< Ezekieli 40 >

1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa kuhamishwa kwetu mwanzoni mwa mwaka siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya mji kuchukuliwa-katika siku hiyo hiyo, mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu na alinichukua huko.
At the beginning of the year, on the tenth day of the month of the twenty-fifth year of our exile, (fourteenth years after Jerusalem had been captured), was the exact day that the Lord's power came over me and he took me there to the city.
2 Katika maono ya Mungu akanileta hata nchi ya Israeli. Akanileta kupumzika juu ya kila mlima mrefu sana; upande wa kusini kulikuwa na monekano kana kwamba majengo ya mji.
God took me to the country of Israel in vision and set me down on a very high mountain. On the south side of the mountain there were buildings that seemed to be a city.
3 Kisha akanileta huko. Tazama, kulikuwa na mtu! Mwonekano wake ulikuwa kama mwonekano wa shaba. Alikuwa na uzi wa kitani na mwanzi wa kupimia mkononi mwake, na alisimama katika lango la mji.
When he took me there I saw a man who looked like shining bronze. He was holding a linen cord and a measuring rod as he stood in the entrance way.
4 Huyo mtu akanambia, “Mwanadamu, tazama kwa macho yako na sikiliza kwa masikio yako, na elekeza moyo wako juu ya yote ninayokufunulia, kwa kuwa ulinileta hapa ili niweze kukufunulia haya wewe. Toa taarifa ya kila kitu utakachokiona kwa nyumba ya Israeli.
“Son of man,” he told me, “watch with your eyes, listen with your ears. Concentrate on everything I'm about to show you, because that's the reason you were brought here. You are to explain to the people of Israel what you've been shown, everything you see.”
5 Kulikuwa ukuta uliokuwa umezunguka eneo la hekalu. Urefu wa kipimo cha mwanzi katika mkono wa mtu ulikuwa dhiraa sita urefu, kila urefu wa dhiraa ulikuwa dhiraa moja na kipimo cha kiganja cha mkono urefu. Aliupima ukuta; ulikuwa kipimo cha mwanzi mmoja na ufito mmoja urefu.
I could see a wall that surrounded the Temple. The measuring rod the man was holding was six long cubits in length (a long cubit is a cubit plus a handbreadth). He measured the wall as six cubits thick and six cubits high.
6 Kisha akaenda hata kwenye lango la hekalu lililokuwa limeelekea mashariki. Akapanda ngazi na kuipima kizingiti cha lango-mwanzi mmoja upana.
Then he went up the steps of the east-facing gate. He measured the gate's threshold as six cubits deep.
7 Vyumba vya ulinzi vilikuwa kila mwanzi mmoja urefu na mwanzi mmoja upana; kulikuwa na dhiraa tano katika kila vyumba viwili, na kizingiti cha lango la hekalu karibu na tawa la hekalu kilikuwa mwanzi mmoja urefu.
Beyond that were alcoves that measured six cubits by six cubits, with five cubits between the alcoves. The threshold of the inside entrance facing the porch measured six cubits.
8 Akapima tawa la lango; ulikuwa mwanzi mmoja urefu.
Then he measured the entrance porch.
9 Akapima tawa la lango. Ilikuwa mwanzi mmoja kwenda chini. Mihimili ilikuwa dhiraa mbili upana. Hili lilikuwa tawa la lango kuelekea hekalu.
It was eight cubits deep, and its posts were two cubits thick. The entrance porch faced the Temple.
10 Kulikuwa na vyumba vitatu vya ulinzi pande zote za lango la mashariki, na yote yalikuwa na kipimo kile kile, na kuta zilizokuwa zimezigawanya zilikuwa na kipimo kile kile.
There were three alcoves on each side of the east gate entrance that all measured the same. The posts on each side also measured the same.
11 Kisha yule mtu akapima upana wa njia ya lango la kuingia-dhiraa kumi; na akapima urefu wa njia ya lango la kuingia-dhiraa kumi na tatu.
He measured the width of the entrance gateway as ten cubits. It was thirteen cubits long.
12 Akaupima ukuta uliokuwa mpaka mbele ya vyumba-dhiraa moja urefu. Vyumba vilipimwa dhiraa sita kila upande.
A wall one cubit high was in front of alcove, and the alcoves measured six cubits by six cubits.
13 Kisha akapima lango la njia kutoka kwenye paa ya chumba kimoja kuelekea chumba kingine-dhiraa ishirini na tano, kutoka lango la kuingia chumba cha kwanza kuelekea kile cha pili.
Then he measured the entrance gateway from the roof of one alcove to the roof of the one opposite. It was twenty-five cubits from one doorway to the opposite doorway.
14 Kisha akapima ukuta uliokuwa umeenda kati ya vyumba vya ulinzi-dhiraa sitini urefu; alipima kwa mbali na tawa la lango.
Then he measured the distance between the posts as sixty cubits. The gateway led all the way around to the courtyard.
15 Lango la kuingia kutoka lango la mbele kuelekea lango jingine la tawa la mwisho lilikuwa dhiraa hamsini.
It was fifty cubits from the gateway entrance to the far side of the inside porch.
16 Kulikuwa na madirisha yaliyokuwa yamefungwa kuelekea vyumba na kuelekea nguzo zake kati ya malango kuzunguka kote; na vivyo hivyo kwa mabaraza. Kulikuwa na madirisha pande zote za ndani, na kila mhimili ulikuwa umepambwa kwa mitende.
The alcoves and their pillars had narrow windows on all of the inside of the gateway. The porches also had windows on all of the inside. All the posts were decorated with palm tree designs.
17 Kisha huyo mtu akanileta hata ua wa nje mwa hekalu. Tazama, kulikuwa na vyumba, na kulikuwa na kibamba katika ua, pamoja na vyumba thelathini baada ya kibamba.
He took me into the outer courtyard. I saw rooms and a pavement had been constructed around the courtyard. There were thirty rooms facing the pavement.
18 Kibamba kilienda juu hata upande wa malango, na upana wake ulikuwa sawsawa na urefu wa malango. Hiki kilikuwa kibamba cha chini.
This was termed the lower pavement and it extended along the sides of the gateways and was the same length as them.
19 Kisha huyo mtu akapima umbali kutoka mebele ya lango la chini hata mbele ya lango la ndani; ilikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki, na sawasawa na upande wa kaskazini.
He measured the distance from the front of the lower gateway to the far side of the inner courtyard as one hundred cubits, both to the east side and the north.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango lililokuwa upande wa kaskazini mwa ua wa nje.
He also measured the length and width of the gateway of the outer courtyard that faced north.
21 Kulikuwa na vyumba vitatu pande zote za lango, na lango na matawa yake yalipimwa sawa na lango kubwa-dhiraa hamsini upana wote na dhiraa ishirini na tano upana.
Its three alcoves on both sides, its posts, and its porch all measured the same as the first gateway and was fifty cubits long and twenty-five cubits wide.
22 Madirisha yake, tawa, vyumba, na mitende yake vilikabiliana na lango ambalo linaloelekea mashariki. Ngazi saba kuupandia juu hata kwenye tawa lake.
Its windows, porch, and palm tree decorations were the same as those of the east-facing gate. It had seven steps leading up to it, with its porch facing them.
23 Kulikuwa na lango kwenye ua wa ndani mbele kuelekea mashariki; huyo mtu alipima kutoka lango moja hadi lango jingine-dhiraa mia moja umbali.
There was an entrance to the inner courtyard facing the north gate, just like the east gate. He measured the distance from the entrance to the gate as a hundred cubits.
24 Kisha huyo mtu akanileta hata kwenye lango la kuingia la kusini, na kuta zake na tawa vilipimwa sawa kama malango mengine ya nje.
He took me to the south side, and I saw a gateway that faced south. He measured its posts and its porch, and they measured the same as those previously.
25 Kulikuwa na madirisha yaliyofungwa katika lango la njia na tawa lake kama lile lango. Lango la kusini na tawa lake vilipimwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
Both the gateway and its porch had windows all around it that were like the other windows. It was fifty cubits long and twenty-five cubits wide.
26 Kulikuwa na ngazi saba hadi kwenye lango na matawa yake, na kulikuwa na mitende iliyochongoka juu ya kuta pande zote.
It had seven steps leading up to it, and its porch faced them. It had one post on each side with palm tree designs on them.
27 Kulikuwa na lango la ua wa ndani upande wa kusini, na yule mtu akapima kutoka hilo lango hata lango la kuingia upande wa kusini-dhiraa mia moja umbali.
The inner courtyard also had an entrance facing south, and he measured the distance from the entrance to the south gate as a hundred cubits.
28 Kishi huyo mtu akanileta hata ua wa ndani karibu na lango lake la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo vile vile kama malango mengine.
He took me into the inner courtyard through the south gate, and he measured the south gate. It measured the same as those previously.
29 Vyumba vyake, kuta, na matao vilipimwa sawa kama malango mengine; kulikuwa na madirisha kuzunguka matao yote. Lango la ndani na matao yake yalipimwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
Its alcoves, posts, and porch had the same measurements as those previously. The gateway and its porch had windows all around. It was fifty cubits long and twenty-five cubits wide.
30 Pia kulikuwa na matao pande zote za kuta za ndani; haya yalikuwa dhiraa ishirini na tano urefu na dhiraa tano upana.
(The other surrounding porches measured twenty-five cubits long and five cubits deep.)
31 Hili tawa lilielekea ua wa nje pamoja na mitende iliyochongwa juu ya kuta zake na ngazi nane kuupandia.
Its porch faced the outer courtyard, and its pillars were decorated with palm tree designs. It had eight steps leading up to it.
32 Kisha yule mtu akanileta hata kwenye ua wa ndani karibu na njia ya kaskazini na kulipima lango, ambalo lilikuwa na vipimo sawa kama malango mengine.
He took me to the inner courtyard on the east side. He measured the gateway and it measured the same as those previously.
33 Vyumba vyake, kuta, na matawa yalikuwa na kipima sawa kama cha malango, na kulikuwa na madirisha pande zote. Laango la ndani na matawa yake yalikuwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
Its alcoves, posts, and porch measured the same as those previously. The gateway and its porch had windows all around. It was fifty cubits long and twenty-five cubits wide.
34 Matawa yake yalielekea nje ya ua; ilikuwa na mitende pande zote za hiyo na ngazi nane za kuupandia.
Its porch faced the outer courtyard, and its posts were decorated with palm tree designs. It had eight steps leading up to it.
35 Kisha huyo mtu akanileta hata lango la kaskazini na kulipima; likapimwa vivyo hivyo kama malango mengine.
He took me to the north gate and measured it. It measured the same as those previously,
36 Vyumba vyake, kuta, na ukumbi vilipimwa sawa na malango mengine, na kulikuwa na madirisha pande zote. Njia ya lango na matao yake yalipimwa dhiraa hamsini urefu na upana dhiraa ishirini na tano.
including its alcoves, posts, and porch. The gateway and its porch had windows all around. It was fifty cubits long and twenty-five cubits wide.
37 Tatawa lake lilielekea ua wa nje; ilikuwa na mitende pande zote za huo na ngazi nane kuupandia.
Its porch faced the outer courtyard, and its posts were decorated with palm tree designs on all sides. It had eight steps leading up to it.
38 Kulikuwa na chumba pamoja na mlango karibu na kila lango la ndani. Hapa ndipo ambako walipooshea sadaka za kutekezwa.
A room with a doorway stood beside by the porch of the inner gateways. This was where the burnt offering was washed.
39 Kulikuwa na meza mbili kila upande wa kila ukumbi, ambako sadaka ya kuteketezwa ilipochinjiwa, na pia sadaka ya dhambi na sadaka ya hatia.
Inside the gateway porch were two tables on both sides, where the sacrificial animals were slaughtered for burnt offerings, sin offerings, and guilt offerings.
40 Karibu na ukuta wa ua, kuelekea juu kwenye lango kuelekea kaskazini, kulikuwa na meza mbili. Pia kwa upande mwingine kulikuwa na meza mbili kwenye lango la ukumbi.
Outside, on the way up to the entrance of the north gateway, were two tables on one side of the gate's porch and two tables on the other side.
41 Kulikuwa na meza nne pande zote karibu na lango; wakachinja wanyama juu ya meza nane.
So there were four tables on the inside the of gateway and another four outside, making a total of eight tables. This is where the sacrifices were slaughtered.
42 Kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, dhiraa moja na nusu urefu, dhiraa moja na nusu upana, na kimo dhiraa moja. Juu yake waliweka vyombo pamoja ambavyo walivichinjia sadaka za kuteketezwa kwa ajili ya sadaka.
There were also four tables of cut stone for the burnt offering. They each measured one and a half cubits long, one and a half cubits wide, and a cubit high. The tools used to slaughter the burnt offerings and the other sacrifices were placed on these tables.
43 Kulabu mbili ujazo wa kiganja urefu uliokuwa umeunganishwa katika ua pande zote, na nyama ya matoleo ilikuwa imewekwa juu ya meza.
Hooks measuring the width of a hand were attached to the walls inside the room. The meat of the offering was to be placed on the tables.
44 Karibu na lango la ndani, katika ua wa ndani, kulikuwa na vyumba vya waimbaji. Moja ya hivi vyumba kilikuwa upande wa kaskazini, na kingine kusini.
Outside the inner gate but inside the inner courtyard were two rooms. One was beside the north gate and faced south; the other beside the south gate and faced north.
45 Kisha yule mtu akanambia, “Hiki chumba kinachoelekea kusini ni kwa ajili ya makuhani walio zamu katika hekalu.
The man told me: “The room that faces south is for the priests in charge of the Temple,
46 Chumba kilichoelekea kaskazini kilikuwa kwa ajili ya makuhani waliokuwa zamu kwenye madhabahu. Hawa ni wana wa Sadoki ambaye huja humkaribia Yahwe kumtumikia; ambao ni miongoni mwa wana wa Lawi.”
and the room that faces north is for the priests in charge of the altar. These priests are the descendants of Zadok and are the only Levites who are allowed to come near to the Lord and minister before him.”
47 Kisha akaupima ule ua-dhiraa mia moja urefu na dhiraa mia moja upana mraba, pamoja na madhabahu mbele ya nyumba.
He measured the square courtyard: a hundred cubits long and a hundred cubits wide. The altar stood in the courtyard in front of the Temple.
48 Kisha yule mtu akanileta hata kwenye varanda ya nyumba na kupima mwimo wa milango yake-ilikuwa dhiraa tano unene upande huu. Njia ya kuingilia yenyewe ilikuwa dhiraa kumi na nne, na kuta pande zote za huo zilikuwa dhraa tatu upana.
He took me to the Temple porch and measured the pillars of the porch as five cubits on each side. The gateway was fourteen cubits wide and its sides measured three cubits.
49 Urefu wa ukumbi ulikuwa dhiraa ishirini, na upana wake ulikuwa dhiraa kumi na moja. Kulikuwa na ngazi zilizokuwa zimepanda juu na nguzo zilizokuwa zimesimama pande zote za huo.
The porch was twenty cubits wide and twelve cubits deep, and had ten steps leading up to it. There were columns by the posts, one on both sides.

< Ezekieli 40 >