the fifteenth day of the month, on the feast, shall he prepare the like during the seven days, both the sin-offering, as also the burnt-offering, and the meat-offering, and the oil.

< Ezekieli 45 >