< Ezekieli 40 >

1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa kuhamishwa kwetu mwanzoni mwa mwaka siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya mji kuchukuliwa-katika siku hiyo hiyo, mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu na alinichukua huko.
En el año veinticinco de nuestro cautiverio, al principio del año, en el día diez del mes, en el año catorce después de que la ciudad fue golpeada, en el mismo día, la mano de Yahvé estuvo sobre mí, y me llevó allí.
2 Katika maono ya Mungu akanileta hata nchi ya Israeli. Akanileta kupumzika juu ya kila mlima mrefu sana; upande wa kusini kulikuwa na monekano kana kwamba majengo ya mji.
En las visiones de Dios me llevó a la tierra de Israel, y me puso en un monte muy alto, en el que había algo parecido a la estructura de una ciudad al sur.
3 Kisha akanileta huko. Tazama, kulikuwa na mtu! Mwonekano wake ulikuwa kama mwonekano wa shaba. Alikuwa na uzi wa kitani na mwanzi wa kupimia mkononi mwake, na alisimama katika lango la mji.
Me llevó allí, y he aquí que había un hombre cuyo aspecto era semejante al del bronce, con un cordel de lino en la mano y una caña de medir; y estaba en la puerta.
4 Huyo mtu akanambia, “Mwanadamu, tazama kwa macho yako na sikiliza kwa masikio yako, na elekeza moyo wako juu ya yote ninayokufunulia, kwa kuwa ulinileta hapa ili niweze kukufunulia haya wewe. Toa taarifa ya kila kitu utakachokiona kwa nyumba ya Israeli.
El hombre me dijo: “Hijo de hombre, mira con tus ojos y escucha con tus oídos, y pon tu corazón en todo lo que te voy a mostrar; porque has sido traído aquí para que te lo muestre. Anuncia todo lo que veas a la casa de Israel”.
5 Kulikuwa ukuta uliokuwa umezunguka eneo la hekalu. Urefu wa kipimo cha mwanzi katika mkono wa mtu ulikuwa dhiraa sita urefu, kila urefu wa dhiraa ulikuwa dhiraa moja na kipimo cha kiganja cha mkono urefu. Aliupima ukuta; ulikuwa kipimo cha mwanzi mmoja na ufito mmoja urefu.
He aquí que había un muro en la parte exterior de la casa por todo el contorno, y en la mano del hombre una caña de medir de seis codos, de un codo y un palmo de ancho cada una. Así midió el grosor del edificio, una caña; y la altura, una caña.
6 Kisha akaenda hata kwenye lango la hekalu lililokuwa limeelekea mashariki. Akapanda ngazi na kuipima kizingiti cha lango-mwanzi mmoja upana.
Luego llegó a la puerta que mira hacia el oriente, y subió sus escalones. Midió el umbral de la puerta, de una caña de ancho, y el otro umbral, de una caña de ancho.
7 Vyumba vya ulinzi vilikuwa kila mwanzi mmoja urefu na mwanzi mmoja upana; kulikuwa na dhiraa tano katika kila vyumba viwili, na kizingiti cha lango la hekalu karibu na tawa la hekalu kilikuwa mwanzi mmoja urefu.
Cada posada tenía una caña de largo y otra de ancho. Entre las logias había cinco codos. El umbral de la puerta, junto al pórtico de la puerta hacia la casa, era de una caña.
8 Akapima tawa la lango; ulikuwa mwanzi mmoja urefu.
Midió también el pórtico de la puerta hacia la casa, una caña.
9 Akapima tawa la lango. Ilikuwa mwanzi mmoja kwenda chini. Mihimili ilikuwa dhiraa mbili upana. Hili lilikuwa tawa la lango kuelekea hekalu.
Luego midió el pórtico de la puerta, de ocho codos, y sus postes, de dos codos; y el pórtico de la puerta estaba hacia la casa.
10 Kulikuwa na vyumba vitatu vya ulinzi pande zote za lango la mashariki, na yote yalikuwa na kipimo kile kile, na kuta zilizokuwa zimezigawanya zilikuwa na kipimo kile kile.
Los cuartos laterales de la puerta hacia el este eran tres de un lado y tres de otro. Los tres eran de una sola medida. Los postes tenían una sola medida de este lado y del otro.
11 Kisha yule mtu akapima upana wa njia ya lango la kuingia-dhiraa kumi; na akapima urefu wa njia ya lango la kuingia-dhiraa kumi na tatu.
Midió la anchura de la abertura de la puerta, diez codos; y la longitud de la puerta, trece codos;
12 Akaupima ukuta uliokuwa mpaka mbele ya vyumba-dhiraa moja urefu. Vyumba vilipimwa dhiraa sita kila upande.
y un borde delante de las logias, un codo de este lado, y un borde, un codo de aquel lado; y las habitaciones laterales, seis codos de este lado, y seis codos de aquel lado.
13 Kisha akapima lango la njia kutoka kwenye paa ya chumba kimoja kuelekea chumba kingine-dhiraa ishirini na tano, kutoka lango la kuingia chumba cha kwanza kuelekea kile cha pili.
Midió la puerta desde el techo de una habitación lateral hasta el techo de la otra, un ancho de veinticinco codos, puerta contra puerta.
14 Kisha akapima ukuta uliokuwa umeenda kati ya vyumba vya ulinzi-dhiraa sitini urefu; alipima kwa mbali na tawa la lango.
También hizo postes de sesenta codos, y el patio llegaba hasta los postes, alrededor de la puerta.
15 Lango la kuingia kutoka lango la mbele kuelekea lango jingine la tawa la mwisho lilikuwa dhiraa hamsini.
Desde el frente de la puerta de entrada hasta el frente del pórtico interior de la puerta había cincuenta codos.
16 Kulikuwa na madirisha yaliyokuwa yamefungwa kuelekea vyumba na kuelekea nguzo zake kati ya malango kuzunguka kote; na vivyo hivyo kwa mabaraza. Kulikuwa na madirisha pande zote za ndani, na kila mhimili ulikuwa umepambwa kwa mitende.
Había ventanas cerradas en las salas laterales y en sus postes dentro de la puerta, alrededor, y también en los arcos. Las ventanas estaban alrededor hacia adentro. En cada poste había palmeras.
17 Kisha huyo mtu akanileta hata ua wa nje mwa hekalu. Tazama, kulikuwa na vyumba, na kulikuwa na kibamba katika ua, pamoja na vyumba thelathini baada ya kibamba.
Entonces me llevó al atrio exterior. He aquí que había habitaciones y un pavimento hecho para el patio alrededor. En el pavimento había treinta habitaciones.
18 Kibamba kilienda juu hata upande wa malango, na upana wake ulikuwa sawsawa na urefu wa malango. Hiki kilikuwa kibamba cha chini.
El pavimento estaba al lado de las puertas, y correspondía a la longitud de las puertas, hasta el pavimento inferior.
19 Kisha huyo mtu akapima umbali kutoka mebele ya lango la chini hata mbele ya lango la ndani; ilikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki, na sawasawa na upande wa kaskazini.
Luego midió la anchura desde el frente de la puerta inferior hasta el frente del atrio interior exterior, cien codos, tanto al este como al norte.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango lililokuwa upande wa kaskazini mwa ua wa nje.
Midió la longitud y la anchura de la puerta del atrio exterior que da al norte.
21 Kulikuwa na vyumba vitatu pande zote za lango, na lango na matawa yake yalipimwa sawa na lango kubwa-dhiraa hamsini upana wote na dhiraa ishirini na tano upana.
Las puertas de esta puerta eran tres de un lado y tres de otro. Sus postes y sus arcos eran iguales a la medida de la primera puerta: su longitud era de cincuenta codos, y la anchura de veinticinco codos.
22 Madirisha yake, tawa, vyumba, na mitende yake vilikabiliana na lango ambalo linaloelekea mashariki. Ngazi saba kuupandia juu hata kwenye tawa lake.
Sus ventanas, sus arcos y sus palmeras tenían la misma medida que la puerta que da al oriente. Subieron a ella por siete escalones. Sus arcos estaban delante de ellos.
23 Kulikuwa na lango kwenye ua wa ndani mbele kuelekea mashariki; huyo mtu alipima kutoka lango moja hadi lango jingine-dhiraa mia moja umbali.
Había una puerta del patio interior que daba a la otra puerta, al norte y al este. Medía cien codos de puerta a puerta.
24 Kisha huyo mtu akanileta hata kwenye lango la kuingia la kusini, na kuta zake na tawa vilipimwa sawa kama malango mengine ya nje.
Me condujo hacia el sur; y he aquí que había una puerta hacia el sur. Midió sus postes y sus arcos según estas medidas.
25 Kulikuwa na madirisha yaliyofungwa katika lango la njia na tawa lake kama lile lango. Lango la kusini na tawa lake vilipimwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
Había ventanas en ella y en sus arcos alrededor, como las otras ventanas: la longitud era de cincuenta codos, y la anchura de veinticinco codos.
26 Kulikuwa na ngazi saba hadi kwenye lango na matawa yake, na kulikuwa na mitende iliyochongoka juu ya kuta pande zote.
Había siete escalones para subir a ella, y sus arcos estaban delante de ellos. Tenía palmeras, una de un lado y otra de otro, en sus postes.
27 Kulikuwa na lango la ua wa ndani upande wa kusini, na yule mtu akapima kutoka hilo lango hata lango la kuingia upande wa kusini-dhiraa mia moja umbali.
Había una puerta que daba al patio interior hacia el sur. Medía cien codos de puerta a puerta hacia el sur.
28 Kishi huyo mtu akanileta hata ua wa ndani karibu na lango lake la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo vile vile kama malango mengine.
Luego me llevó al patio interior, junto a la puerta sur. Midió la puerta sur de acuerdo con estas medidas;
29 Vyumba vyake, kuta, na matao vilipimwa sawa kama malango mengine; kulikuwa na madirisha kuzunguka matao yote. Lango la ndani na matao yake yalipimwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
con sus alojamientos, sus postes y sus arcos, de acuerdo con estas medidas. Había ventanas en ella y en sus arcos alrededor. Tenía cincuenta codos de largo y veinticinco de ancho.
30 Pia kulikuwa na matao pande zote za kuta za ndani; haya yalikuwa dhiraa ishirini na tano urefu na dhiraa tano upana.
Había arcos alrededor, de veinticinco codos de largo y cinco de ancho.
31 Hili tawa lilielekea ua wa nje pamoja na mitende iliyochongwa juu ya kuta zake na ngazi nane kuupandia.
Sus arcos estaban orientados hacia el atrio exterior. En sus postes había palmeras. La subida a él tenía ocho escalones.
32 Kisha yule mtu akanileta hata kwenye ua wa ndani karibu na njia ya kaskazini na kulipima lango, ambalo lilikuwa na vipimo sawa kama malango mengine.
Me llevó al patio interior, hacia el este. Midió la puerta de acuerdo con estas medidas;
33 Vyumba vyake, kuta, na matawa yalikuwa na kipima sawa kama cha malango, na kulikuwa na madirisha pande zote. Laango la ndani na matawa yake yalikuwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
con sus alojamientos, sus postes y sus arcos, de acuerdo con estas medidas. Había ventanas en ella y en sus arcos alrededor. Tenía cincuenta codos de largo y veinticinco de ancho.
34 Matawa yake yalielekea nje ya ua; ilikuwa na mitende pande zote za hiyo na ngazi nane za kuupandia.
Sus arcos estaban orientados hacia el atrio exterior. En sus postes había palmeras de un lado y del otro. La subida a él tenía ocho escalones.
35 Kisha huyo mtu akanileta hata lango la kaskazini na kulipima; likapimwa vivyo hivyo kama malango mengine.
Me llevó a la puerta del norte, y la midió según estas medidas:
36 Vyumba vyake, kuta, na ukumbi vilipimwa sawa na malango mengine, na kulikuwa na madirisha pande zote. Njia ya lango na matao yake yalipimwa dhiraa hamsini urefu na upana dhiraa ishirini na tano.
sus alojamientos, sus postes y sus arcos. Había en ella ventanas por todas partes. Su longitud era de cincuenta codos y su anchura de veinticinco codos.
37 Tatawa lake lilielekea ua wa nje; ilikuwa na mitende pande zote za huo na ngazi nane kuupandia.
Sus postes estaban orientados hacia el atrio exterior. En sus postes había palmeras de un lado y del otro. La subida a ella tenía ocho escalones.
38 Kulikuwa na chumba pamoja na mlango karibu na kila lango la ndani. Hapa ndipo ambako walipooshea sadaka za kutekezwa.
Junto a los postes de las puertas había una sala con su puerta. Allí lavaban el holocausto.
39 Kulikuwa na meza mbili kila upande wa kila ukumbi, ambako sadaka ya kuteketezwa ilipochinjiwa, na pia sadaka ya dhambi na sadaka ya hatia.
En el pórtico de la puerta había dos mesas a un lado y dos mesas a otro, en las que se mataba el holocausto, el sacrificio por el pecado y la ofrenda por la culpa.
40 Karibu na ukuta wa ua, kuelekea juu kwenye lango kuelekea kaskazini, kulikuwa na meza mbili. Pia kwa upande mwingine kulikuwa na meza mbili kwenye lango la ukumbi.
A un lado, afuera, cuando se sube a la entrada de la puerta hacia el norte, había dos mesas; y al otro lado, que pertenecía al pórtico de la puerta, había dos mesas.
41 Kulikuwa na meza nne pande zote karibu na lango; wakachinja wanyama juu ya meza nane.
De este lado había cuatro mesas, y del otro lado, al lado de la puerta, cuatro mesas en las que se mataban los sacrificios.
42 Kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, dhiraa moja na nusu urefu, dhiraa moja na nusu upana, na kimo dhiraa moja. Juu yake waliweka vyombo pamoja ambavyo walivichinjia sadaka za kuteketezwa kwa ajili ya sadaka.
Había cuatro mesas de piedra cortada para el holocausto, de un codo y medio de largo, un codo y medio de ancho y un codo de alto. Sobre ellas ponían los instrumentos con los que mataban el holocausto y el sacrificio.
43 Kulabu mbili ujazo wa kiganja urefu uliokuwa umeunganishwa katika ua pande zote, na nyama ya matoleo ilikuwa imewekwa juu ya meza.
Los garfios, de un palmo de largo, estaban fijados dentro de todo el contorno. La carne de la ofrenda estaba sobre las mesas.
44 Karibu na lango la ndani, katika ua wa ndani, kulikuwa na vyumba vya waimbaji. Moja ya hivi vyumba kilikuwa upande wa kaskazini, na kingine kusini.
Fuera de la puerta interior había habitaciones para los cantantes en el patio interior, que estaba al lado de la puerta norte. Estaban orientadas hacia el sur. La otra, al lado de la puerta oriental, daba hacia el norte.
45 Kisha yule mtu akanambia, “Hiki chumba kinachoelekea kusini ni kwa ajili ya makuhani walio zamu katika hekalu.
Me dijo: “Esta habitación, que da hacia el sur, es para los sacerdotes que cumplen con el deber de la casa.
46 Chumba kilichoelekea kaskazini kilikuwa kwa ajili ya makuhani waliokuwa zamu kwenye madhabahu. Hawa ni wana wa Sadoki ambaye huja humkaribia Yahwe kumtumikia; ambao ni miongoni mwa wana wa Lawi.”
La sala que da hacia el norte es para los sacerdotes que cumplen la función del altar. Estos son los hijos de Sadoc, que de entre los hijos de Leví se acercan a Yahvé para servirle”.
47 Kisha akaupima ule ua-dhiraa mia moja urefu na dhiraa mia moja upana mraba, pamoja na madhabahu mbele ya nyumba.
Midió el atrio, de cien codos de largo y cien de ancho, en forma cuadrada. El altar estaba delante de la casa.
48 Kisha yule mtu akanileta hata kwenye varanda ya nyumba na kupima mwimo wa milango yake-ilikuwa dhiraa tano unene upande huu. Njia ya kuingilia yenyewe ilikuwa dhiraa kumi na nne, na kuta pande zote za huo zilikuwa dhraa tatu upana.
Luego me llevó al pórtico de la casa, y midió cada poste del pórtico, cinco codos de un lado y cinco codos del otro. La anchura del pórtico era de tres codos de un lado y de tres codos de otro.
49 Urefu wa ukumbi ulikuwa dhiraa ishirini, na upana wake ulikuwa dhiraa kumi na moja. Kulikuwa na ngazi zilizokuwa zimepanda juu na nguzo zilizokuwa zimesimama pande zote za huo.
La longitud del pórtico era de veinte codos y la anchura de once codos, incluso por los escalones por los que se subía a él. Había pilares junto a los postes, uno de este lado y otro del otro.

< Ezekieli 40 >