< Ezekieli 37 >

1 Mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu, na akanitoa kwa Roho wa Bwana Yahwe na kuniweka chini katikati ya bonde; lilikuwa limejaa mifupa.
Et la main du Seigneur fut sur moi, et le Seigneur me ravit en esprit; et il me déposa au milieu d'un champ, et ce champ était rempli d'ossements humains.
2 Kisha akanifanya kupita kati yao kuizunguka pande zote. Tazama! Mingi yao mikubwa ilikuwa katika bonde! Ilikuwa mikavu sana.
Et le Seigneur me conduisit tout autour de ces os, et voilà qu'il y en avait une multitude sur la surface du champ, et ils étaient tout desséchés.
3 Akanambia, “Mwanadamu, Je! Hii mifupa inaweza kuishi kinyume?” Hivyo nikasema, “Bwana Yahwe, wajua wewe pekee.”
Et le Seigneur me dit: Fils de l'homme, ces os revivront-ils? Et je répondis: Seigneur, Seigneur, vous le savez.
4 Kisha akanambia, “Tabiri juu ya hii mifupa na iambie, 'Mifupa mikavu. Lisikilizeni neno la Yahwe.
Et il me dit: Prophétise sur ces ossements, et dis-leur: Ossements desséchés, écoutez la parole du Seigneur.
5 Bwana Yahwe asema hivi kwenye hii mifupa: Tazama! nakaribia kuweka pumzi juu yenu, nanyi mtaishi.
Or voici ce que dit le Seigneur à ces ossements: Je vais amener sur vous un souffle de vie,
6 Nitaweka mishipa juu yenu na kuleta nyama juu yenu. Nitawafunika kwa ngozi na kuweka pumzi ndani yenu hivyo mtaishi. Kisha mtajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
Et je poserai sur vous des nerfs, et j'amènerai sur vous des chairs, et sur vous j'étendrai de la peau, et je mettrai en vous mon souffle, et vous vivrez, et vous saurez que je suis le Seigneur.
7 Hivyo nimetoa unabii kama nilivyokuwa nimeamriwa: nimetabiri, tazama, sauti ikaja, iliyokuwa ya mtetememo. Kisha mifupa ikasogeleana pamoja-mfupa juu ya mfupa.
Et je prophétisai comme le Seigneur me l'avait prescrit, et ceci advint pendant que je prophétisais: Voilà que les ossements s'agitèrent et vinrent se placer chacun dans sa jointure.
8 Nikatazama na, kumbe, mishipa ilikuwa juu sasa, na nyama ikatoka juu na ngozi ikazifunika. Lakini hapakuwa na pumzi juu yao.
Et je regardai; et voilà que sur les os des nerfs et des chairs se produisirent, et de la peau les recouvrit; mais l'esprit n'était pas encore en eux.
9 Kisha Yahwe akanambia, “Itabirie pumzi, tabiri, mwanadamu, na iambie pumzi, 'Bwana Yahwe asema hivi: Pumzi, hutoka pepo nne, na pumzi juu ya hawa walioawa, hivyo wanaweza kuishi.”'
Et le Seigneur me dit: Prophétise à l'esprit, prophétise, fils de l'homme, et dis à l'esprit: Voici ce que dit le Seigneur: Viens des quatre vents, et souffle dans ces morts, et qu'ils vivent.
10 Hivyo nimetabiri kama nilivyokuwa nimeamriwa; pumzi ikawajilia na wakaishi. Kisha wakasimama kwa miguu yao, jeshi moja kubwa sana.
Et je prophétisai comme le Seigneur me l'avait prescrit, et l'esprit entra dans les morts, et ils furent vivants, et ils se dressèrent sur leurs pieds en immense multitude.
11 Kisha Yahwe akanambia, “Mwanadamu, mifupa hii yote ni ya nyumba ya Israeli. Tazama! Wanasema, 'Mifupa yetu imekauka, na tumaini letu limepotea. Tumekatwa.'
Et le Seigneur me parla, disant: Fils de l'homme, ces os sont toute la maison d'Israël, et eux-mêmes disent: Nos ossements sont desséchés, notre espérance a péri, et nous sommes sans voix.
12 Kwa hiyo tabiri na waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Nitayafunua makabiri yenu na kuwapandisha kutoka kwayo, watu wangu. Nitakurudisha hata katika nchi ya Israeli.
À cause de cela, prophétise et dis: Voilà que j'ouvre vos sépulcres, dit le Seigneur; je vais vous en faire sortir, et je vous introduirai en la terre d'Israël;
13 Kisha mtajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapo yafunua makaburi yenu na kuwatoa kutoka kwao, watu wangu.
Et vous saurez que moi je suis le Seigneur, quand j'aurai ouvert vos sépulcres, et que de ces sépulcres j'aurai tiré mon peuple.
14 Nitaweka Roho wangu ndani yenu hivyo mtaishi, na nitawafanya kupumzika katika nchi yenu mtakapojua yakwamba mimi ni Yahwe. Nasema na nitayafanya hayo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
Et je vous donnerai mon esprit, et vous vivrez, et je vous établirai sur votre terre, et vous saurez que je suis le Seigneur. J'ai parlé, et j'exécuterai, dit le Seigneur.
15 Kisha neno la Yahwe likanijia, likisema,
Et la parole du Seigneur me vint, disant:
16 “Sasa wewe, mwanadamu, chukua fimbo moja kwa ajili yako na andika juu yake, 'Kwa ajili Yuda na kwa ajili ya watu wa Israeli, wenzake,' Kisha fimbo nyingine andika juu yake, 'Kwa kuwa Yusufu, tawi la Efraimu, na kwa ajili ya watu wa Israeli, wenzake.
Fils de l'homme, prends une baguette, et sur elle écris: Juda et tous les enfants d'Israël de son parti. Prends une autre baguette, et écris sur elle: Pour Joseph; puis une baguette pour Ephraïm; inscris enfin tous les enfants appartenant à Israël.
17 Walete wote pamoja kwenye fimbo moja, ili wawe kitu kimoja katika mkono wako.
Et tu les réuniras ensemble pour n'être qu'une baguette, après les avoir liées, et elles seront dans ta main.
18 Wakati watu wako watakapokwambia na kusema, 'Je! hutatuambia haya mambo yako yana maana gani?'
Et ceci adviendra: Lorsque les enfants de ton peuple te diront: Ne nous expliqueras-tu point ce que cela signifie?
19 kisha waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Nalichukua tawi la Yusufu ambalo lipo kwenye mkono wa Efraimu na kabila za Israeli wenzake na kuungana nalo hata kwenye tawi la Yuda, ili kwamba wawe tawi moja, na watakuwa kitu kimoja katika mikono yangu.'
Tu leur diras: Ainsi parle le Seigneur: Voilà que je vais prendre la tribu de Joseph, qui est dans la main d'Éphraïm, et les tribus d'Israël qui appartiennent à celle-ci, et je les réunirai à la tribu de Juda, et elles ne formeront qu'une baguette dans la maison de Juda.
20 Shika kwenye mkono wako na matawi uliyoandika mbele ya macho yao.
Et les baguettes sur lesquelles tu as écrit seront en ta main en présence du peuple.
21 Waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! nakaribia kuwachukua watu wa Israeli kutoka miongoni mwa mataifa walipoenda. Nitawakusanya kutoka nchi zilizozunguka na nitawaleta kwenye nchi yao.
Et tu leur diras: Ainsi parle le Seigneur Maître: Voilà que je vais retirer toute la maison d'Israël du milieu des nations où elle est entrée; je les rassemblerai d'entre toutes les contrées d'alentour, et je les ramènerai en la terre d'Israël.
22 Nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi, juu ya milima ya Israeli, na kutakuwa na mfalme mmoja kama mfalme juu yao wote, na hawatakuwa mataifa mawili tena. Hawatagawanyika kwenye falme mbili tena.
Et j'en ferai une nation dans la terre qui m'appartient et sur les montagnes d'Israël. Et il y aura pour eux un seul prince, et ils ne formeront plus deux nations, et ils ne seront plus jamais divisés en deux royaumes,
23 Kisha hawatajitia unajisi tena kwa sanamu zao, mambo yao yachukizao, au dhambi zao nyingine. Kwa kuwa nitawaokoa kutoka matendo yao ya uongo ambayo wamefanya dhambi, na nitawatakasa, hivyo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
Afin de ne plus se souiller de leurs idoles; et je les préserverai de tous les dérèglements où ils sont tombés, et je les purifierai; et ils seront mon peuple, et moi, le Seigneur, je serai leur Dieu.
24 Daudi mtumishi wangu atakuwa mfalme juu yao. Hivyo kutakuwa na mchungaji mmoja juu yao wote, na wataishi kulingana na sheria zangu na watazitunza amri zangu na kuzitii.
Et mon serviteur David sera prince au milieu d'eux; y aura pour eux tous un seul pasteur, parce qu'ils marcheront dans la voie de mes ordonnances et qu'ils garderont mes commandements et les pratiqueront.
25 Wataishi katika nchi niliwapatia watumishi wangu Yakobo, ambapo baba zenu walipoishi. Wataishi humo milele-wao, watoto wao, na wajukuu zao, kwa Daudi mtumishi wangu atakuwa mkuu wao milele.
Et ils habiteront leur terre que j'ai donnée à mon serviteur Jacob, que leurs pères ont habitée; et eux-mêmes y habiteront. Et David, mon serviteur, sera leur prince dans tous les siècles.
26 Nitaweka agano la amani pamoja nao. Litakuwa agano la milele pamoja nao. Nitawaweka na kuwazidisha na kupaweka mahali patakatifu pangu katikati yao milele.
Et je ferai avec eux une alliance de paix; et mon alliance avec eux sera éternelle. Et j'établirai au milieu d'eux mon sanctuaire dans tous les siècles.
27 Maskani yangu yatakuwa pamoja nao; Nitakuwa Mungu wao, na watakuwa watu wangu.
Et mon tabernacle sera chez eux, et je serai leur Dieu; et ils seront mon peuple.
28 Kisha mataifa watajua yakwamba mimi ni Yahwe niliyewatenga Israeli, wakati mahali pangu patakatifu patakapokuwa katikati yao milele.”
Et les nations sauront que je suis le Seigneur qui sanctifie les fils d'Israël, en établissant chez eux mon sanctuaire pour tous les siècles.

< Ezekieli 37 >