< Ezekieli 39 >

1 “Kisha wewe, mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! ni kinyume nawe, Gogu, mkuu wa Mesheki na Tubali.
“And you, son of man, prophesy concerning Gog, and you have said, Thus said Lord YHWH: Behold, I [am] against you, O Gog, Chief prince of [[or prince of Rosh, ]] Meshech and Tubal,
2 Nitakugeuza na kukuongoza; nitakupandisha juu kutoka mbali kaskazini na kukuleta hata milima ya Israeli.
And have turned you back, and enticed you, And caused you to come up from the sides of the north, And brought you in against mountains of Israel,
3 Kisha nitaufunga upinde wako utoke katika mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale kuanguka kutoka kwenye mkono wako wa kuume.
And have struck your bow out of your left hand, Indeed, I cause your arrows to fall out of your right.
4 Utaanguka juu ya milima ya Israeli-wewe na jeshi lako late na maaskari walio pamoja nawe. Nitawapatia ndege mbua na wanyama pori wa mashambani kwa ajili ya chakula.
You fall on mountains of Israel, You, and all your bands, and the peoples who [are] with you, To ravenous bird—a bird of every wing, And [to] a beast of the field, I have given you for food.
5 Utaanguka juu ya uso wa shamba, kwa kuwa mimi mwenyewe nimesema hivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
You fall on the face of the field, for I have spoken, A declaration of Lord YHWH.
6 Kisha nitapeleka moto juu ya Magogu na kwa wale waishio salama juu ya pwani, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.
And I have sent a fire against Magog, And against the confident inhabitants of the islands, And they have known that I [am] YHWH.
7 Kwa kuwa nitalifanya jina langu takatifu lijulikane kati ya watu wangu Israeli, na sitaruhusu tena jina langu takatifu litukanwe; mataifa watajua kwamba mimi ni Yahwe, Mtakatifu katika Israeli.
And I make My holy Name known in the midst of My people Israel, And I do not defile My holy Name anymore, And the nations have known that I, YHWH, the Holy One, [am] in Israel.
8 Tazama! Siku inakuja, na itachukua nafasi-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
Behold, it has come, and it has been done, A declaration of Lord YHWH, It [is] the day of which I spoke.
9 Hao wakaao katika miji ya Israeli watatoka nje na watatumia silaha kuwasha moto na kutengeneza moto na kuwachoma-ngao ndogo, ngao kubwa, pinde, mishale, rungu, na mikuki; watatengeneza mioto pamoja nao kwa muda wa siku saba.
And those dwelling [in the] cities of Israel have gone out, And they have burned and kindled [a fire], With armor, and shield, and buckler, With bow, and with arrows, And with hand weapon, and with javelin, And they have caused a fire to burn seven years with them,
10 Hawatakusanya kuni kutoka mashambani wala kukata miti kutoka kwenye misitu, kwa kuwa watazichoma hizo silaha; watawateka nyara wale watakaotaka kuwateka nyara-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
And they do not take wood out of the field, Nor do they hew out of the forests, For they cause the fire to burn with armor, And they have spoiled their spoilers, And they have plundered their plunderers, A declaration of Lord YHWH.
11 Kisha itakuwa katika hiyo siku ambayo nitaifanya sehemu huko kwa ajili ya Gogu-kaburi la Israeli, bonde kwa ajili ya wale wanaosafiri hata mashariki ya bahari. Litawazuia wale wanaotegemea kupita. Huko watamzika Gogu pamoja na kundi lake lote. Watapaita bonde la Hamon-Gogu.
And it has come to pass in that day, I give a place to Gog there—a grave in Israel, the valley of those passing by, east of the sea, and it is stopping those passing by, and they have buried there Gog, and all his multitude, and have cried, O valley of the multitude of Gog!
12 Kwa muda wa siku saba nyumba ya Israeli itawazika ili kuitakasa nchi.
And the house of Israel has buried them—in order to cleanse the land—seven months.
13 Kwa kuwa watu wa nchi watawazika; itakuwa siku ya kukumbukwa kwao wakati nitakapotukuzwa-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
Indeed, all the people of the land have buried them, and it has been to them for a name—the day of My being honored—a declaration of Lord YHWH.
14 Kisha watawateua watu kuendelea kwenda kwenye nchi, kuwatafuta wale waliokuwa wakisafiri, lakini waliokufa na miili yao kubaki juu ya uso wa nchi, ili kwamba waweze kuwazika, kwa ajili ya kusafisha nchi. Katika siku ya mwisho ya mwezi wa saba wataanza kutafuta.
And they separate men for continual employment, with those passing through, passing on through the land, burying those who are left on the face of the earth, to cleanse it. At the end of seven months they search.
15 Kama hawa watu wapitao kwenye nchi, watakapoona mfupa wowote wa binadamu, wataweka alama kwa huo, hadi wachimba kaburi watakapokuja na kuizika katika bonde la Hamoni Gogu.
And those passing by have passed through the land, and seen a bone of man, and one has constructed a sign near it until those burying have buried it in the valley of the multitude of Gog.
16 Kutakuwa na mji huko unaitwa Hamona. Wataitakasa nchi kwa njia hii.
And also the name of the city [is] The Multitude; and they have cleansed the land.
17 Kwako wewe, mwanadamu, Bwana Yahwe asema hivi: Waambie ndege wote wenye mabawa na wanyama wote wa porini katika mashamba, 'Kusanyikeni pamoja na mje. Kusanyikeni kutoka pande zote kwenda kwenye dhabihu yote ambayo mimi mwenyewe ninayoifanya kwa ajili yako, dhabihu kubwa juu ya milima ya Israeli, ili kwamba mle nyama na kunywa damu.
And you, son of man, thus said Lord YHWH: Say to the bird—every wing, and to every beast of the field: Be assembled and come in, Be gathered from all around, For My sacrifice that I am sacrificing for you, A great sacrifice on mountains of Israel, And you have eaten flesh, and drunk blood.
18 Mtakula nyama ya walio hodari na kunywa damu ya wakuu wa dunia; watakuwa kondoo waume, wana kondoo, mbuzi, na ng'ombe, wote walikuwa wanene katika Basheni.
You eat [the] flesh of [the] mighty, And you drink [the] blood of [the] princes of the earth, Of rams, of lambs, and of male goats, Of calves, fatlings of Bashan—all of them.
19 Kisha mtakula mafuta hata kuridhika kwenu; mtakunywa damu hadi kulewa; hii itakuwa dhabihu nitakayoichinja kwa ajili yenu.
And you have eaten fat to satiety, And you have drunk blood—to drunkenness, Of My sacrifice that I sacrificed for you.
20 Mtatosheka kwenye meza yangu pamoja na farasi, magari ya farasi, shujaa, na kila mtu wa vita-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
And you have been satisfied at My table with horse and rider, Mighty man, and every man of war, A declaration of Lord YHWH.
21 Nitauweka utukufu wangu kati ya mataifa, na mataifa yote yataona hukumu yangu ninayoionyesha na mkono wangu nimeuweka juu yao.
And I have given My glory among nations, And all the nations have seen My judgment that I have done, And My hand that I have laid on them.
22 Nyumba ya Israeli itajua yakwamba mimi ni Yahwe Mungu wao kutoka hiyo siku na kuendelea.
And the house of Israel has known that I [am] their God YHWH, From that day and from now on.
23 Mataifa yatajua kwamba nyumba ya Israeli wameenda uhamishoni kwa sababu ya udhalimu wao kwa kunisaliti, hivyo naficha uso wangu kwao na kuwaweka kwenye mkono wa maadui zao ili kwamba wote waanguke kwa upanga.
And the nations have known That the house of Israel was removed for their iniquity, Because they have trespassed against Me, And I hide My face from them, And give them into the hand of their adversaries, And they fall by sword—all of them.
24 Nimewafanyia kutokana na uchafu wao na dhambi zao, nitakapokuwa nimeuficha uso wangu kwao.
According to their uncleanness, And according to their transgressions, I have done with them, And I hide My face from them.
25 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Sasa nitawarudisha watu wa Yakobo, na kuwa na huruma juu ya nyumba yote ya Israeli, wakati nitakapoona wivu kwa ajili ya jina langu.
Therefore, thus said Lord YHWH: Now I bring back the captivity of Jacob, And I have pitied all the house of Israel, And have been zealous for My holy Name.
26 Kisha watabeba aibu yao na uhaini mkubwa walio nihaini. Watayasahau haya yote watakapopumzika katika nchi yao katika usalama, wala hakuna mtu atakaye waogofya.
And they have forgotten their shame, And all their trespass that they trespassed against Me, In their dwelling on their land confidently and none troubling.
27 Wakati nitakapokuwa nimewarudisha kutoka kwa watu na kuwakusanya kutoka kwenye nchi za maadui zao, nitajionyesha mimi mwenyewe kuwa mtakatifu kwenye uso wa mataifa mengi.
In My bringing them back from the peoples, I have assembled them from the lands of their enemies, And I have been sanctified in them before the eyes of the many nations,
28 Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe Mungu wao, kwa kuwa nimewapeleka utumwani kati ya mataifa, lakini kisha nitawakusanya kuwarudisha hata nchi yao. Sitamuacha hata mmoja wao kati ya mataifa.
And they have known that I [am] their God YHWH, In My removing them to the nations, And I have gathered them to their land, And I leave none of them there anymore.
29 Sitawaficha uso wangu kwao wakati nitakapomwaga Roho wangu katika nyumba ya Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
And I do not hide My face from them anymore, In that I have poured out My Spirit on the house of Israel, A declaration of Lord YHWH!”

< Ezekieli 39 >