< Ezekieli 38 >
1 Neno la Yahwe likanijia, likisema,
And the word of Jehovah came to me, saying:
2 “Mwanadamu, weka uso wako kumwelekea Gogu, nchi ya Magogu, kiongozi mkuu wa Mesheki na Tubali; na kutabiri dhidi yake.
Son of man, set thy face against Gog, of the land of Magog, prince of Resh, Meshech, and Tubal, and prophesy against him,
3 Sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Ni juu yako, Gogu, kiongozi mkuu wa Mesheki na Tubali.
and say, Thus saith the Lord Jehovah: Behold, I am against thee, O Gog, prince of Resh, Meshech, and Tubal!
4 Hivyo nitakugeuza na kuweka kulabu kwenye taya yako; nitakupeleka nje pamoja na jeshi lako lote, farasi, na waendesha farasi, wote wakiwa wamevaa silaha, kusanyiko kubwa pamoja na ngao ndogo na ngao kubwa, wote wakishikilia panga!
And I will turn thee about, and put rings into thy jaws; and I will bring thee forth, thee and all thine army, horses and horsemen, all of them clothed in gorgeous apparel, even a great multitude with bucklers and shields, all of them handling swords.
5 Persia, Kushi, Uajemi wapo pamoja nao, wote pamoja na ngao na chapeo!
Persians, Ethiopians, and Lybians are with them, all of them with shields and helmets.
6 Gomeri na jeshi lake lote, na Beth-Togarma, kutoka sehemu za mbali ya kaskazini, na jeshi lake lote! Watu wengi wako pamoja nawe!
Gomer and all his bands, the house of Togarmah from the north quarters, and all their hosts, many nations are with thee.
7 Kuwa tayari! Ndio, jiandae na jeshi lako waliokusanyika pamoja na wewe, na amiri wao mkuu.
Be prepared, and prepare for thyself, thou and all thy host that are assembled unto thee, and be thou their leader!
8 Utaitwa baada ya siku nyingi, na baada ya miaka michache utaenda kwenye nchi iliyofunikwa kutoka upanga na ambayo iliyokusanywa kutoka watu wengi, iliyowkusanya kuwarudisha milima ya Israeli ambayo imeendelea kuangamizwa. Lakini watu wa nchi watatolewa na kabila za watu, na wataishi salama, wote!
After many days shalt thou be appointed over them. In the latter years shalt thou come into a land that is brought back from the sword, gathered out of many nations upon the mountains of Israel, which had been long desolate; but it is brought forth out of the nations, and they shall dwell securely, all of them.
9 Hivyo utapanda juu kama tufani iendavyo; utakuwa kama wingu lililofunika nchi, wewe na jeshi lako lote, maaskari wako wote pamoja na wewe.
Thou shalt go up like a storm, thou shalt come like a cloud, to cover the land, thou and all thy bands, and many nations with thee.
10 Bwana Yahwe asema hivi: Itakuwa siku hiyo hayo mawazo yataingia moyoni mwako, na utatunga njama mbaya.'
Thus saith the Lord Jehovah: At the same time shall thoughts come into thy mind, and thou shalt meditate an evil design,
11 Kisha utasema, 'nitapanda hata nchi iliyowazi; nitaenda hata kwa watu wapole waishio salama, wote wakiishi mahali ambapo hakuna kuta wala makomeo, na mahali ambapo hakuna malango ya mji.
and shalt say, “I will go up to the land of unwalled villages; I will go to them that are at rest, that dwell securely, all of them dwelling without walls, and having neither bars nor gates,
12 Nitanyakua mateka na kuiba mateka, ili nilete mkono wangu juu kuwaangamiza wale wakazi wapya, na juu ya watu waliokusanyika kutoka mataifa, watu wale waongezao wanyama na mali, na wale waishio katikatika ya dunia.'
to take a spoil and to divide a prey, to turn my hand against the desolated places that have become inhabited, and against a people gathered out of the nations, possessing cattle and goods, dwelling in the heights of the earth.”
13 Sheba na Denani, na wafanya biashara wa Tarshishi pamoja na mahodari wake wote watakwambia, 'Je, umekuja kuteka nyara? Je, umewakusanya majeshi yako kuchukua mateka, kuchukua fedha na dhahabu, kuchukua mifugo yao na mali na kuwakokota mateka wengi sana?'
Sheba, and Dedan, and the merchants of Tarshish, and all the chiefs thereof, shall say to thee, “Art thou come to take a spoil? Hast thou gathered thy company to divide a prey? to carry away silver and gold, to take away cattle and goods, and to divide great spoil?”
14 Kwa hiyo tabiri, mwanadamu, na mwambie Gogu, 'Bwana Yahwe asema hivi: Katika siku hiyo, wakati watu wangu Israeli watakapoishi salama, je, hutajifunza kuhusu wao?
Therefore prophesy, son of man, and say to Gog, Thus saith the Lord Jehovah: In that day when my people Israel dwelleth securely, thou shalt observe it,
15 Utakuja kutoka mahali pangu mbali katika kaskazini pamoja na jeshi kubwa, wote wakiendesha farasi, kusanyiko kubwa, jeshi kubwa.
and thou shalt come up from the regions of the North, thou and many nations with thee, all of them riding upon horses, a great company, and a mighty host;
16 Utawashambulia watu wangu Israeli kama wingu lifunikavyo nchi. Katika siku za baadaye nitakuleta juu ya nchi yangu, ili mataifa wanijue nitakapojifunua mwenyewe kupitia wewe, Gogu, kuwa mtakatifu mbele ya macho yao.
thou shalt come up against my people Israel like a cloud, to cover the land; in the latter days it shall come to pass, that I will bring thee against my land, that the nations may know me, when I shall be sanctified in regard to thee, before their eyes, O Gog!
17 Bwana Yahwe asema hivi: Je, wewe siye yule ambaye niliyeongea naye katika siku za zamani kwa mkono wa watumishi wangu, manabii wa Israeli, waliotabiri katika mda wao wenyewe kwa miaka niliyowaleta juu yao?
Thus saith the Lord Jehovah: Art thou not he of whom I spoke in old time by my servants, the prophets of Israel, who prophesied in those days and years, that I would bring thee against them?
18 Basi itakuwa katika siku hiyo wakati Gogu atakapo ishambulia nchi ya Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-ghadhabu yangu itapanda katika hasira yangu.
And it shall come to pass in that day, in the day when Gog shall come against the land of Israel, saith the Lord Jehovah, that my anger shall ascend in fury.
19 Katika wivu wangu katika hasira ya moto wangu, ninasema kwamba katika siku hiyo kutakuwa na tetemeko kubwa la nchi katika nchi ya Israeli.
For in my jealousy, in the fire of my wrath, have I spoken, Surely in that day there shall be a great shaking in the land of Israel,
20 Watatetemeka mbele yangu-samaki wa baharini na ndege wa angani, wanyama wa mashambani, na viumbe watambaao juu ya nchi, na kila mtu aliyeko juu ya uso wa nchi. Milima itaangushwa chini majabali yataanguka, hadi kila ukuta utaanguka kwenye nchi.
so that the fishes of the sea, and the birds of the heavens, and the beasts of the field; and every creeping thing that creepeth upon the ground, and all the men that are upon the face of the earth, shall shake at my presence; and the mountains shall be thrown down, and the steep places shall fall, and every wall shall fall to the ground.
21 Nitaita upanga dhidi yake juu ya milima yangu yote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-upanga wa kila mtu utakuwa kinyume na ndugu yake.
And I will call for a sword against him throughout all my mountains, saith the Lord Jehovah, and they shall all turn their swords against each other,
22 Kisha nitamuhukumu kwa tauni na damu; nakufurika mvua na mvua ya mawe na kuchoma asidi nitainyeshea chini juu yake na jeshi lake na mataifa mengi yaliyo pamoja naye.
And I will contend against him with pestilence, and with blood; and overflowing showers, and great hailstones, fire and brimstone, will I rain upon him and his hosts, and the many nations that are with him.
23 Kwa kuwa nitaonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu na nitafanya kujulikana mimi mwenyewe katiaka macho ya mataifa mengi, na watajua kwamba mimi ni Yahwe.”
Thus will I show myself in my greatness and glory, and make myself known before the eyes of many nations, and they shall know that I am Jehovah.