< Ezekieli 40 >

1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa kuhamishwa kwetu mwanzoni mwa mwaka siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya mji kuchukuliwa-katika siku hiyo hiyo, mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu na alinichukua huko.
Двадесет пете године робовања нашег, у почетку године, десети дан месеца, четрнаесте године од како се узе град, исти дан дође нада ме рука Господња и одведе ме онамо.
2 Katika maono ya Mungu akanileta hata nchi ya Israeli. Akanileta kupumzika juu ya kila mlima mrefu sana; upande wa kusini kulikuwa na monekano kana kwamba majengo ya mji.
Утварама Божјим одведе ме у земљу Израиљеву, и постави ме на гору врло високу, на којој беше с југа као саграђен град.
3 Kisha akanileta huko. Tazama, kulikuwa na mtu! Mwonekano wake ulikuwa kama mwonekano wa shaba. Alikuwa na uzi wa kitani na mwanzi wa kupimia mkononi mwake, na alisimama katika lango la mji.
И одведе ме онамо, и гле, човек, који на очи беше као од бронзе, с ужем ланеним у руци и с трском мерачком, и стајаше на вратима.
4 Huyo mtu akanambia, “Mwanadamu, tazama kwa macho yako na sikiliza kwa masikio yako, na elekeza moyo wako juu ya yote ninayokufunulia, kwa kuwa ulinileta hapa ili niweze kukufunulia haya wewe. Toa taarifa ya kila kitu utakachokiona kwa nyumba ya Israeli.
И проговори ми тај човек: Сине човечји, гледај очима својим и слушај ушима својим, и узми на ум све што ћу ти показати, јер си доведен овамо да ти покажем; кажи дому Израиљевом све што видиш.
5 Kulikuwa ukuta uliokuwa umezunguka eneo la hekalu. Urefu wa kipimo cha mwanzi katika mkono wa mtu ulikuwa dhiraa sita urefu, kila urefu wa dhiraa ulikuwa dhiraa moja na kipimo cha kiganja cha mkono urefu. Aliupima ukuta; ulikuwa kipimo cha mwanzi mmoja na ufito mmoja urefu.
И гле, беше зид споља око дома, а у руци оном човеку трска мерачка од шест лаката, а лакат беше с подланице дужи од обичног; и измери грађевину у ширину, и беше једна трска, и у висину, и беше једна трска.
6 Kisha akaenda hata kwenye lango la hekalu lililokuwa limeelekea mashariki. Akapanda ngazi na kuipima kizingiti cha lango-mwanzi mmoja upana.
Па дође на врата која беху према истоку, и изиђе уз басамаке, и измери један праг вратима, и беше у ширину једна трска, и други праг, и беше у ширину једна трска;
7 Vyumba vya ulinzi vilikuwa kila mwanzi mmoja urefu na mwanzi mmoja upana; kulikuwa na dhiraa tano katika kila vyumba viwili, na kizingiti cha lango la hekalu karibu na tawa la hekalu kilikuwa mwanzi mmoja urefu.
И клети, и свака беше једну трску дуга и једну трску широка; а између клети беше пет лаката; и праг на вратима код трема на унутрашњим вратима, и беше с једне трске.
8 Akapima tawa la lango; ulikuwa mwanzi mmoja urefu.
И измери трем на вратима унутрашњим, и беше једна трска.
9 Akapima tawa la lango. Ilikuwa mwanzi mmoja kwenda chini. Mihimili ilikuwa dhiraa mbili upana. Hili lilikuwa tawa la lango kuelekea hekalu.
И измери трем на вратима, и беше осам лаката; и довратнике им, и беху два лакта; а трем на вратима беше изнутра;
10 Kulikuwa na vyumba vitatu vya ulinzi pande zote za lango la mashariki, na yote yalikuwa na kipimo kile kile, na kuta zilizokuwa zimezigawanya zilikuwa na kipimo kile kile.
И клети код врата према истоку беху три амо и три тамо, једне мере све три, и једне мере беху довратници тамо и амо.
11 Kisha yule mtu akapima upana wa njia ya lango la kuingia-dhiraa kumi; na akapima urefu wa njia ya lango la kuingia-dhiraa kumi na tatu.
И измери ширину вратима, и беше десет лаката, и тринаест лаката беше у дужину вратима.
12 Akaupima ukuta uliokuwa mpaka mbele ya vyumba-dhiraa moja urefu. Vyumba vilipimwa dhiraa sita kila upande.
И пред клетима беше места један лакат, и за један лакат беше места с друге стране, и у свакој клети беше шест лаката од туда и шест лаката од овуда.
13 Kisha akapima lango la njia kutoka kwenye paa ya chumba kimoja kuelekea chumba kingine-dhiraa ishirini na tano, kutoka lango la kuingia chumba cha kwanza kuelekea kile cha pili.
После измери врата од крова једне клети до крова друге, и беше у ширину двадесет и пет лаката, врата према вратима.
14 Kisha akapima ukuta uliokuwa umeenda kati ya vyumba vya ulinzi-dhiraa sitini urefu; alipima kwa mbali na tawa la lango.
И начини довратнике од шездесет лаката, и пред довратницима трем на вратима унаоколо.
15 Lango la kuingia kutoka lango la mbele kuelekea lango jingine la tawa la mwisho lilikuwa dhiraa hamsini.
И од лица врата на која се улази до лица трема на унутрашњим вратима беше педесет лаката.
16 Kulikuwa na madirisha yaliyokuwa yamefungwa kuelekea vyumba na kuelekea nguzo zake kati ya malango kuzunguka kote; na vivyo hivyo kwa mabaraza. Kulikuwa na madirisha pande zote za ndani, na kila mhimili ulikuwa umepambwa kwa mitende.
И беху прозори на клетима и на довратницима њиховим сужени унутра око врата, тако и на тремовима, прозори беху изнутра свуда унаоколо, и по довратницима палме.
17 Kisha huyo mtu akanileta hata ua wa nje mwa hekalu. Tazama, kulikuwa na vyumba, na kulikuwa na kibamba katika ua, pamoja na vyumba thelathini baada ya kibamba.
Потом ме уведе у спољашњи трем, и гле, беху клети и под начињен свуда унаоколо у трему, тридесет клети на поду.
18 Kibamba kilienda juu hata upande wa malango, na upana wake ulikuwa sawsawa na urefu wa malango. Hiki kilikuwa kibamba cha chini.
А тај под покрај врата према дужини врата беше нижи под.
19 Kisha huyo mtu akapima umbali kutoka mebele ya lango la chini hata mbele ya lango la ndani; ilikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki, na sawasawa na upande wa kaskazini.
Потом измери ширину од лица доњих врата до лица унутрашњег трема споља, и беше сто лаката к истоку и северу.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango lililokuwa upande wa kaskazini mwa ua wa nje.
И врата која беху к северу на трему спољашњем измери у дужину и у ширину;
21 Kulikuwa na vyumba vitatu pande zote za lango, na lango na matawa yake yalipimwa sawa na lango kubwa-dhiraa hamsini upana wote na dhiraa ishirini na tano upana.
И беху три клети тамо и три амо, и довратници им и тремови беху исте мере као у првих врата; педесет лаката беше у дужину а у ширину двадесет и пет лаката;
22 Madirisha yake, tawa, vyumba, na mitende yake vilikabiliana na lango ambalo linaloelekea mashariki. Ngazi saba kuupandia juu hata kwenye tawa lake.
И прозори им и тремови и палме беху на меру као на вратима која гледају на исток, и иђаше се к њима уза седам басамака, и тремови беху пред њима.
23 Kulikuwa na lango kwenye ua wa ndani mbele kuelekea mashariki; huyo mtu alipima kutoka lango moja hadi lango jingine-dhiraa mia moja umbali.
И врата од унутрашњег трема беху према вратима северним и источним, и измери од врата до врата, и беше сто лаката.
24 Kisha huyo mtu akanileta hata kwenye lango la kuingia la kusini, na kuta zake na tawa vilipimwa sawa kama malango mengine ya nje.
После ме одведе к југу, и гле, беху врата према југу; и измери им довратнике и тремове, и беше иста мера.
25 Kulikuwa na madirisha yaliyofungwa katika lango la njia na tawa lake kama lile lango. Lango la kusini na tawa lake vilipimwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
И беху прозори на њима и на тремовима њиховим унаоколо као они прозори; педесет лаката беше у дужину и двадесет и пет лаката у ширину.
26 Kulikuwa na ngazi saba hadi kwenye lango na matawa yake, na kulikuwa na mitende iliyochongoka juu ya kuta pande zote.
И иђаше се к њима уза седам басамака, и тремови беху пред њима, и палме једна од туда, а једна од овуда по довратницима.
27 Kulikuwa na lango la ua wa ndani upande wa kusini, na yule mtu akapima kutoka hilo lango hata lango la kuingia upande wa kusini-dhiraa mia moja umbali.
И врата од унутрашњег трема беху према југу; и измери од врата до врата к југу, и беше сто лаката.
28 Kishi huyo mtu akanileta hata ua wa ndani karibu na lango lake la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo vile vile kama malango mengine.
Тада ме уведе у унутрашњи трем јужним вратима; и измери јужна врата, и беше иста мера.
29 Vyumba vyake, kuta, na matao vilipimwa sawa kama malango mengine; kulikuwa na madirisha kuzunguka matao yote. Lango la ndani na matao yake yalipimwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
И клети њихове и довратници и тремови беху исте мере, и прозори на њима и на тремовима унаоколо; педесет лаката беше у дужину, и двадесет и пет лаката у ширину.
30 Pia kulikuwa na matao pande zote za kuta za ndani; haya yalikuwa dhiraa ishirini na tano urefu na dhiraa tano upana.
И тремови беху унаоколо, двадесет и пет лаката у дужину и пет лаката у ширину.
31 Hili tawa lilielekea ua wa nje pamoja na mitende iliyochongwa juu ya kuta zake na ngazi nane kuupandia.
И тремови им беху према спољашњем трему, и палме по довратницима, и уз осам басамака иђаше се к њима.
32 Kisha yule mtu akanileta hata kwenye ua wa ndani karibu na njia ya kaskazini na kulipima lango, ambalo lilikuwa na vipimo sawa kama malango mengine.
Потом ме одведе у унутрашњи трем к истоку, и измери врата, и беше иста мера;
33 Vyumba vyake, kuta, na matawa yalikuwa na kipima sawa kama cha malango, na kulikuwa na madirisha pande zote. Laango la ndani na matawa yake yalikuwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
И клети им и довратници и тремови беху исте мере; и беху прозори на њима и на тремовима њиховим унаоколо; у дужину беше педесет лаката, а у ширину двадесет и пет лаката;
34 Matawa yake yalielekea nje ya ua; ilikuwa na mitende pande zote za hiyo na ngazi nane za kuupandia.
И тремови им беху према спољашњем трему, и палме по довратницима и тамо и амо, и уз осам басамака иђаше се к њима.
35 Kisha huyo mtu akanileta hata lango la kaskazini na kulipima; likapimwa vivyo hivyo kama malango mengine.
Потом одведе ме на северна врата и измери их, и беху исте мере.
36 Vyumba vyake, kuta, na ukumbi vilipimwa sawa na malango mengine, na kulikuwa na madirisha pande zote. Njia ya lango na matao yake yalipimwa dhiraa hamsini urefu na upana dhiraa ishirini na tano.
Тако и клети им и довратници и тремови и прозори унаоколо; у дужину педесет лаката, а у ширину двадесет и пет лаката.
37 Tatawa lake lilielekea ua wa nje; ilikuwa na mitende pande zote za huo na ngazi nane kuupandia.
И довратници им беху према спољашњем трему, и палме по довратницима и тамо и амо, и уз осам басамака иђаше се к њима.
38 Kulikuwa na chumba pamoja na mlango karibu na kila lango la ndani. Hapa ndipo ambako walipooshea sadaka za kutekezwa.
И клети с вратима беху код довратника тих врата, онде се праху жртве паљенице.
39 Kulikuwa na meza mbili kila upande wa kila ukumbi, ambako sadaka ya kuteketezwa ilipochinjiwa, na pia sadaka ya dhambi na sadaka ya hatia.
А у трему од врата беху два стола с једне стране и два стола с друге стране да се на њима кољу жртве паљенице и жртве за грех и за кривицу;
40 Karibu na ukuta wa ua, kuelekea juu kwenye lango kuelekea kaskazini, kulikuwa na meza mbili. Pia kwa upande mwingine kulikuwa na meza mbili kwenye lango la ukumbi.
И на страни споља како се улази на северна врата беху два стола, и на другој страни у трему од истих врата беху два стола;
41 Kulikuwa na meza nne pande zote karibu na lango; wakachinja wanyama juu ya meza nane.
Четири стола беху с једне стране и четири с друге стране уз врата, осам столова, на којима се кољаше.
42 Kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, dhiraa moja na nusu urefu, dhiraa moja na nusu upana, na kimo dhiraa moja. Juu yake waliweka vyombo pamoja ambavyo walivichinjia sadaka za kuteketezwa kwa ajili ya sadaka.
А четири стола за жртву паљеницу беху од тесаног камена, у дужину подруг лакта, и подруг лакта у ширину а у висину један лакат, и на њима се остављаше оруђе којима се кољаху жртве паљенице и друге жртве.
43 Kulabu mbili ujazo wa kiganja urefu uliokuwa umeunganishwa katika ua pande zote, na nyama ya matoleo ilikuwa imewekwa juu ya meza.
И унутра беху куке с подланице свуда у наоколо, а на столове се меташе месо од жртава.
44 Karibu na lango la ndani, katika ua wa ndani, kulikuwa na vyumba vya waimbaji. Moja ya hivi vyumba kilikuwa upande wa kaskazini, na kingine kusini.
И споља пред вратима унутрашњим беху клети за певаче у унутрашњем трему; једне беху уз врата северна и гледаху према југу, а друге беху уз источна врата и гледаху према северу.
45 Kisha yule mtu akanambia, “Hiki chumba kinachoelekea kusini ni kwa ajili ya makuhani walio zamu katika hekalu.
Тада ми рече: Ове клети што гледају на југ јесу за свештенике који служе око дома;
46 Chumba kilichoelekea kaskazini kilikuwa kwa ajili ya makuhani waliokuwa zamu kwenye madhabahu. Hawa ni wana wa Sadoki ambaye huja humkaribia Yahwe kumtumikia; ambao ni miongoni mwa wana wa Lawi.”
А оне клети што гледају на север јесу за свештенике који служе код олтара; то су синови Садокови, који између синова Левијевих приступају ка Господу да Му служе.
47 Kisha akaupima ule ua-dhiraa mia moja urefu na dhiraa mia moja upana mraba, pamoja na madhabahu mbele ya nyumba.
Потом измери трем, и беше у дужину сто лаката и у ширину сто лаката, четвртаст; и олтар беше пред домом.
48 Kisha yule mtu akanileta hata kwenye varanda ya nyumba na kupima mwimo wa milango yake-ilikuwa dhiraa tano unene upande huu. Njia ya kuingilia yenyewe ilikuwa dhiraa kumi na nne, na kuta pande zote za huo zilikuwa dhraa tatu upana.
После ме одведе у трем од дома, и измери довратнике трему, и беше пет лаката отуд и пет лаката одовуд; а врата беху широка три лакта отуд и три лакта одовуд;
49 Urefu wa ukumbi ulikuwa dhiraa ishirini, na upana wake ulikuwa dhiraa kumi na moja. Kulikuwa na ngazi zilizokuwa zimepanda juu na nguzo zilizokuwa zimesimama pande zote za huo.
Дужина трему беше двадесет лаката, а ширина једанаест лаката, и уз басамаке се иђаше к њему, и ступови беху уз довратнике, један отуд и један одовуд.

< Ezekieli 40 >